Mauaji ya Albino: Kushindwa kwa serikali?

Mauaji ya Albino: Kushindwa kwa serikali?

Jamani, hivi solution ya mauaji ya albino ni nini? ina maana selikali imeshindwa? au kwasababu viongozi wenyewe ndo wanashindaga huko kwa waganga na wametandaza hirizi kwenye viono vya vitambi vyao mle ndo maana wanasuasua kulimaliza?

Hawa waganga ni kuwafuta tu ili tz tusiwe na kitu inaitwa waganga wa jadi. kwasababu hawa walianza kuwaula watu wenye vipara na viungo vyao kupelekwa kwa waganga. watu wenye vipara walikuwa na wakatu mgumu sana nakumbuka kipindi fulani. ikaja watu kuchunana ngozi na kuipeleka kwa mganga. kule mbeya kulikuwa na upigaji watu nondo halafu ile nondo wanasema inapelekwa kwa mganga wa jadi aiuze kwa wenye mabusha ati ile damu aliyompiganayo mtu nyama zitatoka sana. wamekuja kwenye kung'ofoa viungo vya siri na kuviuza, hawa waganga wa nini? we need to solve this prob as soon as possible,

kwasababu, kuna siku wakimaliza albino, wataanza watu warefu na mangongochi kama sisis, wakimaliza hao watakuja watu wafupi, pengine watakuwa watu wanene, itafika kipindi yaani hapakaliki...hahaha. sasa hawa waganga wana nini haswa hata kutuyumbisha kiasi hiki? wahusika wa dola wanashindwa nini kuwashughulikia hawa watu, hivi waganga wa kienyeji wana faida kweli hapa tz? mbona ulaya watu wanaishi tu bila hawa waganga bwana....mi naona tuwafute, sheria itungwe kukataza uganga zt. nyie mnasemaje wajemeni.

...hawa (waganga wa kienyeji) ni sawa na wale wanaopromote ethnic cleansing! Tatizo nilionalo kwa viongozi wetu kuogopa kukemea suala hili kwa ukali, au kulitungia sheria ni 'jinsi tulivyo' na imani potofu ya kuwaogopa/kuwasifia watu wa Sumbawanga, mlingotini, nk kwa madunguli yao!

Ndio tamaduni hiyo, it's here to stay!
 
Watakaofuata ni MAFISADI na vizazi vyao.......

Tanzanianjema
 
Hivi yule mganga alie ojiwa hatua gani imechukuliwa!? au ndi hadi tume iundwe

Una maana mganga atato ushauri kwa mteja iwapo anataka utajiri basi akamletee kichwa cha mjukuu wa waziri??..nchi itakuwa ndogo...!!!
__________________


Sio tu kichwa cha mjukuu me nadhani cha mke ama mume wa waziri ndio hatua itachukuliwa, tumechoshwa na haya mauwaji ya ndugu zetu malbino.
 
hahaha, hii inatisha. kama hao waganga wangesikia, basi waelekeze mambo yao kwa mafisadi, nafikiri ndo mafisadi wataisha nchini humu...hahaha.(just kidding) i don't promote murder hata siku moja.
 
Albino aliyenusurika kuuawa aomba hifadhi hospitaliNa Osoro Nyawangah, Geita

BINTI mwenye ulemavu wa ngozi (albino), Bibiana Mbushi (10), ameuomba uongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Geita kumruhusu pamoja na ndugu zake wawili waendelee kuishi hospitalini hapo ili asiuawe na watu waliomkata mguu usiku akiwa amelala nyumbani kwa shangazi yao.

Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili, Bibiana ambaye amepata ulemavu wa kudumu baada ya watu wasiojulikana kuukata mguu wake wa kulia na kutoroka nao, alisema anajisikia kuwa salama zaidi akiishi kwenye hospitali hiyo kuliko akirudi kwao ambako anahofu kwamba anaweza kuuawa na watu walimkosa safari iliyopita.

Akiwa na mdogo wake, Tindi Chebwa (7) ambaye pia ni albino na dada yake mkubwa, Sikujua Mbushi (13) ambaye si albino, alisema hivi sasa hakuna binadamu mwenye roho nzuri duniani zaidi madaktari na wauguzi waliookoa maisha yake kutokana na ukatili aliofanyiwa.

Alisema kuwa tukio la kukatwa mguu wake na watu wasiojulikana kulisababishwa na imani za kishirikina kwamba kuwa baadhi ya viungo vya albino vinabati ya kuleta utajiri kwa wafanyabiashara za uvuvi na madini.

