Matumizi ya maneno "hayati" na "marehemu"

Matumizi ya maneno "hayati" na "marehemu"

mhondo

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2011
Posts
968
Reaction score
354
Nini tofauti ya matumizi ya maneno hayati na marehemu na yanatakiwa kutumika wakati gani?
 
Hayati inatumika kwa mtu maarufu ambaye amekufa lkn marehemu ni kwa watu wa kawaida na watoto wa mbwa kama sisi
 
Kumbuka kuwa hayo maneno yote mawili yametokana na lugha tamu ya Kiarabu,

Kwa maana halisi, Hayati ni "maisha yangu". Kiarabu ukisema Hayati "maisha yangu" kum address mtu akiwepo au asiwepo unamaanisha upendo wa hali ya juu na huyo ni mshirika wa maisha (shirka til hayaa) yako awepo au asiwepo.

Marehemu = Aliyesamehewa au ni kifupisho cha kusema "tunamuombea awe katika walio samehewa (Mercy) na Mwenyeezi Mungu".
 
Kama tutakwenda kwenye chimbuko la maneno Marhum na al hayat, Marehemu ni mtu aliyekufa au mwendazake wakati hayati ni maisha kwa ujumla mfano, Al-Hayat Al-Dunya (The Life of This World]. Ni bahati mbaya kuwa neno hayati hutumika vibaya na kinyume cha maana yake halisi. Si neno hilo tu. Hata neno kusudi. Wengi husema makusudi jambo ambalo ni kinyume cha dhana nzima ya neno husika. Siku hizi hata baada na badala zachanganywa na kukosewa mara nyingi ukiachia maneno mengine kama vile kumwita mwanamke binadamu wakati ni bintadamu. Anyways, leo sitongoi sana ingawa nimeishafunga nyama na nyasi zimeishatandikwa ugani tayari farasi kufungiana nyama na nyangwa.
 
Hayati inatumika kwa mtu maarufu ambaye amekufa lkn marehemu ni kwa watu wa kawaida na watoto wa mbwa kama sisi

Kwahiyo kwa Nyerere (Rais wa kwanza) hastahili kuitwa marehemu bali hayati? Basi kazi ipo.
 
Kama tutakwenda kwenye chimbuko la maneno Marhum na al hayat, Marehemu ni mtu aliyekufa au mwendazake wakati hayati ni maisha kwa ujumla mfano, Al-Hayat Al-Dunya (The Life of This World]. Ni bahati mbaya kuwa neno hayati hutumika vibaya na kinyume cha maana yake halisi. Si neno hilo tu. Hata neno kusudi. Wengi husema makusudi jambo ambalo ni kinyume cha dhana nzima ya neno husika. Siku hizi hata baada na badala zachanganywa na kukosewa mara nyingi ukiachia maneno mengine kama vile kumwita mwanamke binadamu wakati ni bintadamu. Anyways, leo sitongoi sana ingawa nimeishafunga nyama na nyasi zimeishatandikwa ugani tayari farasi kufungiana nyama na nyangwa.

Inabidi zifanyike jitihada za kutosha ili lugha isipotoshwe.
 
Kumbuka kuwa hayo maneno yote mawili yametokana na lugha tamu ya Kiarabu,

Kwa maana halisi, Hayati ni "maisha yangu". Kiarabu ukisema Hayati "maisha yangu" kum address mtu akiwepo au asiwepo unamaanisha upendo wa hali ya juu na huyo ni mshirika wa maisha (shirka til hayaa) yako awepo au asiwepo.

Marehemu = Aliyesamehewa au ni kifupisho cha kusema "tunamuombea awe katika walio samehewa (Mercy) na Mwenyeezi Mungu".

Ukimwita mtu ambaye bado hajafa hayati si unaweza kuibua ugomvi mkubwa?. Sijawahi kusikia neno hayati likitumiwa kwa mtu ambaye hajafa.
 
Ukimwita mtu ambaye bado hajafa hayati si unaweza kuibua ugomvi mkubwa?. Sijawahi kusikia neno hayati likitumiwa kwa mtu ambaye hajafa.

