Matumizi ya dola ya kimarekani kama sarafu ya Tanzania

Matumizi ya dola ya kimarekani kama sarafu ya Tanzania

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Nimeshindwa kuelewa niiweke wapi thread hii baada ya kusoma makala moja pale Mwanachi kuhusu mada ambayo imekuwa inakera akili yangu muda mrefu sana. Thread ingeweza kuwa siasa, uchumi au kwenye falsafa; nikaamua kuiweka hapa kwenye falsafa.

Nimekuwa na bahati sana ya kutembea na kuishi katika nchi nyingi sana duniani, ila sijawahi kufika nchi ambako biashara zote zinafanyika katika dola za kimerakni zaidi ya marekani kwenyewe. Hata Kanada ambayo ni jirani kabisa na marekani na raia wake wanafanya manunuzi yao sehemu yoyote ya mpaka, ukishavuka kuingia Canada unatumia Canadian Dollar, na ukirudi Marekani unatumia American Dollar.

Je kinachotusumbua watanzania ni ulimbukeni au kweli ni udhaifu wa sarafu yetu? Nimeangalia trends kwa muda wa miaka kumi kuhusu mabadiliko ya thamani ya sarafu mbalimbali dhidi sarafu ya kimarekani na kugundua kuwa sarafu yetu ni stable kiasi cha kutosha, kwani haijawahi kubadilika ghafla ghafla. Ingawa kuna nchi nyingine kama Kenya na South Afrika zilikuwa stable zaidi yetu lakini mabadiliko ya sarafu ya Tanzania hayajawa so alarming kiasi kuwa biashara zetu tuziendeshe kwa hela ya kigeni; nikitoka Tabora na hela yangu ya madafu siwezi kulala hoteli za maana Tanzania mpaka ninunue dola za kimarekani na kumpa faida muuzaji wa dola hizo kabla sijampa faida mtu wa hoteli, je hiyo kweli halali kwa nchi?

Chini hapo nimeweka trends zinazoonyesha jinsi sarafu mbalimbali zilivyobadilika katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Ingawa sarafu ya Tanzania imekuwa inapoteza thamani, upotezu huo ni kwa currency investors tu wanaoinvest kwa muda mrefu kwani hauathiri kabisa katika biashara za kila siku kwa vile thamani hiyo ilikuwa inapotea kidogo kidogo. Mabadiliko ya thamani ya sarafu ya kitanzania hayatofautiani kabisa na yale ya sarafu ya Botswana lakini mpaka kesho hutakuta Botswana wanaendesha biashara ya ndani kwa kutumia dola ya kimarekani. India vile vile mambo ni hayo hayo.

Wataalamu wa mambo ya pesa mtusaidie kwenye tatizo hio.

Wabunge wakerwa matumizi ya dola

dola+px.jpg


Dola ya Marekani.PICHA|MAKTABA
Kwa ufupi
Matumizi ya sarafu ya Marekani yanadaiwa kuchangia kushuka kwa thamani ya sarafu ya Tanzania



Dodoma.Wabunge wameonyesha kukerwa na mtindo unaoshamiri wa matumizi ya Dola ya Marekani nchini, jambo ambalo linasababisha kuporomoka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania.

Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya (BoT) ya mwaka 2006, imebainisha wazi kuwa shilingi ya Tanzania ndiyo fedha halali kwa malipo ya bidhaa na huduma ikiwamo hotelini, maduka makubwa na taasisi nyingine.

Mjadala huo ulichochewa na taarifa ya Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara kwa kipindi cha Machi hadi Desemba 15 iliyowasilishwa na Mwenyekiti wake, Mahmoud Mgimwa.

"Matangazo mengi na ulipaji huduma na bidhaa nchini yamewekwa kwa fedha za kigeni, kitendo ambacho ni kinyume cha sheria," alisema Mgimwa.
Pia, Mgimwa alisema uchunguzi wao umebaini baadhi ya maduka ya kubadilisha fedha (Bureau de Change) yamekuwa yakijihusisha na uhamishaji fedha kwenda nchi za nje.

"Maduka hayo yanatumika kama uchochoro wa kutorosha fedha nje ya nchi na kusababisha kupotea kwa mapato ya Serikali, huku thamani ya shilingi ya Tanzania ikishuka thamani," alisema.

Kamati hiyo inaitaka Serikali kuwachukulia hatua wafanyabiashara wanaomiliki maduka hayo na kwamba, iongeze usimamizi ili kukomesha tatizo hilo lenye athari kwa uchumi wa nchi.

"Uzoefu wa nchi nyingi kama Afrika ya Kusini, Kenya na Ethiopia unaonyesha huwezi kupata fedha za kigeni kama hujaonyesha sababu, kitambulisho na hati ya kusafiria," alisema.

