Matukio yasiyosahaulika aliyoyafanya dikteta Idd Amin Dada

Matukio yasiyosahaulika aliyoyafanya dikteta Idd Amin Dada

Ben Zen Tarot

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2014
Posts
4,298
Reaction score
7,612
Moja kati ya Matukio ya kufedhehesha na ambayo hayatasahaulika aliyoyafanya Idd Amin kule Nchini Uganda ni lile tukio la kuwauwa Omba Omba vilema waliokuwa wakiishi mjini kampala baada ya kuwakusanya na kwenda kuwamwaga ndani ya mto Nile.

Sababu kubwa ya Idd Amin kuwamwaga ombaomba hao ndani ya mto Nile ni kutokana mmoja wa vilema hao Ombaomba kufikia hatua ya kumlaumu Idd Amin hadharani walipokutana uso kwa uso mjini Kampala, Idd Amin alilaumiwa juu ya hatua yake ya kuwafukuza wawekezaji nchini humo bila sababu za msingi.

Idd Amin aliulizwa nchi itaendeleaje bila wawekezaji ? Na sisi s itutakufa kwa njaa kwa sababu ajira hazitakuwepo? watu hawatakuwa na pesa hata zakutusaidia sisi ombaomba, alimalizia kwa kumuambia wewe Idd Amini ni zaidi ya kichaa. Baada ya kumwambia Amin maneno yale makali ndipo Maliyamungu aliyekuwa mtu wa karibu sana na Amin alichomoa silaha aina ya Pistol kwa lengo la kumuua lakini Amin alimtuliza asifanye hivyo kisha wakaondoka.

Siku iliyofuata wanajeshi wa Idd Amin walimtafuta na kumkamata yule ombaomba na kuondoka nae na hapo ukawa mwisho wakujua historia ya ombaomba yule, hata hivyo inasadikika aliuwawa. Wiki moja baadae ndipo taarifa zikatolewa kwamba vilema ombaomba waishio mjini Kampala waripoti kwenye vituo vya polisi ili wapatiwe misaada.

Mamia ya ombaomba walikwenda kuripoti vituo vya polisi ili kusubiri misaada ya Amin lakini walipofika huko mambo yalikuwa tofauti na vile walivyoambiwa, kwani walikusanywa kwa pamoja na kupandishwa kwenye magari Aina ya Tipper kisha kupelekwa hadi lilipokuwa Daraja la Karuma Falls ambapo ni umbali wa km 200 kutoka Kampala kwenda Gulu, Daraja hilo la Nkurumah Falls lipo umbali wa takriban mita 100 kutoka kwenye maporomoko hayo.

Hapo Askari waliamriwa kuwamwaga ombaomba hao wasiojiweza ambapo walisafirishwa na maporomoko hayo hadi Mto Nile na huo ukawa mwisho wa historia yao. Idd Amin alisema kwamba aliamua kufanya Vile ili kuondoa kero na usumbufu wa Ombaomba mjini kampala.

Nb: hizi ninazoandika siyo propaganda ni ukweli kabisa wa matukio aliyoyafanya Amin.
FB_IMG_1632590532214.jpg
 
Hilo tukio lilishakanushwa siku nyingi, ni uvumi uliovumishwa na wapinzani wa field marshal Idi Amin Dada, waliokuwa wanaishi nje ya Uganda, ni kama vile mlivyo sikia maadui wa Saddam Hussein, aliyekuwa raisi wa Iraq, walizusha kuwa amelimbikiza silaha za nyuklia, huo ulikuwa ni uongo mtupu, sababu baada ya Sadam kuondokewa madarakani, walishindwa kuzionyesha hizo nyuklia zilipofichwa.
 
Hilo tukio lilishakanushwa siku nyingi,ni uvumi uliovumishwa na wapinzani wa field marshal Idi Amin Dada,waliokuwa wanaishi nje ya Uganda, ni kama vile mlivyo sikia maadui wa Saddam Hussein,aliyekuwa raisi wa Iraq,walizusha kuwa amelimbikiza silaha za nyuklia,huo ulikuwa ni uongo mtupu,sababu baada ya Sadam kuondokewa madarakani,walishindwa kuzionyesha hizo nyuklia zilipofichwa.
Upo sawa kabisa, ila Idd Amin bwana,alikuwa anagonga machungwa 12 kila siku enzi za mwisho wa uhai wake wakati anaumwa figo
 
Wananchi wa Uganda hawakusikia habari hizo? Kama walisikia, je, walipaza sauti? Na vipi kuhusu jumuiya za kimataifa, hazikuingilia kati?
 
Watawala madikteta huwa hawana mshipa wa huruma, kuua ni kawaida yao, hata akiona sisimizi anausakama utawala wake anamsiginia mbali, hala wanasilizwa sana na vyombo vya umma hata kama mambo si mazuri yatafanywa tu kwa ajiili yake
 
Wananchi wa Uganda hawakusikia habari hizo? Kama walisikia, je, walipaza sauti? Na vipi kuhusu jumuiya za kimataifa, hazikuingilia kati?
Ndiyo maana ilikuwa rahisi sana kwa majeshi ya Tanzania kumfurumusha Idiamin dada kwani wananchi wake walimchukia. Na sababu ni ukatili wake. Wananchi wa uganda walikuwa wanatoa ushirikiano mwingi kwa majeshi ya Tanzania kuliko ya Uganda.
 
Back
Top Bottom