“Mama yangu alifariki miaka mingi iliyopita na baba yangu pia alifariki mwaka jana, sisi tulikuwa tunaishi na shangazi yetu ambako ndiko watu hao walinikata mguu, hivyo huko naona kwamba hakuna usalama kwangu na mdogo wangu ambaye pia ni albino ila hapa hospitalini hivyo naomba watakubali kuishi hapa hapo pamoja na dada yetu kwasababu nikirudi huo wataniua mimi au mdogo wangu,” alisema binti huyo.

Muuguzi Mkuu wa hospitali hiyo, Rosemary Binamungu, aliwasema Bibiana ameshapona mguu wake na kwamba amepewa magongo ya kumsaidia kutembea na anatakiwa kurudi nyumbani kwao ili kuwaepusha na maradhi ya kuambukiza wakiendelea kuishi hospitalini hapo.

''Sasa hivi ameshapona kabisa na kwa mujibu wa taraibu zetu anapaswa yeye na wenzake waondoke, lakini tatizo lililopo ni usalama wao, nasi bado hatujui mahali salama pa kuwapeleka kama walivyoomba kuendelea kubaki hapa,'' alisema Binamungu na kuongeza kwamba uongozi wa hospitali unawasiliana na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Geita ili kulipatia ufumbuzi tatizo hilo.

Alisema kuwa watoto hao wameisahawazoea watumishi hospitali na wajinaona wako salama zaidi, kiasi kwamba hawawezi kuzungumza na mtu yeyote bila kuwepo wauguzi wanaowafahamu. Kwa mujibu wa Sikujua, Bibiana alipata mkasa huo takriban miezi mitano iliyopita ambapo watu wasiojulikana waliwavamia usiku wakiwa wamelala nyumbani kwa shangazi yao na kumkata mguu na kuondoka nao.

Courtesy Mwananchi

Tuwasaidieje hawa ndugu zetu watamalizwa
 
Hivi kwa nini viongozi wote wa sehemu ambako mambo haya yanatendeka wasiwajibishwe? Kuanzia Mjumbe wa nyumba kumi, OCD na kuendelea. Mambo haya yanatia kinyaa!
 
Mchungaji albino aishi mafichoni kwa vitisho vya kukatwa viungo
Na Burhani Yakub, Tanga.

MCHUNGAJI wa Kanisa la Free Pentecost Church ( FPCT) wa Tarafa ya Masama mkoani Kilimanjaro mwenye ulemavu wa ngozi (albino), Emmanuel Swai ametoweka nyumbani kwake na kwenda mafichoni akihofia kuuawa.


Mchungaji Emmanuel ambaye anaongoza makanisa mawili katika Tarafa hiyo likiwamo la Sawe hajaonekana kanisani wala nyumbani kwake kwa zaidi ya wiki moja sasa baada ya watu wasiojulikana kumtumia ujumbe kwenye simu yake kumtishia kumuua.


Mchungaji Kiongozi wa FPCT, Mkoa wa Kilimanjaro,Cleoper Kweka, alilifahamisha Mwananchi jana kwa njia ya simu kuwa Emmanuel ametoweka na nyumbani na kwamba haijajulikana alikojificha.


Alisema taarifa za kutoweka kwa Mchungaji huyo alizipata wiki iliyopita baada ya

watu wa familia yake pamoja na waumini wa makanisa anayoongoza kumtaarifu kuwa

kiongozi wa hawamuoni.


Mchungaji kiongozi huyo alisema baada ya kusikia taarifa hizo alikwenda Sawe

kufuatilia na kukuta mchungaji huyo hayupo na kwamba hata namba yake ya simu ya

mkononi aliyokuwa akiitumia aliibadilisha kwa kuhofia kuuawa.


Anasema mwishoni mwa wiki iliyopita Mchungaji Emmanuel alimpigia simu kumtaarifu kuwa yuko mafichoni ingawa hakubainisha mahali alikojichimia.


''Nilipopata taarifa hizi, niliwasiliana na kiongozi wa kikundi cha wanaharakati wa walemavu ambaye pia ni albino nilyetajiwa kwa jina moja la Toner ambaye yuko Tanga na kumpaa taarifa hizi na kuomba ushauri zaidi,'' alisema Kweka.


Kweka alisema aliamua kutoa taarifa hizi kwa Toner kwa kuwa ni mwanaharakati ambaye yupo mstari wa mbele kutetea haki za maalbino na pia ni mtumishi katika kituo kinachojihusisha na utoaji huduma kwa vijana na watoto wenye ulemavu, chenye makao yake makuu jijini Tanga.


