Mavazi yanayofaa kuvaa wakati wa Usahili 'interview '

Mavazi yanayofaa kuvaa wakati wa Usahili 'interview '

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
IMG_20210426_132902_009.jpg


Vaa aina ya mavazi yanayokuonesha kuwa ni nadhifu na uko makini 'professional' .

Kwa mwanaume unaweza vaa suti, au shati na suruali ya kitambaa, pamoja na kiatu cha kufunika cha kiofisi.

Mwanamke unaweza kuvaa blauzi na sketi nzuri, isiwe fupi au ndefu sana hadi kukuletea usumbufu, vilevile unaweza kuvaa suti. Epuka viatu virefu sana na vyenye kutoa sauti kubwa unapotembea.

Aidha, rangi ya nguo ya bluu, nyeusi na hudhurungi ni rangi ambazo zinapendeza zaidi kwenye Usahili.
 
Upvote 1
Kabisa na hakikisha kwa wanaume lau rangi ya kiatu inafanania na mkanda.
Pili usiwe unatafuna kitu mdomoni kama chewing gum. Huwa tunaziita bigG
Hakikisha umeoga wengine huwa nanakuja na vile vijasho visivyo rasmi hadi board room inajaa majasho. Sijui huwa inakuwa ni woga au nini
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom