Morani75 & Fundi Mchundo.....nisaidieni yafuatayo.....
1.Hivi barabara zetu zinafanyiwa safety audits?
2.Nini sifa za Highway
Ogah,
Swali lako la kwanza sintakujibu maana miye nipo Sikonge na huku hata Tabora mjini kwenyewe barabara za lami unaweza kuzihesabu kwa kwa vidole vya mono mmoja.
kwanza nianze na MATUTA. Mie ni MPINZANI mkubwa sana wa MATUTA kwenye HIGHWAY. Kama mtu wa fani hii NALAANI sana kuweka MATUTA kwenye high way, ila kwenye MIJI yote naweza kusuport kwa kiasi fulani hasa sehemu za makazi ya watu sehemu za speed ya 20-30km/hr. Kama mtu wa fani hii nasema Express Road, Highway roads haziwezi kuwekewa MATUTA.
Sifa kubwa ya HIGHWAY kwa nchi nyingi ni kuwa:-
-Zinakuwa na fance.
-Speed yake inakuwa ni around 120/130km/hr na hawaruhusu binadamu kupita juu ya hizi barabara au Matrekta. Lane zake zina upana wa mita 3,50 hadi 3,75m. Kwa hiyo kama kuna lane 4, inakuwa 7x2. Kuna kistreep cha ndani ambacho kinakuwa na 0.5m na kwa nje sehemu ya kusimama kwa dharura inakuwa na 3.m. Ukichukulia na msitari unaogawanya ambao tuseme uwe na mita 3, highyway utaona inakuwa na kama mita 25 upana. Hapo ukiongeza na yale lile eneo liitwalo la Roads Right, highway inaweza kuwa na upana wa mita 120.
-Alivyosema Morani ni kweli kuwa Highywa inaunganisha miji mikubwa. Sasa ni ukiona hata watu wa Kimara wanatumia hiyo barabara ujuwe hiyo si HIGHWAY. Hiyo sana sana ni National Road tu na kwa maana hiyo Class yake iko chini sana.
-Highyway inatakiwa zipite mbali na miji ili kuzuia hiki kizaazaa cha ajali. Mkipata balaa highway ikapita kwenye kijiji chenu basi kijiji huwa kinakuwa kama kimepata mpaka.Inabidi wahandisi wajenge kitukama VIADUCT (madaraja) ambayo watu, magari, wanyama nk watapita kutoka upande mmoja kwenda mwingine ingawa kisheria ni HIGHWAY siku zote lazime iwe chini na barabara la Low class zinakuwa juu.
-Kitendo cha Wahandisi kupitishia hii waiitayo HIGHWAY kwenye vijiji ni makosa ya hali ya juu. Inabidi ipite msituni tu kama ilivyo Train na sana sana karibu na miji na hapo barabara ndogo zinzwekwa kwenda kwenye hiyo miji.
-Ukishapitisha barabara ndani ya vijiji hiyo haiwi HIGHWAY tena. Inabidi kuweka vitu vingi sana kuzuia speed. Na si MATUTA tu husaidia kupunguza speed. Unaweza weka hata surface course ya mawemawe na hivyo kila asogeaye pale hupunguza speed ingawa si sawa na kujibamiza kwenye tuta.
-Waweke KAMERA zinazopiga picha magari yanayopita kwa speed kali. Hizi zinaweza wekwa kila sehemu palipo na hizi alama za kupunguza speed.
-POLISI wawekwe wengi hasa wa kiraia na kuwe na tuseme gari lenye kamera na kila RAIA akivuka sehemu ya barabara pasipo na alama za kuvuka, akamatwe na hapo alipishwe sh. 10,000 au akafanye kazi za kusafisha mji.
Ila hii sina uhakika nayo maana Kuanzia juu hadi Chini, tanzania ni Curupt. Ila kama juu wangelikuwa makini, YES WE CAN.