Maumivu ya mtoki

Maumivu ya mtoki

Joyceline

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2009
Posts
1,010
Reaction score
167
habari zenu wapendwa

Nina mdogo wangu anaumwa sana mtoki tangu juzi, hana kidonda wala infection yoyote.
akienda hospital doctor anamwambia anywe dawa za maumivu tu na hazimsaidii.
Ila kuna mtu kaniambia kwamba mawazo makali sana pia yanasababisha mtoki tena ambayo umeyawaza masaa matatu kabla ya kuanza kuumwa, naomba mwenye uelewa aniambie na anayejua tiba.
 
jaman mdogo wangu anakauvimbe kati ya paja na nyonga upande wa kulia kanavimba halafu baada ya muda kanapotea kakiambatana na maumivu nilimpeleka hospital akaambiwa ni mtoki
amekunya flucamox na ampliclox lakin bado hakaishi ameipiga ultrasound hawajaona kitu akapewa dawa tena lakini bado kanauma na kupotea anapata maumivu hadi kwenye kitovu ikiambatana na gesi pamoja na tumbo kuunguruma. tunaomba msaada wana jf maana ni mwezi mmoja na nusu sasa anapata shida
 
mpeleke muhimbili (kama mpo dar es salaam) pale mtapata jibu tu!
 
Nauliza kuwa kuna uhusiano gan kati ya kuwa na kidonda mahali fulan mwilini hasa miguuni na kutokwa nauvimbe maeneo ya joint za mapaja na kiuno (mtoki)
Naomba msaada wenu
 
Back
Top Bottom