Mauaji ya Albino: Kushindwa kwa serikali?

Mauaji ya Albino: Kushindwa kwa serikali?

Unafikiri wangekuwa wanauawa watoto wa viongozi mpaka leo wasingekamatwa wahusika kwa hili kunakitu nyuma yake Albino ni watu kama sisi wengine
 
Inahitajika research ya ndani sana. Ninafahamu mmang'ati mmoja alivunjika mguu kwenye ajali akalazwa hospitali. Wakati akiendelea na matibabu, ikaonekana amekuwa kilema. Ni ajabu sana kwamba ndugu zake, walimwekea sumu kwenye chakula akafariki. Niliumia na sikutaka kusikiliza hizi hadithi za makabila na walemavu.

Wale walifahamika wamempa sumu kwa kuwa walikuwa wakibishana pembeni huku watu wengine wakisikia. Eti sababu hataweza tena kutembea na mifugo.

Hoja yako ni ya msingi. Inatakiwa utafiti juu ya hili suala.

Lakini HAKUNA JUSTIFICATION YA KUUA BINADAMU NO MATTER YUKO NA ULEMAVU GANI. MAUAJI YOTE HAYO NI USHETANI WA HALI YA MBAYA SANA.


hebu tuwe wakweli tatizo hili liko kanda ya ziwa tu? mbona sijaona albino mmasai au mchagga? mbona sijaona kiwete mmasai? wakizaliwa huwa wanaenda wapi?
 
Nimeona kupitia vyombo vyetu vya habari, ndugu zetu Albino wa ukanda wa ziwa, wakilalamika kuwa wanahisi kuwa wanasiasa wetu wa nchi hii, wanathamini maisha ya Tembo wetu kwenye mbuga mbalimbali za Taifa wasiteketee, lakini wakati huo huo hawajali jinsi Albino wanavyozidi kuteketezwa kwenye nchi hii kila kukicha!

Wametoa mfano kuwa wakati tembo wetu walipokuwa wakiteketezwa kiasi cha kutisha kwenye mbuga zetu, wanasiasa wetu walianzisha Operesheni Tokomeza Majangili, lakini wakati huo huo hawajashuhudia hapa nchini, pamoja na Albino wanazidi kuteketezwa, hakuna wakati wowote wanasiasa wetu, wamekuja na mkakati wa Operesheni Tokomeza Wauaji wa Albino.

Kwa mazingira hayo, naamini kwa mtu yeyote ataungana mkono na Albino hao kuwa wako sahihi kuhisi kuwa maisha ya Tembo wetu kwenye mbuga za wanyama yana thamani zaidi, kuliko maisha ya binadamu wenzetu Albino!

Vile vile tunapata ushahidi wa mazingira kuwa masterminders wa mauaji ya Albino hawa, ni wanasiasa wetu,kwa imani za kishirikina kuwa viungo vya Albino vitawapa 'mvuto' mkubwa sana, kiasi kuwa watapata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Ushahidi huo wa mazingira kuwa main suspects wa mauaji haya ya Albino kuwa ni wanasiasa wetu unazidi kupata nguvu, kwa kuwa rate ya kuuawa Albino huwa inapanda sana, kila ifikapo mwaka wowote wa uchaguzi mkuu.

Hebu tulijadili kwa pamoja suala hili zito sana linalohusu uhai wa binadamu wenzetu, unavyozidi kuteketezwa na watanzania wenzetu, kwa kile kinachoonekana ni kwa ajili ya imani za kishirikina.
 
Kwa nini Operesheni Tokomeza isiwepo kwa wauaji wa albino
Ndilo swali kubwa wanalouliza hao ndugu zetu wa Albino ya kuwa kama wanasiasa wetu walianzisha 'chapuchapu' Operesheni Tokomeza Majangili, wanaoua Tembo wetu, wanashindwa nini basi kuanzisha Operesheni Tokomeza wauaji wa Albino?!

Hicho 'kigugumizi' cha kutotaka kuanzisha Operesheni Tokomeza wauaji wa Albino, ndiyo inayowajengea hisia ndugu zetu wa Albino kuwa masterminders wa mauaji hayo ya Albino, watakuwa wenyewe wanasiasa wetu!
 
Nina maanicha Kwa kua selikali inaongozwa na ccm wangekua siliasi na kukemea mauaji ya ndugu zetu Kwa hili CCM hawa kwepi sio
 
Jamani wana JF tujadili kuhusu haya mauaji ya albino,yaani wanauawa kama vile hakuna serikali,wanasiasa wanalaani lakini mtoto wa mkulima aliposema wauaji nao wauawe bunge likaja juu,tafadhali changieni
 
Kwa watanzania nilazima tuache upumbavu kuona binadam aliezaliwa kama wewe ati anaweza kukutajirisha kwa kiungo chale tuache imani za kipumbavu kabisa
 
MWENYEKITI wa Chama
cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema),
Freeman, ameisema
Serikali ya Rais Jakaya
Kikwete imeshindwa
kutetea watu wenye
ulemavu wa ngozi
(albino) na vikongwe,
kwa kuwa inanufaika na
mauaji yao.
Amesema, Kikwete na
serikali yake imeshindwa
kuwalinda watu na mali
zao wakiwemo albino
ambao wanatekwa,
kupotezwa na kisha miili
yao kuokotwa ikiwa
imekatwa baadhi ya
viungo. Ni kwa sababu,
Kikwete na marafiki zake
wananufaika na mauaji
hayo. Habari kamili soma
----------- ONLINE.Source:Mwana.halisi forum
 
Kusema ukweli issue ya albino inasikitisha sana, rais (mzee wa kutembelea wafiwa na matamko) hajasema chochote hadi sasa!!!

Kama alivyosema Okwi hapo juu... nguvu iliyotumika kwenye operesheni tokomeza, na mwamko wa serikali kulinda albino!!

It is sad

Thanks Kamanda Mbowe
 
Mbowe yuko sahihi 100%, nakumbuka kuna mwandishi wa BBC alifanya investigative journalism, akafanikiwa kumrekodi mganga wa kienyeji aliekuwa anatuma watu waue Albino, wakati mwandishi huyo anafanya hivyo, Serikali ya MKWERE imelala. CCM wanahusika na uhalifu huu
 
Back
Top Bottom