Akizungumza na Mwananchi jana kiongozi huyo, Josephati Toner, alikiri kupta taarifa hizo na kufafanua kuwa Emmanuel hakubali kuwasiliana na mtu yeyote kwa kuwa haamini kama ni mtu mwema kwake na kwamba anahofia kuwa wanaweza kumtafuta na kumuua.


Hata hivyo ,Toner alifanikiwa kumuunganisha Mchungaji Emmanuel na Mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu baada ya kumpa maelezo kuwa mmoja ni mchungaji na mwingine ni mwandishi wa habari.


Katika mazungumzo naye, Mchungaji Emmanel alisema ameamua kujificha baada ya kupokea ujembe mfupi wa maadishi kwenye simu yake zikimitishia kuwa popote atakapokutwa atauawa na kukatwa viungo vyake.


''Nazungumza na wewe kutokana na imani niliyonayo kwa Toner, lakini kwa taarifa yako siwezi kujitokeza kwasababu walionitumia meseji wamesema wataniua na kukatwa viungo vyangu,'' alisema Mchungaji Emmanuel.


Mchungaji huyo alisema anahisi kuwa watu hao waliipata namba ya simu yake kwa waumnini wake na kwamba amelazimika kuikimbia familia yake pamoja na shughuli za kanisa ili kunusuru maisha yake.


Alisema kuna mambo muhimu ambayo ameyakosa baada ya kujificha ikiwamo ibada ya ubatizo wa mtoto wake ambaye alibatizwa Jumapili iliyopia wakati akiwa

mafichoni.


''Sina la kufanya katika hili ila naomba msaada wako, haya ni maisha ya mateso na sijui nitaishi hivi hadi lini,'' alisema kwa sauti ya unyonge iliyojaa masikitiko.


Baada ya kupata taarifa hizo, Mwananchi ilikwenda kwa Afisa Upelelezi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga, Seleman Nyakipande, ambaye aliwawasiliana na jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro ili waweze kushughulikia tatizo hilo.


''Nimewasiliana na RCO wa Kilimanjaro hadi hivi sasa tunapozungumza ameshatuma kikosi kwenda eneo hilo na ameaniahidi kuwa polisi wamelipa uzito wa juu tatizo hilo na kwamba watahakikisha linapatiwa ufumbuzi haraka.''


Nyakipande aliuomba uongozi wa FPCT Mkoa wa Kilimanjaro kuwasiliana na Mchungaji Emmanuel ili aende katika kituo cha polisi cha Msama ili apwewe msaada z
 
Naamini kwamba Emmanuel ni mtumishi wa Mungu alie hai na ameitwa na Mungu ili atumike na hicho kituo ni Mungu mwenyewe amempa hivyo asogope hao wanao ua mwili tu,bali amwogope Mungu na kama kweli Mungu ndie alie mweka hapo basi hakuna mwanadamu atakae weza kushindana na Mungu na biblia inasema mkiwa na juhudi katika kumtumikia Mungu basi hakuna kitakacho wadhuru,hivyo kukimbia kituo chako cha kazi ni kosa kubwa na najua hizo ni hila za shetani tu arudi kazini aendelee kuchapa injili kwa bidii sana na Mungu mwenyewe ataitetea kazi yake na mtumishi wake.
 
Albino auawa na kunyofolewa viungo
Mathias Byabato, Bukoba
Daily News; Tuesday,September 09, 2008 @00:02

Mtu mmoja albino ameuawa kinyama kwa kukatwakatwa kwa mapanga na wauaji kutokomea na baadhi ya viungo vya mwili wake, Polisi wamethibitisha. Kwa mujibu wa taarifa ya Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Arthur Magoti, kwa waandishi wa habari jana, tukio hilo lilitokea usiku wa Jumatano iliyopita katika Kijiji cha Kagondo wilayani Biharamulo.

Alimtaja albino aliyeuawa kuwa ni Sauda Ibrahimu (20) ambaye baada ya kuuawa alikatwa mikono yote miwili lakini wauaji walitokomea na mkono wa kulia. Polisi wanaamini kuwa chanzo cha mauaji hayo ni imani za kishirikina.

Aliongeza kuwa hadi hivi sasa hakuna mtu anayeshikiliwa na Polisi kuhusiana na tukio hilo lakini alifafanua kwamba Polisi wanaendelea na uchunguzi ili kubaini mtandao wa watu wanaosaka viungo vya binadamu kwa imani za ushirikina.

