Kwa macho ya kitoto,aliwatazama,akajawa hofu. Alilia kitoto,kiganja cha mtu mzima, kikakibana kabisa kinywa cha mtoto Yohana Bahati.Sauti yake haikusikika kabisa.
Yohana Bahati hakujua kama yeye ni albino. Kwa akili za kitoto, saikolojia ya watoto, yeye alijiona salama mikononi mwa mama yake. joto la kifua cha mama, joto la manyonyo ya mama lilimburudisha na kujiona anapendwa tena yu salama.
Wanaume hawa wamemkaba...akiwa hai wanamnyofoa mikono mara miguu, maumivu makali ya visu na mapanga ya buchani yanasikika yakitenga ngozi, maumivu yanaingia ndani kwenye nyama na misuli,panga na kisu kinapogusa mfupa mchanga wa mtoto Yohana Bahati. Moyo mchanga wa Bahati unazimika. Hatimaye Bahati wa Geita kakata roho!!!
Yohana Bahati ameuawa hajui kama yeye ni albino.
Bahati ameishi mwaka mmoja na miezi miwili tu tangu aje duniani....
Kumbe Bahati hakujua kwamba yeye ni 'deal'.
Haya sasa mumeuuwa, Njooni...pandeni majukwaa ya kisiasa, tuwape "KULA" zetu. Pandeni jukwaani.
Mngetaka "KURA" zetu, MUSINGEMUUWA mtoto albino Yohana Bahati.
Mwaka 2009 waliwauwa albino wengi tu...
Wanausaka utajili...
Wauaji na wateja wanasaka vyeo vya kisiasa...
Vyeo na utajili uliojaa damu za albino....
Utajili na vyeo vyenye vilio na laana ya dunia yote.
Mabara matano ya dunia hii yamelaani mauaji haya. Visiwa vimelaani roho hii ya uroho wa madaraka na utajili ivumayo Tanzania.
Kwa heri, buriani mtoto Yohana Bahati...kifuani mwa Ibrahimu tutakuona. Pumzika mtoto mzuri...Bwana atakufuta machozi yako...usilie pumzika,,,nyamaza...Kisasi ni cha BWANA!!!
Yohana Bahati hakujua kama yeye ni albino. Kwa akili za kitoto, saikolojia ya watoto, yeye alijiona salama mikononi mwa mama yake. joto la kifua cha mama, joto la manyonyo ya mama lilimburudisha na kujiona anapendwa tena yu salama.
Wanaume hawa wamemkaba...akiwa hai wanamnyofoa mikono mara miguu, maumivu makali ya visu na mapanga ya buchani yanasikika yakitenga ngozi, maumivu yanaingia ndani kwenye nyama na misuli,panga na kisu kinapogusa mfupa mchanga wa mtoto Yohana Bahati. Moyo mchanga wa Bahati unazimika. Hatimaye Bahati wa Geita kakata roho!!!
Yohana Bahati ameuawa hajui kama yeye ni albino.
Bahati ameishi mwaka mmoja na miezi miwili tu tangu aje duniani....
Kumbe Bahati hakujua kwamba yeye ni 'deal'.
Haya sasa mumeuuwa, Njooni...pandeni majukwaa ya kisiasa, tuwape "KULA" zetu. Pandeni jukwaani.
Mngetaka "KURA" zetu, MUSINGEMUUWA mtoto albino Yohana Bahati.
Mwaka 2009 waliwauwa albino wengi tu...
Wanausaka utajili...
Wauaji na wateja wanasaka vyeo vya kisiasa...
Vyeo na utajili uliojaa damu za albino....
Utajili na vyeo vyenye vilio na laana ya dunia yote.
Mabara matano ya dunia hii yamelaani mauaji haya. Visiwa vimelaani roho hii ya uroho wa madaraka na utajili ivumayo Tanzania.
Kwa heri, buriani mtoto Yohana Bahati...kifuani mwa Ibrahimu tutakuona. Pumzika mtoto mzuri...Bwana atakufuta machozi yako...usilie pumzika,,,nyamaza...Kisasi ni cha BWANA!!!