LGE2024 Matukio Yaliyojiri Kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga - Novemba 27, 2024

LGE2024 Matukio Yaliyojiri Kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga - Novemba 27, 2024

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Tanga.jpg

HISTORIA YA MKOA
Mkoa wa Tanga ni moja kati ya mikoa 31wenye eneo la 27,348 km² na upo Kaskazini Mashariki mwa Tanzania ukipakana na Kenya upande wa Kaskazini, Bahari Hindi upande wa mashariki na mikoa yaTANGA Morogoro, Manyara na Kilimanjaro. Mpaka upande wa kusini unafuata mto wa Mligaji. Mkoa wa Tanga unaunganisha sehemu za pwani pamoja na milima ya ndani kama Usambara.

Tanga inasemekana imeanzishwa na wafanyabiashara Waajemi katika karne ya 14 baada ya kristo, Baada ya kuanzishwa kwa ukoloni wa Kijerumani (DOA) mji ulikuwa makao makuu ya mkoa wa Tanga.

Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 yanaonesha kuwa idadi ya watu katika Mkoa wa Tanga ni 2,615,597; wanaume 1,275,665 na wanawake 1,339,932.

SOMA PIA

MUHTASARI WA MAENEO YA UTAWALA, MKOA WA TANGA
Mkoa wa Tanga ni moja ya mikoa ya kaskazini mwa Tanzania, ukiwa na mfumo wa utawala unaojumuisha mamlaka za miji na wilaya. Mkoa huu umejigawa katika maeneo tofauti ya kiutawala kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi na kusimamia maendeleo.

Tanga.PNG

Chanzo: TAMISEMI
Mamlaka za Miji
Kwenye upande wa mamlaka za miji;

1. Mji wa Handeni una kata 12 na mitaa 60.
2. Mji wa Korogwe una kata 11 na mitaa 29.
3. Jiji la Tanga lina kata 27 na mitaa 181.

Jumla kwa mamlaka hizi za miji ni kata 50 na mitaa 270.

Mamlaka za Wilaya
Kwa mamlaka za wilaya, kuna wilaya nane ambazo zinasimamia maeneo ya vijijini.

1. Wilaya ya Bumbuli ina kata 18, vijiji 83, na vitongoji 673.
2. Wilaya ya Handeni ina kata 21, vijiji 91, na vitongoji 770
3. Wilaya ya Kilindi ina kata 21, vijiji 102, na vitongoji 611.
4. Wilaya ya Korogwe ina kata 29, vijiji 118, na vitongoji 610.
5. Wilaya ya Lushoto ina kata 33, vijiji 125, na vitongoji 942.
6. Wilaya ya Mkinga ina kata 22, vijiji 85, na vitongoji 335.
7. Wilaya ya Muheza ina kata 37, vijiji 126, na vitongoji 494
8. Wilaya ya Pangani ina kata 14, vijiji 33, na vitongoji 96.

Kwa ujumla, wilaya za mkoa wa Tanga zina jumla ya kata 195, vijiji 763, na vitongoji 4,531, wakati mamlaka za miji zina kata 50 na mitaa 270.

Mkoa wa Tanga unafikia jumla kuu ya kata 245, mitaa 270, vijiji 763, na vitongoji 4,531, ukionyesha muundo wa utawala unaolenga kuleta uwiano mzuri kati ya maeneo ya mijini na vijijini katika utoaji wa huduma na maendeleo ya kijamii.

MAJIMBO YA KIUCHAGUZI
Mkoa wa Tanga una jumla ya majimbo 12 ya kiuchaguzi. Majimbo haya ni Tanga Mjini, Muheza, Pangani, Korogwe Mjini, na Korogwe Vijijini. Pia kuna majimbo ya Handeni Mjini, Handeni Vijijini, na Kilindi, ambayo yanapatikana katika maeneo ya katikati ya mkoa. Vilevile, majimbo ya Lushoto, Mkinga, Mlalo na Bumbuli yanakamilisha idadi ya majimbo ya kiuchaguzi katika mkoa huu.

HALI YA KISIASA
Mkoa wa Tanga ni miongoni mwa mikoa ambayo kwa kiwango kikubwa nafasi za uongozi katika ngazi za serikali za mitaa, udiwani na ubunge zinashikiliwa na Chama cha Mapinduzi CCM ambapo hali hiyo ilisababishwa na uchaguzi wa serikali za Mitaa mwaka 2019 na uchaguzi mkuu 2020.

uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 uliwapitisha bila kupingwa wagombea wa CCM huku mikoa mingine ambayo wagombea wake walipita bila kupingwa ni Katavi, Ruvuma na Njombe

Katika uchaguzi wa serikali za mitaa watia nia wa nafasi za uongozi katika nafasi hizo kutoka vyama vya upinzani walienguliwa kwa madai ya kukosa sifa za kugombea nafasi hizo na hivyo kupelekea kuondoa ushindani katika uchaguzi huo na kuacha wagombea wa Chama tawala CCM kupita bila kupingwa.

Kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024, inatarajiwa kuwepo kwa mabadiliko na uimarishwaji wa demokrasia ili kutoa nafasi kwa vyama vyote kushiriki kikamilifu kwa uhuru na haki katika uchaguzi huo ili kutoa fursa kwa wananchi wote wenye mitazamo na milengo tofauti kugombea nafasi hizo.

MATUKIO KUELEKEA NOVEMBA 27
 

HISTORIA YA MKOA
Mkoa wa Tanga ni moja kati ya mikoa 31wenye eneo la 27,348 km² na upo Kaskazini Mashariki mwa Tanzania ukipakana na Kenya upande wa Kaskazini, Bahari Hindi upande wa mashariki na mikoa yaTANGA Morogoro, Manyara na Kilimanjaro. Mpaka upande wa kusini unafuata mto wa Mligaji. Mkoa wa Tanga unaunganisha sehemu za pwani pamoja na milima ya ndani kama Usambara.

Tanga inasemekana imeanzishwa na wafanyabiashara Waajemi katika karne ya 14 baada ya kristo, Baada ya kuanzishwa kwa ukoloni wa Kijerumani (DOA) mji ulikuwa makao makuu ya mkoa wa Tanga.

Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 yanaonesha kuwa idadi ya watu katika Mkoa wa Tanga ni 2,615,597; wanaume 1,275,665 na wanawake 1,339,932.

SOMA PIA

MUHTASARI WA MAENEO YA UTAWALA, MKOA WA TANGA
Mkoa wa Tanga ni moja ya mikoa ya kaskazini mwa Tanzania, ukiwa na mfumo wa utawala unaojumuisha mamlaka za miji na wilaya. Mkoa huu umejigawa katika maeneo tofauti ya kiutawala kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi na kusimamia maendeleo.

View attachment 3108423
Chanzo: TAMISEMI
Mamlaka za Miji
Kwenye upande wa mamlaka za miji;

1. Mji wa Handeni una kata 12 na mitaa 60.
2. Mji wa Korogwe una kata 11 na mitaa 29.
3. Jiji la Tanga lina kata 27 na mitaa 181.

Jumla kwa mamlaka hizi za miji ni kata 50 na mitaa 270.

Mamlaka za Wilaya
Kwa mamlaka za wilaya, kuna wilaya nane ambazo zinasimamia maeneo ya vijijini.

1. Wilaya ya Bumbuli ina kata 18, vijiji 83, na vitongoji 673.
2. Wilaya ya Handeni ina kata 21, vijiji 91, na vitongoji 770
3. Wilaya ya Kilindi ina kata 21, vijiji 102, na vitongoji 611.
4. Wilaya ya Korogwe ina kata 29, vijiji 118, na vitongoji 610.
5. Wilaya ya Lushoto ina kata 33, vijiji 125, na vitongoji 942.
6. Wilaya ya Mkinga ina kata 22, vijiji 85, na vitongoji 335.
7. Wilaya ya Muheza ina kata 37, vijiji 126, na vitongoji 494
8. Wilaya ya Pangani ina kata 14, vijiji 33, na vitongoji 96.

Kwa ujumla, wilaya za mkoa wa Tanga zina jumla ya kata 195, vijiji 763, na vitongoji 4,531, wakati mamlaka za miji zina kata 50 na mitaa 270.

Mkoa wa Tanga unafikia jumla kuu ya kata 245, mitaa 270, vijiji 763, na vitongoji 4,531, ukionyesha muundo wa utawala unaolenga kuleta uwiano mzuri kati ya maeneo ya mijini na vijijini katika utoaji wa huduma na maendeleo ya kijamii.

MAJIMBO YA KIUCHAGUZI
Mkoa wa Tanga una jumla ya majimbo 12 ya kiuchaguzi. Majimbo haya ni Tanga Mjini, Muheza, Pangani, Korogwe Mjini, na Korogwe Vijijini. Pia kuna majimbo ya Handeni Mjini, Handeni Vijijini, na Kilindi, ambayo yanapatikana katika maeneo ya katikati ya mkoa. Vilevile, majimbo ya Lushoto, Mkinga, Mlalo na Bumbuli yanakamilisha idadi ya majimbo ya kiuchaguzi katika mkoa huu.

HALI YA KISIASA
Mkoa wa Tanga ni miongoni mwa mikoa ambayo kwa kiwango kikubwa nafasi za uongozi katika ngazi za serikali za mitaa, udiwani na ubunge zinashikiliwa na Chama cha Mapinduzi CCM ambapo hali hiyo ilisababishwa na uchaguzi wa serikali za Mitaa mwaka 2019 na uchaguzi mkuu 2020.

uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 uliwapitisha bila kupingwa wagombea wa CCM huku mikoa mingine ambayo wagombea wake walipita bila kupingwa ni Katavi, Ruvuma na Njombe

Katika uchaguzi wa serikali za mitaa watia nia wa nafasi za uongozi katika nafasi hizo kutoka vyama vya upinzani walienguliwa kwa madai ya kukosa sifa za kugombea nafasi hizo na hivyo kupelekea kuondoa ushindani katika uchaguzi huo na kuacha wagombea wa Chama tawala CCM kupita bila kupingwa.

Kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024, inatarajiwa kuwepo kwa mabadiliko na uimarishwaji wa demokrasia ili kutoa nafasi kwa vyama vyote kushiriki kikamilifu kwa uhuru na haki katika uchaguzi huo ili kutoa fursa kwa wananchi wote wenye mitazamo na milengo tofauti kugombea nafasi hizo.

MATUKIO KUELEKEA NOVEMBA 27
Leo tutaona kama Ummy na Mwana FA walifanya kazi yao vizuri kwenye hamasa😃😃
 
Mmmh huku nahisi CCM atakimbiza, sijasikia wapinzani wakikomaa kabisa
 
Back
Top Bottom