Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Waasi wa kundi la ADF wameishambulia tena wilaya ya Beni Kaskazini mwashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na kuuwa watu 22 katika tarafa za Ndombi na Kamango.

"Walipoingia walianza kuwafyetulia raia risasi, waliojeruhiwa ni wengi na waliouawa wapo. Milio ya risasi ilikuwa mingi kupita kiasi, jeshi liliingilia kati lakini lilichelewa kidogo. Isingelikuwa uingiliaji kati wa jeshi hilo, sote tungeliuwawa," alisema mmoja wa wakaazi wa Beni.
Mauwaji haya yanaendelea wakati jeshi la serikali linaendesha operesheni dhidi ya ADF, lakini wadadisi wa masuala ya usalama wanasema kuna uzembe katika uongozi wa jeshi hasa katika operesheni zinazotajwa na jeshi la Serikali kuwa ndio za mwisho kufanyika katika eneo hili, ili kuwatokomeza waasi wa ADF wanaowauwa watu kila uchao.
Mwanasheria Omar Kavota, mdadisi wa masuala ya usalama na akiwa pia naibu mwenyekiti wa mashirika ya kutetea haki za binaadamu CEPADHO, anahoji kwamba, mikakati ya kuwalindia usalama wakaazi katika viunga vya maeneo ya vita, haikupangwa vizuri kwani inajulikana wazi ya kwamba, ADF wanaposhambuliwa katika maeneo ya misitu, basi na wao wanawashambulia na kuwaua wakaazi katika maeneo ambayo operesheni bado hazijaanzishwa.
Ikumbukwe kuwa, katika ziara yake mjini Beni, na alipotangaza kwamba operesheni kabambe zitaanzishwa katika eneo hilo dhidi ya waasi wa ADF, rais Félix Tshisekedi aliwahi kuwaahidi wakaazi, kwamba waasi hao watatokomezwa kabla ya sherehe za Krismasi pamoja na mwaka mpya. Lakini ahadi hiyo inaonekana kubakia kuwa ndoto tu.

Wakaazi wa wilaya ya Beni kwa mara nyingine wanahesabu maiti za wapendwa wao waliouawa kinyama na waasi wa ADF. Mmoja wa wakaazi aliyeponea chupuchupu katika eneo la Kamango, aliyezungumza na DW kwa njia ya simu, amesema walipoingia kijijini mwake waasi hao kutoka Uganda ADF walikuwa wakiuwa watu kiholela."Walipoingia walianza kuwafyetulia raia risasi, waliojeruhiwa ni wengi na waliouawa wapo. Milio ya risasi ilikuwa mingi kupita kiasi, jeshi liliingilia kati lakini lilichelewa kidogo. Isingelikuwa uingiliaji kati wa jeshi hilo, sote tungeliuwawa," alisema mmoja wa wakaazi wa Beni.
Mauwaji haya yanaendelea wakati jeshi la serikali linaendesha operesheni dhidi ya ADF, lakini wadadisi wa masuala ya usalama wanasema kuna uzembe katika uongozi wa jeshi hasa katika operesheni zinazotajwa na jeshi la Serikali kuwa ndio za mwisho kufanyika katika eneo hili, ili kuwatokomeza waasi wa ADF wanaowauwa watu kila uchao.
Mwanasheria Omar Kavota, mdadisi wa masuala ya usalama na akiwa pia naibu mwenyekiti wa mashirika ya kutetea haki za binaadamu CEPADHO, anahoji kwamba, mikakati ya kuwalindia usalama wakaazi katika viunga vya maeneo ya vita, haikupangwa vizuri kwani inajulikana wazi ya kwamba, ADF wanaposhambuliwa katika maeneo ya misitu, basi na wao wanawashambulia na kuwaua wakaazi katika maeneo ambayo operesheni bado hazijaanzishwa.
Ikumbukwe kuwa, katika ziara yake mjini Beni, na alipotangaza kwamba operesheni kabambe zitaanzishwa katika eneo hilo dhidi ya waasi wa ADF, rais Félix Tshisekedi aliwahi kuwaahidi wakaazi, kwamba waasi hao watatokomezwa kabla ya sherehe za Krismasi pamoja na mwaka mpya. Lakini ahadi hiyo inaonekana kubakia kuwa ndoto tu.