Mauaji ya Kimbari ya Rwanda

Mauaji ya Kimbari ya Rwanda

TEAM 666

JF-Expert Member
Joined
Dec 7, 2017
Posts
4,399
Reaction score
8,594
9e2044e67cbb8e940e666915a402326a.jpg

Vifuvu katika Shule ya Kiufundi ya Murambi, nchini Rwanda


Mauaji ya Kimbari ya Rwanda yalikuwa mauaji ya halaiki nchini Rwanda mnamo mwaka wa 1994 ambapo Watutsi , Watwa na baadhi ya watu wa kabila la Kihutu waliuliwa na serikali iliyosimamiwa na viongozi wa Kihutu.

Katika kipindi cha takriban siku 100, kuanzia kuuliwa kwa Habyarimana na Ntaryamira tarehe 6 Aprili hadi katikati mwa mwezi Julai, walau watu 500,000 waliuawa, au karibu asilimia 20% ya idadi ya watu nchini Rwanda wakati huo.

Ujumbe wa ma jaji wa Ufaransa Jumamosi waliwasili mjini Kigali kwa lengo la kuchunguza chanzo cha mauaji ya kimbari ya Rwanda na kuanguka kwa ndege iliyokuwa imembeba Juvenail Habyarimana rais wa wakati huo wa Rwanda.

Kuuawa Habyarimana tarehe 6 Aprili 1994 kulikuwa chanzo muhimu cha mauaji ya kimbari nchini humo.

Kuhusiana na kuuawa Habyarimana, Wahutu wenye misimamo ya kufurutu mpaka walihusisha tukio la kutunguliwa ndege yake na wapinzani wa Kitutsi na kulitumia kama

kisingizio cha kuanzishia ma shambulio na mauaji makubwa na ya kutisha dhidi ya Watusi, Watwa na Wahutu wenye misimamo ya wastani.

Mauaji ya kimbari nchini Rwanda yaliendelea kwa muda wa siku 100 hadi hali ya mambo ilipodhibitiwa na vikosi vya waasi wa wakati huo wa RPF, wapiganaji wake wengi wakiwa ni Watutsi.

Inasemekana kuwa watu wapatao laki nane waliuawa, wengi wao wakiwa Watutsi, lakini wakiwemo pia Wahutu wenye misimamo ya wastani.

Huko nyuma Rais Paul Kagame wa Rwanda alituhumiwa na Jean-Lousi Bruguiere, mmoja wa majaji maarufu wa Ufaransa kuwa alishiriki katika mauaji ya halaiki ya wananchi wa nchi hiyo na vilevile mauaji ya Habiyarimana.

Hatua hiyo iliipelekea serikali ya Kigali nayo kuwatuhumu viongozi wa Ufaransa kuwa walishiriki katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.

Kwa utaratibu huo Kamisheni Huru ya Kitaifa ambayo iliamuriwa na serikali ya Kigali ikusanye
nyaraka na ushahidi unaothibitisha nafasi ya
Paris katika mauaji ya Rwanda, ilitayarisha nyaraka zilizofichua jinsi Ufaransa ilivyoshiriki katika mauaji hayo, ambayo yalipewa jina la "Jinai za Watenda Jinai".

Kwa mujibu wa ripoti ya kamisheni hiyo, nduru za juu za kisiasa, za kidiplomasia na za kijeshi za Ufaransa ziliratibu na kutekeleza mauaji hayo ya kimbari.

Vilevile ripoti hiyo ilisema kwamba, Paris ilishiriki katika kutoa mafunzo kwa wanajeshi na waasi wa Kihutu, kutoa silaha na suhula za kijeshi, kusaidia kwa siri mauaji,

ubakaji na mateso katika ardhi ya Rwanda. Tuhuma hizo zilivuruga kabisa uhusiano wa Ufaransa na Rwanda.

Hata hivyo mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka 2009 viongozi wa nchi hizo mbili waliamua kuhuisha tena uhusiano wao na serikali ya Paris kuwapa majaji jukumu la kufuatilia faili la mauaji ya kimbari ya Rwanda.

Wachambuzi wa mambo wanaamini kuwa, hamu ya nchi hizo mbili ya kutaka kuanzisha tena uhusiano wao wa kisiasa haiwezi kufuta shaka ya nafasi ya Ufaransa katika mauaji ya kimbari ya Rwanda.

Ufaransa ambayo siku zote imekuwa ikisisitiza kuungwa mkono ngano ya mauaji ya kimbari ya Wayahudi katika Vita vya pili vya Dunia , hivi sasa inapaswa kutoa jibu kuhusiana na tuhuma zilizotolewa dhidi yake na Kamisheni ya Uchunguzi ya Rwanda.

0274d915ed11ee3236e17683442db21e.jpg


Paul Kagame Japokuwa ni mmoja kati ya mwanajumuiya ya
Watusi , ameonekana kuuanganisha Utusi wake. Huyu ndiye mhusika mkuu wa kuondosha Uhutu na Utusi na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo (Mauaji ya kimbari ya Rwanda).

Hata hivyo, mara nyingi anatazamwa kama
dikteta kwa kuwa na rekodi mbaya ya ukiukaji wa haki za binadamu .

Kagame ameweka kipaumbele katika maendeleo ya [ taifa]], akilenga kufanya Rwanda isiwe tena kati ya nchi maskini kufikia mwaka 2020. Kweli nchi imepiga hatua kubwa katika masuala mengi, kama vile afya na elimu . Kati ya miaka 2004 na
2010 pato liliongezeka 8% kwa mwaka.

Uhusiano na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo si mzuri, hata baada ya vita kusimamishwa rasmi mwaka 2003 ; asasi za kutetea haki za binadamu zinadai Rwanda inaendelea kutegemeza makundi ya waasi ili kufaidika na maliasili ya nchi hiyo jirani, ingawa Kagame anakanusha.

TEAM B-13
 
Na Hapo Ilikuwa Ni Miezi 3 Na Siku Kadhaa Tu Wangeachwa Walikuwa Wanamalizana Hawa Jamaa Na Utulivu Uliopo Ni Wa Muda Tu Paka Akiachia Ngazi Lazima Kinuke
 
Back
Top Bottom