Akichangia taarifa hiyo, Mbunge wa Kisesa, Lwaga Mpina alisema hakuna nchi duniani inayoweza kufanya mambo ya kitoto kama Tanzania kudhibiti matumizi holela ya fedha za kigeni.


Sarafu ya Tanzania
tanzania-currency.png


Sarafu ya Kenya

kenya-currency.png


Sarafu ya Afrika ya kusini

south-africa-currency.png

Sarafu ya India
india-currency.png


Sarafu ya Botswana
botswana-currency.png

Sarafu ya Canada
canada-currency.png
 
Kichuguu;

Mwenyewe una makosa. Kwanini unaita sarafu ya Tanzania ni ya madafu wakati hiyo ndio pesa halali ya malipo nchini? Bila kuwepo na hiyo sarafu, mwenye akiba za dola za kimarekani nchini Tanzania hawezi kufaidi akiba yake. Hivyo ni lazima tuipe heshima hiyo sarafu.
 
Kichuguu;

Mwenyewe una makosa. Kwanini unaita sarafu ya Tanzania ni ya madafu wakati hiyo ndio pesa halali ya malipo nchini? Bila kuwepo na hiyo sarafu, mwenye akiba za dola za kimarekani nchini Tanzania hawezi kufaidi akiba yake. Hivyo ni lazima tuipe heshima hiyo sarafu.

Hapana mimi siiiti kuwa ni ya madafu. Ninaiheshimu!
 
Hapana mimi siiiti kuwa ni ya madafu. Ninaiheshimu!

Sarafu ya nchi ni commodity na kuna watu wanaoishi kwa kufanya biashara ya sarafu. Vilevile sarafu ya nchi inatumika katika kuweka akiba za watu. Hivyo kuna logic explanations zinazowafanya watanzania kutumia dola.

Moja ya explanation hizo ni uncertainity. Japokuwa shilingi ya Tanzania imekuwa katika kiwango kinachoeleweka kwa muda mrefu, hiyo haitokani kwa sehemu kubwa na sera za pesa za Tanzania. Inatokana na ukweli kuwa sera za pesa za Marekani katika miaka ya karibuni ni kushusha thamani ya dola.
 
Tunazihitaji sana dola za kimarekani kwa sababu tuna-import zaidi kuliko tuwezavyo ku-export, katika hali kama hii hauna option zaidi ya kuitafuta dola kwa namna yeyote ile.
 
Tunazihitaji sana dola za kimarekani kwa sababu tuna-import zaidi kuliko tuwezavyo ku-export, katika hali kama hii hauna option zaidi ya kuitafuta dola kwa namna yeyote ile.

Kwani unapo-import huwa unalipa hela taslimu, yaani unatuma boksi la manoti au unatuma karatasi tu inayoonyesha kuwa pesa zinatoka katika benki yako hapa Tanzania na kwenda kwenye benki ya anayekuuzia bidhaa huko aliko ?
 
Sarafu ya nchi ni commodity na kuna watu wanaoishi kwa kufanya biashara ya sarafu. Vilevile sarafu ya nchi inatumika katika kuweka akiba za watu. Hivyo kuna logic explanations zinazowafanya watanzania kutumia dola.

Moja ya explanation hizo ni uncertainity. Japokuwa shilingi ya Tanzania imekuwa katika kiwango kinachoeleweka kwa muda mrefu, hiyo haitokani kwa sehemu kubwa na sera za pesa za Tanzania. Inatokana na ukweli kuwa sera za pesa za Marekani katika miaka ya karibuni ni kushusha thamani ya dola.

Maisha ya sarafu duniani kote ni uncertain, hakuna sarafu duniani ambayo haibadiliki thamani, kila sarafu including dolar ya kimarekani, hubadilika thamani yake karibu kila siku. Kinachokosekana ni watanzania kutokuwa na imani na sarafu yao tu. Inflation ndiyo jambo ambalo linalosababisha watu wasiwe na imani na sarafu yoyote ile, kwa Tanzania inflation rate ni ya chini sana ukilinganisha na nchi nyingi duniani ambazo hazitumii dola ya kimarekani. Hebu angalia hiyo post ya Nyani Ngabu hapo chini.

Miaka kama kumi na mbili iliyopita nilikuwa natafuta viza (H1B) kwenye ubalozi wa marekani nikaambiwa nilipe ada ya dola 400, nikatoa dola hizo lakini wakanikatalia kwa kunitaka nilipe katika shilingi za kitanzania ambazo exchange rate waliyonipa ilikuwa ni nzuri hata kuliko hata ile ya kwenye Bureau de Change. Iwapo wamarekani wenyewe waliona hawana haja ya kutumia dola katika nchi nyingine inakuwaje sisi tunaishobokea namna hiyo?
 
