Mauaji ya Polisi, Sauti kutokea maeneo ya tukio haziwezi Kupuuzwa

Mauaji ya Polisi, Sauti kutokea maeneo ya tukio haziwezi Kupuuzwa

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Inatia moyo kuwa sauti zaidi zinazidi kusikika.

Kwamba:

"Machifu wa mkoa wa Mara nao pia wameomba kufanyika kwa uchunguzi wa kina kuhusu tukio la mauaji ya watu watatu yalitokea wilayani Serengeti waliouwawa kwa kupigwa risasi na askari polisi kwa tuhuma za ujambazi."

Hili ni jambo la kheri sana. Wito huu umfikie chifu mwenzao Hangaya popote kule aliko.

Inafahamika kuwa si nadra kwa polisi kujichukulia sheria mikononi na kuuwa au hata kuwapora watuhumiwa kinyume cha sheria.



Imethibitika sehemu nyingi kuwa walioporwa na hatimaye kuuwawa na polisi walikuwa wahanga wala hawakuwa majambazi.

Inawezekana hata Tarime ni yale yale ya Ifakara, Mtwara na kwingine kwingi.

NInakazia: ni aliye mhalifu pekee ndiye anayeweza kupinga kufanyika uchunguzi wa kuaminika kwenye kadhia kama hizi.

Source:

Machifu Mara wataka uchunguzi mauaji yaliyofanywa na polisi
 
Mama anafanya nini sijui wenyewe mnasema....kazi iendelee
 
Mi naona hao kweli ni majambazi, ila sababu wahusika wakuu ni mmoja wao wa ndugu za chadema.
Ndio maana wamelishikia bango...

Kuna dogo anaelekezwa nini cha kujibu, ni kwamba anayerekodi anajua na anamkumbusha tu
 
Mama anafanya nini sijui wenyewe mnasema....kazi iendelee

IMG_20220928_112538_686.jpg
 
Mi naona hao kweli ni majambazi, ila sababu wahusika wakuu ni mmoja wao wa ndugu za chadema.
Ndio maana wamelishikia bango...

Kuna dogo anaelekezwa nini cha kujibu, ni kwamba anayerekodi anajua na anamkumbusha tu

Kinachogomba hapa ni kuwa polisi wamekamata watuhumiwa asubuhi wakaenda kuwauwa usiku wa manane pasipokuwa na uhalali wowote.

Polisi wenyewe hawajathibitisha kuwa marehemu walikuwa ni majambazi. Bali wanasema waliwauwa kwa sababu walitaka kutoroka chini ya ulinzi.

NInakazia: ni aliye mhalifu pekee ndiye anayeweza kupinga kufanyika uchunguzi wa kuaminika kwenye kadhia kama hizi.
 
Back
Top Bottom