Kiswahili limezoweleka kutumika kwa waliofariki. Mimi nimetoa asili na maana ya hilo neno kutokana na lugha ya lilipotoka. Na hata kwa hicho Kiswahili linapotumika kwa aliyekufa linamaanisha mapenzi ya hali ya juu kwa aliyeondoka, kumaanisha kuwa huyo alikuwa ni part ya maisha yako, "hayati" lina maanisha "maisha yangu".

Msikilize huyu mama Oum Kulthum legend wa fani ya muziki wa kiarabu na analitumia neno "hayati" katika nyimbo yenye mashairi ya mahaba yaliotukuka katika nyimbo yake inayoitwa "Alf Lela u Lela", sikiliza kuanzia dakika ya 8 na sekunde 40. : http://www.youtube.com/watch?v=Y1Pr0KPeQio&feature=fvwrel

Kula raha kidogo kwa nyimbo nzuri sana.
 
Hili neno Hayat/ Hayati ni moja kati ya maneno yaliyokuwa yananisumbua maana yake .
Ninaona katika Kiswahili linatumika kwa mtu aliyekufa, lakini huku nilipo naona kuna magazeti yanaitwa al hayat
hapo ndipo nilipochanganyikiwa. Lakini kwa maelezo Mkuu Zomba sasa nimeelewa .Nashukura kwa aliyeuliza
 
Kwahiyo kwa Nyerere (Rais wa kwanza) hastahili kuitwa marehemu bali hayati? Basi kazi ipo.

Enzi za hayati Mwl Nyerere. Maana yake enzi za uhai wake , maisha yake nk. Huwezi kusema hayati Nyerere but Marehemu Nyerere.
 
Neno hayati linatokana na neno la kiarabu Hayatollah na maana yake ni mheshimiwa,wabongo wanalitumia vibaya kwa mtu alifariki.
 
neno hayati Linatokana na neno la kiarabu la Hayatollah maana yake ni mheshimiwa,wabongo wanali2mia kinyume kwa mtu alikufa.
 
Hili neno Hayat/ Hayati ni moja kati ya maneno yaliyokuwa yananisumbua maana yake .
Ninaona katika Kiswahili linatumika kwa mtu aliyekufa, lakini huku nilipo naona kuna magazeti yanaitwa al hayat
hapo ndipo nilipochanganyikiwa. Lakini kwa maelezo Mkuu Zomba sasa nimeelewa .Nashukura kwa aliyeuliza

Sisi tunaoishi nchi za kiarab hilo neno tunatumia sana kwa my dia, au kwa wapenzi wetu ndio tunawaita hayaty, au kwa kichombeza unamuita yaa hayaty, hata wanaume tunaitana habiby ni kawaida kabisa huku
 
Ninashukuru kwa ufafanuzi uliotolewa na wachangiaji karibu wote. Ufahamu wangu umefunguka zaidi.
 
hayati inatumika kwa mtu maarufu ambaye amekufa lkn marehemu ni kwa watu wa kawaida na watoto wa mbwa kama sisi
maelezo ya juu ni sahihi ila ya mwisho si sahihi, kwani umejidunisha mtoto wa mbwa hawezi kuandika wala kutoa hoja!!! Wewe si mtoto wa mbwa!!!! Je ni sahihi?
 
Sisi tunaoishi nchi za kiarab hilo neno tunatumia sana kwa my dia, au kwa wapenzi wetu ndio tunawaita hayaty, au kwa kichombeza unamuita yaa hayaty, hata wanaume tunaitana habiby ni kawaida kabisa huku

Weeeh! Mi ukiniita Habiby lazima nikutolee uvivu! Hahaaa
 
Kumbuka kuwa hayo maneno yote mawili yametokana na lugha tamu ya Kiarabu,

Kwa maana halisi, Hayati ni "maisha yangu". Kiarabu ukisema Hayati "maisha yangu" kum address mtu akiwepo au asiwepo unamaanisha upendo wa hali ya juu na huyo ni mshirika wa maisha (shirka til hayaa) yako awepo au asiwepo.

Marehemu = Aliyesamehewa au ni kifupisho cha kusema "tunamuombea awe katika walio samehewa (Mercy) na Mwenyeezi Mungu".

Liongo, kwenda huko!
 
Back
Top Bottom