Last edited by a moderator:
Bitcoin drove the point home. The point being all monetary systems - from the most primitive shell systems to the microsecond crunching trades on NYSE- and conventions are arbitrary, backed by intransigent high priests prone to the temptation to rig the LIBOR.

But that's just paraphrasing J. M Keynes.

Where is John Mashaka when you need him?
 
Last edited by a moderator:
Maisha ya sarafu duniani kote ni uncertain, hakuna sarafu duniani ambayo haibadiliki thamani, kila sarafu including dolar ya kimarekani, hubadilika thamani yake karibu kila siku. Kinachokosekana ni watanzania kutokuwa na imani na sarafu yao tu. Inflation ndiyo jambo ambalo linalosababisha watu wasiwe na imani na sarafu yoyote ile, kwa Tanzania inflation rate ni ya chini sana ukilinganisha na nchi nyingi duniani ambazo hazitumii dola ya kimarekani. Hebu angalia hiyo post ya Nyani Ngabu hapo chini.


Kichuguu;

Sababu ya kuwepo kwa Central Banks and monetary policies ni kupunguza au kuondoa hizo uncertainties. Ukisema kuwa inflation ni sababu ya watu kutumia dola, sioni kuwa hiyo ni hoja ya msingi.

Hii ni kwa sababu inflation ya Tanzania inakokotolewa kwa bidhaa kama unga, maharage, chumvi, sukari, viazi n.k. Hivi ni vitu ambavyo watanzania wengi wenye kutumia dola havina matatizo nayo.

Kwa maoni yangu binafsi, inawezekana wenye uwezo wanalinda assets na wealth kwa kutumia accounts za kigeni. Vilevile watanzania wanatumia sana imported goods ambao uagizaji wake unategemea dollar ya kimarekani.
 
Mkuu mijadala ya hapa ni muhimu sana kwa mambo mbali mbali kuhusu nchi yetu. Hawa Watawala wangekuwa wanakuja hapa kuiba mawazo ya GTs mbali mbali hapa jamvini na kuyaingiza katika sera zao na kuhakikisha yanafanyiwa kazi basi madudu katika utendaji yangepunguzwa sana kama siyo kutokomezwa kabisa, lakini wako busy kujikusanyia mabilioni na kupanga mikakati ya kuisambaratisha CHADEMA!!!!

BUBU BAK Umenikumbusha kuwa tuliwahi kuliongelea jambo hili miaka sita iliyopita, lakini serikali yetu haijawahi kulifanyia kazi muda wote huo.
 
Ni ombwe kubwa la uongozi lililopo nchini ndio linasababisha matatizo yote likiwemo hili. Lilizungumziwa sana miaka michache baada ya Kikwete kuingia madarakani lakini hadi hii leo hakuna dalili zozote zilizohukuliwa.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...x-transactions-in-tanzania-govt-to-act-2.html


Son;

Wakati mwingine kuna tatizo la capability. Tanzania ilitumia miaka ya mwanzo ya uhuru wake kujenga uchumi wa kijamaa ambao ulisema pesa si msingi wa maendeleo. Nchi haikusomesha financiers kwa sababu ilikuwa ni kujifunza ubepari. Sasa mnataka nchi ifanye miujiza kwa kitu ambacho haikujiandaa? Endelea kula matunda ya Chuo Kikuu Cha Chama Kigamboni.
 
Son hili la kuzuia dollarization nchini halihitaji kuwa na financiers. Kama ingekuwa ni Serikali makini basi ingesimamia kauli zake chungu nzima ilizozitoa tangu mwaka 2007 wakati wa Meghji kama Waziri wa Fedha hili tatizo lingeshakuwa ni history miaka 6 iliyopita, lakini kwa kuwa utendaji ni SIFURI limeendelea kuwepo hadi hii leo. Hao financiers unaowazungumzia hawahusiani kwa namna yoyote na tatizo hili.

Son;

Wakati mwingine kuna tatizo la capability. Tanzania ilitumia miaka ya mwanzo ya uhuru wake kujenga uchumi wa kijamaa ambao ulisema pesa si msingi wa maendeleo. Nchi haikusomesha financiers kwa sababu ilikuwa ni kujifunza ubepari. Sasa mnataka nchi ifanye miujiza kwa kitu ambacho haikujiandaa? Endelea kula matunda ya Chuo Kikuu Cha Chama Kigamboni.
 
