Mauaji ya Albino: Kushindwa kwa serikali?

Kwa jinsi wanavyoelezewa hao usalama wa taifa huku mitaani najiuliza kua labda uwezo wao umepungua kiutendaji ama wafanya kusudi pengine rushwa au wamebadilishiwa majukumu
 
Ndugu zangu. Ninaomba tufumbue macho yetu sote tuone, tutumie akili zetu kutafakari na mioyo yetu iwe na amani kwa maamuzi tunayofikia.

1. Ni idara gani ya serikali iko kwa ajili ya wananchi kwa sasa? Mwenye jibu aseme.

2. Ni idara gani inayoongozwa kwa kutumia wasomi waadilifu na wazalendo waliojaa nchi nzima zaidi ya wateuliwa kwa misingi isiyo na maslahi ya taifa?

3. Si kweli kwamba, ikiwa kuna wasomi walioko kwenye system, hawakuteuliwa kwa ajili ya usomi wao ili wautumie kwa maslahi ya taifa zaidi ya mahusiano ya kibinafsi na watawala?

4.Ni lini kwa mara ya mwisho serikali ya ccm imechukua hatua zinazoonyesha kwamba iko na inajali maisha ya Watanzania katika idara zake zote, kama si pale tu kwa namna moja palihusisha uhai wa ccm na usalama wa familia tawala?

5. Hii inatofauti gani na tawala za Saddam Hussein aliyekuwa akiishi maisha ya juu sana na familia yake, pamoja na jamaa alikouwa karibu naye hapo baghdadi wakati raia wengine wakitembea, wanawaza mauti zao zitakuwa za namna gani. Angalieni walivyokuwa wakiishi kama ngedere, wakizikwa wanaume na vijana wa kiume kwenye makaburi ya pamoja, wengine wakitwangwa kwenye motor za kokoto wakiwa hai katika nchi ya maziwa na asali. Iraq ya Saddam.

6. Ni dhahiri kwamba ccm na serikali yake haipo kwa ajli ya watanzania wa kwenye peripherals. Hii tusahau ndugu zanguni.. Serikali iko kwa ajili ya kulilnda maslahi ya viongozi wa ccm na watawala tu!. Hamjifunzi kwa katiba pendekezwa?

Hamwoni huduma zote za Afya? Miundo Mbinu? Polisi? TISS hao? Elimu? Kilimo? Tamisemi? Katiba? n.k, ni kwa kiasi gani vinafanywa kuwa mbali na maslahi ya wananchi wa kawaida huku vikitoa mwanya kwa watawala kujiimarisha na kujijengea maisha safi wao na vizazi vyao?

Tufungukeni macho. Tutakwisha. Kwa suala la Albino, ni sawa na suala lingine lolote linalohusu usalama wa sisi watanzani wa kawaida. Tusitegemee serikali ya ccm. Hiyo haipo kwa ajili yetu ndugu zangu. Tuliunda majesi ya sungusungu ili kujilinda na ndiyo yamekuwa msaada mkubwa kwa usalama wetu kuliko hao polisi warugaruga wa ccm.

Ninashauri, bila kuchelewa, tuunde kitengo katika Sungusungu zetu. Kitengo cha inteligensia ambacho kitajumuisha kila sungusungu, maalumu kuangalia na kusimia suala la ukataji viungo vya binadamu kwa ushirikina ikiwemo albino.

Tutawadhibiti tu, badala ya serikali. Serikali si ya kwetu. ni ya viongozi wa ccm na watawala.
 
Reactions: BAK
Binafsi siamini kama usalama wa Taifa wameshindwa, Nahisi kuna namna wanasiasa wanahusika kwa namna moja ama nyingine.

Na mtandao wao ni mkubwa na haigusiki kama wa madawa ya kulevya.
 
Naamini hakuna usalama wa Taifa bali kuna genge la watesaji wapinzani, nilikua nasikililiza kipindi cha Madawa ya Kulevya Radio ya Upendo ni aibu kubwa sana BAK
 
Last edited by a moderator:
Naamini hakuna usalama wa Taifa bali kuna genge la watesaji wapinzani, nilikua nasikililiza kipindi cha Madawa ya Kulevya Radio ya Upendo ni aibu kubwa sana BAK

Mkuu Elli , zamani ilikuwa mtu akisemwa kuwa huyu ni Usalama wa taifa kila mtu anataka ampe favor yeyote ili hata kama ni kumnunulia soda au kumpa lift. Sasa hivi ukijitaja kuwa wewe Usalama wa taifa ujue umetangaza uadui na wanaokuzunguka.
Na kwa ukweli kabisa, hii Taasisi imeharibika sana hii awamu ya nne ya uongozi.
 
Last edited by a moderator:

Ukitaka kuwajua usalama wa taifa we anzisha mgomo au andamana. Huna hata nusu saa utajikuta unateswa
 
Waswahili wanasema mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe, hili jambo sababu hakuna ndugu zao na watoto wao ndo maana haliwagusi, iliyobaki wananchi tuungane tuingie mzigoni wenyewe hakika kwa pamoja tunaweza, ingelikuwa kuna watoto wao hadi FBI wangeletwa kusaidia hilo jambo.
BAK kwanini mambo haya in kipindi cha uchaguzi tu? Kuna nini hapa?????
 
Last edited by a moderator:
Kila kiongozi anakemea , wananchi tunasikitika, wanaotakiwa kutulinda nao wanakemea, wateja wa hivyo viungo ukute nao wanakemea tena kwa nguvu na wakati huo huo mauaji yanaendelea bila kukoma. Sasa tujiulize ni nani mwenye jukumu la kulinda wananchiiii
 
Wewe ndio uachane na uvivu wa kufikiri, kazi ya vyombo vya dola ikiwemo huo usalama wa Taifa, unadhani hawa wanauawa ama kunyofolewa viungo vya mbali mbali wangekuwa watoto wa viongozi unadhani hili tatizo lingedumu muda mrefu kiasi hiki!? Uwe una tafakari kwa kina badala ya kukurupuka na kuandika pumba.

Tatizo ni la jamii nzima na kuna vyombo husika ambavyo vinatakiwa kusimamia hili tatizo kuhakikisha linatokomezwa kabisa, kuendelea kuwepo kwa tatizo hili ni ushahidi tosha kwamba vyombo hivyo vimeshindwa kwenye utendaji wake wa kupambana na tatizo hili.


Hili tatizo ni la jamii nzima sio mtu mmoja au taasisi moja.acheni uvivu wa kufikiri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…