Mbute na chai
JF-Expert Member
- Jul 21, 2012
- 564
- 593
Nimeshawishika kushiriki maarifa haya baada ya kuwepo kwa taarifa za matumizi na uhifadhi mbaya wa silaha hasa kwa raia.
Kila mtu Tanzania anayo haki ya kumiliki silaha kwa matumizi binafsi kama vile ulinzi binafsi, kuwinda n.k. Leo sitaongelea namna ya upatikanaji wa haki hii bali vitu vya kuzingatia ili waliyopata haki hii wasije wakajikuta wanaijutia.
1. KANUNI ZA USALAMA WA SILAHA YA MOTO (FIREARM SAFETY RULES).
A. Kila silaha huwa ipo tayari kupiga hadi utakapojiridhisha vinginevyo. Dhana hii ikikukaa akilini kamwe hautaweka mzaa kwenye silaha. Hivyo, unaposhika silaha, ikague na jiridhishe kuwa iko salama.
B. Kila unaposhika silaha elekeza mtutu mahali salama ambapo hata risasi ikitoka kwa bahati mbaya haitaleta madhara kwa binadamu, wanyama na mali. Fanya hivi hata kama silaha haina risasi. Ukiwa na mazoea haya kamwe hautadhuru mtu au kitu kwa bahati mbaya.
C. Unaposhika silaha usiguse, kwa namna yoyote, kitufe cha kufyatulia (finger off the trigger) hadi pale utakapokuwa tayari kupiga. Fanya hivi hata kama silaha haina risasi. Madhara ya bahati mbaya mara nyingi huusishwa na ubonyezaji wa kitufe cha kufyatulia kwa bahati mbaya.
D. Unapokuwa tayari kupiga hakikisha nini kipo nyuma ya mtu au kitu unachotaka kukipiga. Baadhi ya risasi kama vile full metal jacket (FMJ) huweza kupenya na kutokea upande wa pili hivyo kudhuru kilichopo nyuma ya kilengwa.
E. Unapohifadhi risasi zako hakikisha kileta madhara (bullet) kinaangalia chini. Risasi (cartridge/round) ni mjumuiko wa vitu vitatu; kilipuzi (primer), kilipuka kilicho ndani ya ganda ( casing) (explosive powder) na kileta madhara (bullet). kilipuzi hugongwa na pini ya kufyatulia na huwasha moto unaopelekea kilipuka kulipuka na kuondosha kileta madhara kwa kasi isiyoonekana kwa macho. Hivyo, unapohifadhi risasi huku kileta madhara kikielekea chini utaepuka mdhara ya tokanayo na risasi kulipuka kwa namna yoyote ile.
F. Unapohifadhi silaha yako, hakikisha unaiacha kwenye hali ambayo haiwezi kutumika kwa haraka (incapable of immediate use). Hivyo, hakikisha unatenganisha risasi na silaha. Mfano; kijana aliyechukua silaha ya baba yake kilimanjaro (taarifa ya zamani kidogo) na kujiua asingeweza kufanya hivyo kama mmiliki wa sila hiyo angezingatia kanuni hii.
LEO TUKOMEE HAPA. ANDIKO JINGINE LITAHUSU UHIFADHI NA MATUMIZI SAHII.
Kila mtu Tanzania anayo haki ya kumiliki silaha kwa matumizi binafsi kama vile ulinzi binafsi, kuwinda n.k. Leo sitaongelea namna ya upatikanaji wa haki hii bali vitu vya kuzingatia ili waliyopata haki hii wasije wakajikuta wanaijutia.
1. KANUNI ZA USALAMA WA SILAHA YA MOTO (FIREARM SAFETY RULES).
A. Kila silaha huwa ipo tayari kupiga hadi utakapojiridhisha vinginevyo. Dhana hii ikikukaa akilini kamwe hautaweka mzaa kwenye silaha. Hivyo, unaposhika silaha, ikague na jiridhishe kuwa iko salama.
B. Kila unaposhika silaha elekeza mtutu mahali salama ambapo hata risasi ikitoka kwa bahati mbaya haitaleta madhara kwa binadamu, wanyama na mali. Fanya hivi hata kama silaha haina risasi. Ukiwa na mazoea haya kamwe hautadhuru mtu au kitu kwa bahati mbaya.
C. Unaposhika silaha usiguse, kwa namna yoyote, kitufe cha kufyatulia (finger off the trigger) hadi pale utakapokuwa tayari kupiga. Fanya hivi hata kama silaha haina risasi. Madhara ya bahati mbaya mara nyingi huusishwa na ubonyezaji wa kitufe cha kufyatulia kwa bahati mbaya.
D. Unapokuwa tayari kupiga hakikisha nini kipo nyuma ya mtu au kitu unachotaka kukipiga. Baadhi ya risasi kama vile full metal jacket (FMJ) huweza kupenya na kutokea upande wa pili hivyo kudhuru kilichopo nyuma ya kilengwa.
E. Unapohifadhi risasi zako hakikisha kileta madhara (bullet) kinaangalia chini. Risasi (cartridge/round) ni mjumuiko wa vitu vitatu; kilipuzi (primer), kilipuka kilicho ndani ya ganda ( casing) (explosive powder) na kileta madhara (bullet). kilipuzi hugongwa na pini ya kufyatulia na huwasha moto unaopelekea kilipuka kulipuka na kuondosha kileta madhara kwa kasi isiyoonekana kwa macho. Hivyo, unapohifadhi risasi huku kileta madhara kikielekea chini utaepuka mdhara ya tokanayo na risasi kulipuka kwa namna yoyote ile.
F. Unapohifadhi silaha yako, hakikisha unaiacha kwenye hali ambayo haiwezi kutumika kwa haraka (incapable of immediate use). Hivyo, hakikisha unatenganisha risasi na silaha. Mfano; kijana aliyechukua silaha ya baba yake kilimanjaro (taarifa ya zamani kidogo) na kujiua asingeweza kufanya hivyo kama mmiliki wa sila hiyo angezingatia kanuni hii.
LEO TUKOMEE HAPA. ANDIKO JINGINE LITAHUSU UHIFADHI NA MATUMIZI SAHII.