Mauaji ya Sauda yametokea siku chache baada ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Khamis Kagasheki kuliambia Bunge kuwa albino 16 walikuwa wameuawa nchini katika miezi ya karibuni huku mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiongoza. Mkoa wa Mwanza unaongoza kwa mauaji ya albino 16.

Wiki iliyopita Bunge la Ulaya lilitoa tamko la kulaani mauaji ya albino nchini na kupongeza hatua zilizochukuliwa na Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kukomesha mauaji hayo na kwa kumteua Al-Shymaa Kwegyir kama Mbunge wa kwanza albino nchini.

Wabunge wa Bunge la Ulaya walitoa tamko la kulaani vitendo hivyo wakati wa mkutano wao uliomalizika mwishoni mwa wiki mjini Brussels, Ubelgiji walikokuwa wakijadili masuala mbalimbali ya demokrasi na haki za binadamu. Katika maazimio yao kuhusu mauaji ya albino, wabunge hao walieleza kushtushwa na ripoti ya idadi ya albino waliouawa nchini.
 
Inasikitisha sana, hivi kweli Serikali inashindwa kufanya uchunguzi wa kina na kuwakamata washenzi wanaohusika? mimi sidhani kuwa ni vigumu kuwakamata, na hukumu kwa yoyote atakayekutikana na hatia kwa unyama huu iwe Kitanzi! hio ndio itakuwa fundisho kwa wengine , bila hivyo hawa wanyama wataendelea na unyama wao tu!! F***ing Barbarians!!!!
 
Kwanini Serikari haidhibiti haya mauhaji maana tangu nimeanza kuyasikia nikitambo sasa haya yangu mie macho.
 
Kwanini Serikari haidhibiti haya mauhaji maana tangu nimeanza kuyasikia nikitambo sasa haya yangu mie macho.

Hata wewe unaweza kuathirika. Serikali haiwezi kudhibiti majambazi yanayo hold down hospitali, mjini, Kinondoni, wataweza kweli kudhibiti mauaji ya soft target za mtu mmoja mmoja wa kumkamata barabarani ? Toka lini polisi hawa wakaweza kutafuta muuaji? Majambazi yanaua yanavyotaka, iwe albino au yeyote. Sote tunaweza kuwa waathirika wa mauaji.
 
Hata wewe unaweza kuathirika. Serikali haiwezi kudhibiti majambazi yanayo hold down hospitali, mjini, Kinondoni, wataweza kweli kudhibiti mauaji ya soft target za mtu mmoja mmoja wa kumkamata barabarani ? Toka lini polisi hawa wakaweza kutafuta muuaji? Majambazi yanaua yanavyotaka, iwe albino au yeyote. Sote tunaweza kuwa waathirika wa mauaji.

Oh really...!!! Vipi kuhusu "investigation" yako kuhusu dokta Masau....imeishia wapi?
 
Huyu si yule wa jana? Pendekezo langu ni serikali kuagiza nyani weupe kutoka Uchina na kuwafuga kwa wingi halafu kuwaachia kwenye misitu ya kanda ya ziwa. Halafu itabidi pia ifanywe kampeni ya siri ya kuwadhihirishia Wananchi wa sehemu hizo kuwa nyani weupe wana nguvu maradufu za kichawi ukilinganisha na Wananchi Albino. Nadhani hii inaweza kusaidida kwa kiasi fulani kwa vile wanaofanya uharamu huu wa kuua Albina wana IQ pngufu kwa hiyo itakuwa si vigumu kuwarubuni.
 
Huyu si yule wa jana? Pendekezo langu ni serikali kuagiza nyani weupe kutoka Uchina na kuwafuga kwa wingi halafu kuwaachia kwenye misitu ya kanda ya ziwa. Halafu itabidi pia ifanywe kampeni ya siri ya kuwadhihirishia Wananchi wa sehemu hizo kuwa nyani weupe wana nguvu maradufu za kichawi ukilinganisha na Wananchi Albino. Nadhani hii inaweza kusaidida kwa kiasi fulani kwa vile wanaofanya uharamu huu wa kuua Albina wana IQ pngufu kwa hiyo itakuwa si vigumu kuwarubuni.

Heheheheheeeee.................
 
Really..........?

Thats right... nilitegemea mtaalamu wa mambo ya Unyani kama wewe ungekuja na expert opinion kuhusu hili wazo, badala yake unakenua meno kaa nyani. You could get hired on the spot to lead this kind of one-of-a-kind, life-saving project never before seen in the whole World...
 
Back
Top Bottom