Matumizi ya Postinor 2

reginahope

Senior Member
Joined
Mar 26, 2013
Posts
163
Reaction score
30
Habari wanajf.

Napenda kuuliza hivi ni kweli hz dawa aina ya postonr 2 zinazuia mimba kwa kumezwa baada ya sex na je hazina madhara yoyote.

Napenda kujua zinafanya kazi vp hadi kuzuia mimba.
 
Kawaida yai(ovum) likishapevuka linatoka kwenye ovary,ikisha linasafirishwa mpaka kwenye fallopian tube ambapo husubiria mbegu ya kiume ili lirutubike,na likirutubika linasafirishwa mpaka kwenye mfuko wa uzazi na hatimae ujauzito.

Postinor 2
ni dawa yenye active ingredient inayoitwa levonorgestrel ambayo ni homoni ya kike inayozuia au kuchelewesha kupevuka kwa yai,au inazuia kusafirishwa kwa yai lilokwisha ungana na mbegu ya kiume kutoka kwenye mfuko wa fallopian tube kwenda kwenye nyumba ya uke(Uterus).Dawa hii hubadilisha pia uterine lining na husababisha mabadiliko ya ute/utelezi/unyevyunyevu unatolewa kwenye uke ambapo kupelekea kushindikana kwa yai kujiekeza kwenye mfuko wa uzazi(Uterus).


Madhara ya Postinor 2
  1. Kuongezeka au kupungua kwa damu ya hedhi
  2. Damu ya hedhi isiyokuwa na mpangilio
  3. Kutapika
  4. Kichefchef
  5. Kizunguzungu
  6. Maumivu ya kichwa
  7. Maumivu ya matiti
  8. Uchovu

MUHIMU
😀awa hii inapaswa kutumika mpaka masaa 72 tangia ulipokutana kimwili na mtu bila kinga baada ya muda huo haitokuwa na manufaa yoyote.

USHAURI
:Tumia kinga(mpira) kuepuka kupata mimba ambazo hujapangilia au tumia njia za uzazi wa mpango.
 

USHAURI
:Tumia kinga(mpira) kuepuka kupata mimba ambazo hujapangilia au tumia njia za uzazi wa mpango.
mimi49, Dr MziziMkavu kwa maelezo hayo kwenye blue hii dawa inamadhara kama utasoma kiumakini. Ushauri tafadhali.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…