Maisha ya sarafu duniani kote ni uncertain, hakuna sarafu duniani ambayo haibadiliki thamani, kila sarafu including dolar ya kimarekani, hubadilika thamani yake karibu kila siku. Kinachokosekana ni watanzania kutokuwa na imani na sarafu yao tu. Inflation ndiyo jambo ambalo linalosababisha watu wasiwe na imani na sarafu yoyote ile, kwa Tanzania inflation rate ni ya chini sana ukilinganisha na nchi nyingi duniani ambazo hazitumii dola ya kimarekani. Hebu angalia hiyo post ya Nyani Ngabu hapo chini.


Kichuguu;

Sababu ya kuwepo kwa Central Banks and monetary policies ni kupunguza au kuondoa hizo uncertainties. Ukisema kuwa inflation ni sababu ya watu kutumia dola, sioni kuwa hiyo ni hoja ya msingi.

Hii ni kwa sababu inflation ya Tanzania inakokotolewa kwa bidhaa kama unga, maharage, chumvi, sukari, viazi n.k. Hivi ni vitu ambavyo watanzania wengi wenye kutumia dola havina matatizo nayo.

Kwa maoni yangu binafsi, inawezekana wenye uwezo wanalinda assets na wealth kwa kutumia accounts za kigeni. Vilevile watanzania wanatumia sana imported goods ambao uagizaji wake unategemea dollar ya kimarekani.

Kwenye niliyowekea rangi, sijui kama umenielewa au kama sikujieleza vizuri.

Mambo mengine ya kiuchumi unayoongelea yako pia katika nchi nyingine, lakini hawafanyi biahsra zao za ndani kwa kutumia sarafu ya nje. Ni nchi moja tu duniani hapa ambayo ilijitangazia rasmi kuendesha biashara zao za ndani kwa kutumia sarafu ya kiamrekani, nchi hiyo ni Zimbabwe ambayo ilikuwa na inflation ya zaidi ya 1000%. Matatizo ya Tanzania ni ulimbukeni na Money Laundering! Yaani kuna Money Launders wanaotaka mambo yawe vile halafu kuna malimbukeni wanaodhani kuwa kuuza kwa dola ndiyo biashara yenyewe. Unaweza kukutana na mfanya biashara anaweka pesa zake benki zikiwa ni mchanganyiko wa sarafu za kitanzania na za kiamrekani, ambazo zikiingia benki zinapewa uzito sawa, lakini bado hataki kutambua hivyo, bado anadai mteja amlipe kwa dola.
 
Kwenye niliyowekea rangi, sijui kama umenielewa au kama sikujieleza vizuri.

Mambo mengine ya kiuchumi unayoongelea yako pia katika nchi nyingine, lakini hawafanyi biahsra zao za ndani kwa kutumia sarafu ya nje. Ni nchi moja tu duniani hapa ambayo ilijitangazia rasmi kuendesha biashara zao za ndani kwa kutumia sarafu ya kiamrekani, nchi hiyo ni Zimbabwe ambayo ilikuwa na inflation ya zaidi ya 1000%. Matatizo ya Tanzania ni ulimbukeni na Money Laundering! Yaani kuna Money Launders wanaotaka mambo yawe vile halafu kuna malimbukeni wanaodhani kuwa kuuza kwa dola ndiyo biashara yenyewe. Unaweza kukutana na mfanya biashara anaweka pesa zake benki zikiwa ni mchanganyiko wa sarafu za kitanzania na za kiamrekani, ambazo zikiingia benki zinapewa uzito sawa, lakini bado hataki kutambua hivyo, bado anadai mteja amlipe kwa dola.


Mkuu Kichuguu;

Nakubaliana na wewe kuhusiana na ulimbukeni. Na ulimbukeni mkubwa unatokana na viongozi na wasomi wenye nafasi. Kwa mfano kuna viongozi wengi wamejenga nyumba za kupangisha ambazo malipo yapo kwenye dollar. Niliona kipande cha habari kuwa Mkapa alipostaafu alitaka alipwe mafao yake kwa mkupuo na kwa dola. Vilevile nilisikia gavana wa benki aliyepita alikuwa analipwa kwa dola.

Kama watu wanaohusika na monetary policies wanafanya hivyo, kwanini mfanya biashara asilinde assets zake kwenye dola?
 
Son hili la kuzuia dollarization nchini halihitaji kuwa na financiers. Kama ingekuwa ni Serikali makini basi ingesimamia kauli zake chungu nzima ilizozitoa tangu mwaka 2007 wakati wa Meghji kama Waziri wa Fedha hili tatizo lingeshakuwa ni history miaka 6 iliyopita, lakini kwa kuwa utendaji ni SIFURI limeendelea kuwepo hadi hii leo. Hao financiers unaowazungumzia hawahusiani kwa namna yoyote na tatizo hili.

Leaders aren't born. They are made. Kikwete alitumia muda mwingi kukimbiza mwenge. Je unategemea nini?
 
Back
Top Bottom