Matumizi mazuri ya dola, uadilifu na Uchapakazi umeijengea imani CCM kwa wananchi

Matumizi mazuri ya dola, uadilifu na Uchapakazi umeijengea imani CCM kwa wananchi

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Hili halina ubishi kabisa kwa sababu kila mtanzania anaona kwa macho yake namna serikali ya awamu ya tano ilivyoweza kufanya mambo makubwa kwa muda mfupi kabisa.

Mfano ni utekelezaji wa mradi mkubwa ambao utakuwa mfano mkubwa wa kuigwa mradi wa tril 6+ za kitanzania ambao umepewa jina la JNHPP.

Pia ujenzi wa reli ya Standard gauge ambao kama ukikamilika utakuwa ni mradi ambao utasaidia kusafirisha mizigo. Sio kwa watanzania tu bali hata kwa jirani zetu ukanda wa Africa mashariki. Na hivyo kuleta nafuu kwa wananchi wa nchi hizi.

Lakini kutekeleza miradi hii sio jambo rahisi kama chama dola hakiwezi kutumia dola vizuri ili kudhibiti wizi na ubadhirifu.

Mfano kwenye mradi wa Sgr polisi wamefanikiwa kiasi kikubwa kudhibiti wezi wa mafuta, vifaa na material ya kujengea na haya ndio matumizi sahihi ya dola.

Pia katika miradi mbali mbali ambayo imekuwa inatekelezwa PCCB wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa fedha zinazotolewa zinafanya kazi inayotakiwa. Hivyo ubadhirifu na ufisadi umedhibitiwa ndio maana tumeshuhudiab Zahanati,vituo vya afya hospital,madaraja n.k vikihengwa kwa kasi.

Kwa mantiki hii Chama tawala kikitumia dola vizuri kutekeleza ilani yake ya uchaguzi kinaweza kukaa madarakani kwa muda mrefu sababu wananchi wanataka matokeo chanya ili waweze kufurahia kodi zao.

Mimi Chagu wa Malunde nikiwa Igunga safarini kuja dar.
0787600790
 
Hili halina ubishi kabisa kwa sababu kila mtanzania anaona kwa macho yake namna serikali ya awamu ya tano ilivyoweza kufanya mambo makubwa kwa muda mfupi kabisa.

Mfano ni utekelezaji wa mradi mkubwa ambao utakuwa mfano mkubwa wa kuigwa mradi wa tril 6+ za kitanzania ambao umepewa jina la JNHPP.

Pia ujenzi wa reli ya Standard gauge ambao kama ukikamilika utakuwa ni mradi ambao utasaidia kusafirisha mizigo. Sio kwa watanzania tu bali hata kwa jirani zetu ukanda wa Africa mashariki. Na hivyo kuleta nafuu kwa wananchi wa nchi hizi.

Lakini kutekeleza miradi hii sio jambo rahisi kama chama dola hakiwezi kutumia dola vizuri ili kudhibiti wizi na ubadhirifu.

Mfano kwenye mradi wa Sgr polisi wamefanikiwa kiasi kikubwa kudhibiti wezi wa mafuta, vifaa na material ya kujengea na haya ndio matumizi sahihi ya dola.

Pia katika miradi mbali mbali ambayo imekuwa inatekelezwa PCCB wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa fedha zinazotolewa zinafanya kazi inayotakiwa. Hivyo ubadhirifu na ufisadi umedhibitiwa ndio maana tumeshuhudiab Zahanati,vituo vya afya hospital,madaraja n.k vikihengwa kwa kasi.

Kwa mantiki hii Chama tawala kikitumia dola vizuri kutekeleza ilani yake ya uchaguzi kinaweza kukaa madarakani kwa muda mrefu sababu wananchi wanataka matokeo chanya ili waweze kufurahia kodi zao.

Mimi Chagu wa Malunde nikiwa Igunga safarini kuja dar.
0787600790

Akili ndogo ikiwa kazini, Bila shaka akili za mwisi au ibologero
 
Imani itajengwa kwa uaminifu, uadilifu na matokeo chanya, siyo kutumia maguvu. hapo umejenga UOGA siyo imani.
 
Wapi imetumika nguvu? Kukamata wahalifu na kudhibiti rushwa na ufisadi?

Usidanganyike kitoto hivyo, rushwa imethibitiwa kwa kiwango gani? wabunge na madiwani wa upinzani wamenunuliwa na ushahidi wa video umetolewa ni hatua gani ilichukuliwa? Wake up dude.

Askari aliyefyatua risasi ikamuuwa akwilina alitakiwa kuwa mhalifu lakini amechukuliwa hatua gani hadi sasa? bashite kuvamia clouds kwa silaha na tena usiku wa maanani, ule ni uhalifu lakini alichukuliwa hatua gani, unazungumzia wahalifu gani sasa? acha ujinga.

Aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani alifukuzwa kazi kwa ufisadi bila hatua nyingine kuchukuliwa dhidi yake, leo hii amepewa wizara nyingine, amekuja waziri wa mambo ya ndani mwingine kafukuzwa kazi kwa ufisadi tena, then baada ya hapo what next? unaongelea ufisadi wa aina gani? acha upuuzi.
 
Hakuna La Maana uliloliandika Hapo Isipokuwa Kujionyesha Kuwa Haujitambui...Mambo Mazuri Yanajieleza yenyewe na kama unaamini kila mtu anajua yua nini Kutumia nguvu nyingu kuyaelezea Hapa. Kama CCM inakubalika, Uchaguzi ufanyike Octoba, Polisi/tume ya uchanguzi itende haki. Mbona Utajidharau na Kujiona hakuna lolote wala chochote watu wanakikubali...
 
Usidanganyike kitoto hivyo, rushwa imethibitiwa kwa kiwango gani? wabunge na madiwani wa upinzani wamenunuliwa na ushahidi wa video umetolewa ni hatua gani ilichukuliwa? Wake up dude.

Askari aliyefyatua risasi ikamuuwa akwilina alitakiwa kuwa mhalifu lakini amechukuliwa hatua gani hadi sasa? bashite kuvamia clouds kwa silaha na tena usiku wa maanani, ule ni uhalifu lakini alichukuliwa hatua gani, unazungumzia wahalifu gani sasa? acha ujinga.

Aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani alifukuzwa kazi kwa ufisadi bila hatua nyingine kuchukuliwa dhidi yake, leo hii amepewa wizara nyingine, amekuja waziri wa mambo ya ndani mwingine kafukuzwa kazi kwa ufisadi tena, then baada ya hapo what next? unaongelea ufisadi wa aina gani? acha upuuzi.
Hizo zote ni tuhuma tu. Mahakama ndio chombo pekee cha kumtia mtu hatiani. Na hicho kikisema huyu mharifu kwa kutoa rushwa au kutumia madaraka vibaya ndio linakuwa jibu.
 
Back
Top Bottom