Matunduizi's Journal: mambo mbalimbali ninayojifunza kila siku kutoka katika vyanzo mtambuka

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Unapoamka asubuhi, amka kama simba dume, usiamke kinyonge kama nyumbu.

“Arise like a lion to serve your Creator in the morning” (Shulchan Aruch 1,1)

Kuna uhusiano mkubwa kati ya jinsi unavyoamka na jinsi siku yako itakavyoisha.



comment chochote kitakachokuvutia. nitakupa like.

TUPIA CHOCHOTE CHEMA NA CHANYA AMBACHO UMEJIFUNZA SIKU YA LEO HAPA KINACHOHUSU JAMBO LOLOTE.
 
mtu mvivu ni kama bawabu ya mlangoni.
anabadilisha mapozi tu kitandani ila anabaki hapohapo hata wakati wa kuzalisha
 
Kitabu cha injili ya barnaba ni fake. Usikiamini wala usikitegemee popote utakapokikuta licha ya kuwa ni kikubwa kuliko wenda agano jipya nzima ukiliunganisha.
 
martin luther Jr na Mahatma Ganthi wakiwa kwenye umri wa adolesensi waliwahi kutaka kujiua
 
Namba moja nimekuelewa sana, ndio staili yangu ya kuamka. Hara nilale vipi ukilitaja jina language nashtuka usingizini
mkuu utakuwa Myahudi wewe. Maana hii ni kauli mbiu ya wayahudi wengi hata huo mstari nimeutoa kwenye mavitabu yao.
kweli tusilalelale hovyo kama komba.
 
Jihadi ya kweli ni kukomaa wewe na familia yako kwenda peponi. usipigane kwa sababu ya dini. Hata shetani atakushangaa.
 
nimejifunza.
kama baba wa familia alafu ni mkristo unapopanga kujenga nyumba ujenge na kachobisi flani kwenye chumba chako kwa ajili ya SALA. Humo utakuwa peke yako au na mke wako kukutana na Mungu.

wengine wanaiita madhabahu. Hii haiingiliani na ibada za familia sebuleni.
 
sio kila kitu majibu yake ni maneno.
kuna mambo mengi sana ambayo unajibu maneno wakati jibu lake lilipaswa kuwa UKIMYA.
 
ni ujinga kushangaa kwa nini unachukiwa bila sababu.siku zote tambua utachukiwa bila sababu. USISHANGAE MAMBO YA Kawaida.
 
Kuna ugonjwa wa akili unaoitwa Chelophobia. mtu anaoumwa ugonjwa huu muda wote anataka kujifanya yuko siriasi tu na hapendi kuhave fun.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…