Matunda kuoshwa na sabuni DAR.......

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,282
Reaction score
117,244
Sijui kama watu wengi wanajua hii

imeingia fashen ya 'kuosha matunda na sabuni ya unga Dar...

matunda kama machungwa,maembe,matikiti....kwa wauza matunda hasa wa barabarani...

ukiona matunda yanang'aa sana na unayatamani.....basi probably ndo hayo...

sasa sijui hili lina madhara gani....kwa watumiaji...
 
eti nini? we umeyatoa wapi?

mimi nimeona kwa macho
kariakoo na tegeta..
wanayaosha na sabuni na kuyafuta na vitambaa
yanang'aa mno halafu...

ndo mbinu ya biashara wamegundua...
 
Kama yanasuuzwa vizuri sidhani kama kuna ubaya. Kungekua na ubaya hata vyombo tunavyolia vingesababisha matatizo.
Sema ile harufu sasa. . . .
 
mimi nimeona kwa macho
kariakoo na tegeta..
wanayaosha na sabuni na kuyafuta na vitambaa
yanang'aa mno halafu...
ndo mbinu ya biashara wamegundua...
we ukitaka kuyala huyaoshi? si utaosha tena?
 
Kama yanasuuzwa vizuri sidhani kama kuna ubaya. Kungekua na ubaya hata vyombo tunavyolia vingesababisha matatizo.
Sema ile harufu sasa. . . .


kumbee
mimi nilikuwa sijui its ok....
 
kumbee
mimi nilikuwa sijui its ok....

Nimesema "sidhani". Hata hivyo sabuni sio sumu, otherwise usingekua unaosha vyombo vyako na sabuni. Sema kama hawasuuzi wanafuta tu huo ni uchafu mara mbili.
 
Mimi naona iko poa, ila wayasuuze vizuri.
 
hata mimi huwa naosha na sabuni kabla ya kuyahifadhi kwenye fridge.
 
Matunda mengine unakuta yaliwekewa pesticides ili kuyakinga na vijidudu, so ni vizuri kuosha na sabuni hasa yale matunda yanayoliwa na maganda yake mf. apples. Kwa matunda kama nanasi, tikiti maji au ndizi sidhani kama kuna ulazima.
 
Hii inanikumbusha kuna miaka nilipita na Dakar, Senegal nikakuta wa Senegali wanaosha nyama kwa sabuni (wanaifua) kabla ya kuipika. Kuuliza nikaambiwa hao ni Waislaam na dini yao inawaambia wasile damu, kwa hiyo wanahakikisha nyama haibaki na damu kabla ya kuipika.

Umeona mambo hayo? sisi huku tunaiosha kwa maji tu na kuipika (nyumbani) wauza mishkaki mitaani huko mwiko kuosha nyama, wanakuambia unaitoa ladha, hapo sasa.
 

hao waislam wa senegal kiboko...lol
 
kuna mtu tunafanya nae ofisi moja
yeye ni mpenzi wa matunda na akiisha nunua
ni lazima ayaoshe na sabuni, tena ya unga.
haya ndo mambo ya ajabu ninayoyaona huku mjini huko kwetu huwa
hakuna mambo kama haya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…