Matumizi ya SMS na Simu yanapungua, wamejua na wanaongeza bei za data

Matumizi ya SMS na Simu yanapungua, wamejua na wanaongeza bei za data

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Kwenye mawasiliano mtu anaweza kutumia SMS au simu za kawaida kuwasiliana. Hata hivyo uwepo wa internet unaonesha watu wengi wanapiga simu kwa namna nyingine tofauti na kutumia ujumbe kwa njia nyingine zaidi ya SMS.

Uwepo wa mitandao kama WhatsApp, Telegram etc unaonesha watu wanaweza kupigiana na kutumiana ujumbe huko badala ya kutuma sms au kupiga simu kawaida.

Badala ya kuheshimu matumizi haya ya internet bado bei za data zimezidi kwenda juu kama kukomoa watu wanaotumia njia hizo kuwasiliana. Bila kujua athari zake sio tu kwenye mawasiliano bali shughuli nyingine za kiuchumi ambazo kimsingi zinatumia internet kufanya kazi katika uchumi huu wa kidigitali.

Hapa chini nawaonesha trends za sms na simu, zinavyopungua. Data nimezitoa kwenye ripoti za kila robo za TCRA.

1666587323136.png

Niwakumbushe sera ya TEHAMA ya Tanzania ya 2016 imetaka uwepo wa internet thabiti na yenye gharama nafuu.
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Maswali mawili kwa mtoa mada:-

1) Hizo units ni Idadi ya calls, au duration, sekunde, dakika au nini - hebu toa ufafanuzi tupate kuelewa zaidi.

2) Hizo ni takwimu ni za hadi kufikia Novemba mwaka jana, je hali ikoje kwa sasa, kwa mfano hadi kufikia Oktoba mwaka huu?
 
Back
Top Bottom