Matumizi ya Mbolea katika kilimo cha karanga

Vp mwanzo ulivuna kiasi gani , kwa nusu heka ?
 
Inategemea na aina ya udongo kwanza katika kichanga weka mbolea na miziz inapata urahisi wa kupenya
 
Tuna shida kubwa sana ya wataalamu wa KILIMO ili kupata utaalamu wao kuhusu aina ya udongo na matumizi yake

Mara nyingi sana mazao yanakua treated tofauti kulingana na aina ya udongo

Kuna aina ya udongo ukiweka mbolea ya aina fulani shina la karanga linakua kubwa sana limemea vizuri na linaweka karanga nyingi chini tena kubwa kweli LAKINI ukiimenya karanga unakuta kakaranga kadogo kamesinyaa

Niliwahi kulima mahindi ya DK Singida sikupata vizuri kama nilivyokuja kulima tumbili

Nadhani serikali kupitia wataalamu wa kilimo wangefanya utafiti wa aridhi yote tanzania na kutupa muongozo wa kila aridhi inafaa mbegu gani na mbolea gani

Kenye wamejitahidi sana katika hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…