Mawakala wa Tanzania mbona hatuoni kazi yenu

Mawakala wa Tanzania mbona hatuoni kazi yenu

Mndengereko One

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2015
Posts
340
Reaction score
243
kama sikosei tanzania ina mawakala sio chini ya saba lakini naona kama hamna wakala vile nao wakumbuka saidi tuli,hemed remtula,salehe ally,yussufu bahresa, John ndumbaro na jamal kisongo lakini kati ya hao sizan kama yupo aliye itendea haki said tuli sijawai kumsikia amempeleka . kwenye try yeyote.hemed remtula mchezaji wa mwisho kumsikia pale alipo muuza heri josephu baada ya hapa sikumbuki kama aliwahi kupeleka mwingine.salehe ally hapa nisiwe muongo huyu wa visiwani sina ripoti zake yussufu barharesa tokea ampeleke boko israel na ngasa west ham sijamsikia tena bahati mzuri sasa hivi kwake kuna madini yapo anayaangali tu faridi musa,mudathir yahaya na himid mao hii ilikuwa biashara nzuri kwake.john ndumbaro sijaona kazi yake ata moja hapa ndo na umia zaidi namkumbuka kaka yake damas ndumaro wakala wakweli aliyekuwa tanzania wakala wa ulimwengu wakala wa bobani aliacha uwakala kwasababu wachezaji wali mwangusha aliwahi kupeleka vijana ujerumani wakafuzu wakakaa mwezi wakaludi kisa baridi aka hamua kuacha uwakala.jamali kisongo wa ukaya nilimfahamu wakati nipo kibiti kwenye mambo ya siasa ni mtu makini kufanya nae kazi amepambana na sasa amepata uwakala hili ndo tumaini pekee kwa tanzania wachezaji wetu wenye nia wafanye kazi na huyu mtu wakala wa mbwana samata,haji ungando na kuna huyu mwingine denis kadito sasa hivi ataki kufanya kazi na wa bongo wenzie ana fanya kazi na waburundi amesha mtoa abdul fiston amempeleka south sisi atutaki kisa alichofanywa na kapombe naomba tujadili hapa kwann mawakala wetu hawa watafutii timu wachezaji wetu
 
toto la kindengereko

Jifunze kuandika, bandiko bovu kama hili lisilozingatia kanuni za uandishi tegemea kuchangia peke yako.

Kama sikosei Tanzania ina mawakala sio chini ya saba lakini naona kama hamna wakala vile.

Ninaowakumbuka ni Said Tuli,Hemed Remtula,Salehe Ally,Yussufu Bakhresa, John Ndumbaro na Jamal Kisongo lakini kati ya hao sidhani kama yupo aliyeitendea haki.

Said Tuli sijawahi kumsikia amempeleka mchezaji yeyote kwenye majaribio yoyote.

Hemed Remtulah, mchezaji wa mwisho kumsikia pale alipomuuza Heri Joseph baada ya hapa sikumbuki kama aliwahi kupeleka mwingine.

Salehe Ally hapa nisiwe muongo huyu wa visiwani sina ripoti zake.

Yusuf Bakhresa tokea ampeleke Boko Israel na Ngasa West Ham sijamsikia tena bahati mzuri sasa hivi kwake kuna madini yapo anayaangali tu kama Faridi Musa,Mudathir Yahaya na Himid Mao hii ilikuwa biashara nzuri kwake.

John Ndumbaro sijaona kazi yake hata moja hapa ndio naumia zaidi, namkumbuka kaka yake Damas Ndumaro wakala wa kweli aliyekuwa Tanzania wakala wa Ulimwengu,Bobani aliacha uwakala kwasababu wachezaji walimwangusha. Aliwahi kupeleka vijana Ujerumani wakafuzu wakakaa mwezi wakarudi kisa baridi akaamua kuacha uwakala.

Jamali Kisongo wa Ukaya nilimfahamu wakati nipo Kibiti kwenye mambo ya siasa, ni mtu makini kufanya nae kazi.Amepambana na sasa amepata uwakala. Hili ndio tumaini pekee kwa Tanzania wachezaji wetu wenye nia wafanye kazi na huyu mtu wakala wa Mbwana Samata.

Haji Ungando na kuna huyu mwingine Denis Kadito sasa hivi hataki kufanya kazi na wabongo wenzie anafanya kazi na waburundi, ameshamtoa Abdul Fiston amempeleka South Afrika.

Sisi hatutaki kisa alichofanywa na Kapombe.

Naomba tujadili hapa kwanini mawakala wetu hawawatafutii timu wachezaji wetu?
 
chachu ombala kweli kama konokono ingekuwa kwenye karatasi ningekataa sio mwandiko wangu
 
wachezaji wapo ndemla faridi musa huyu mchezaji timu yeyote ulaya ukimpeleka anafuzu
 
Ili uwe mwanamichezo mzuri unapaswa kuwa na vitu hivi skills ,ambition na work ethics sasa wachezaji wetu wana fail sana kwenye ambition na work ethics
ambition ya wachezaji wetu wengi wa kibongo huwa zinaishia level ya simba na Yanga wakihojiwa utasikia wanataka kuchezea soka la kipro ila angalia jitihada wanazofanya kufika huko inakatisha tamaa hata wakipelekwa huko hawaoneshi kuwa wanania ya kufika mbali (thanks to ulimwengu kwenye hili alionesha mapema kuwa ana ambitions za kufika mahali )
work ethics mpira ni career inayoitaji nidhamu kubwa wachezaji wetu sijui ni kukosa elimu au mpira wao kutopitia kwenye academy wanafeli sana kwenye ethics kuanzia uwanjan mpk nje ya uwanjan uvutaji bangi starehe kupitiliza vitendo vya kina nyoso kuheshimu muda sasa ukizingatia kuwa uwakala ni biashara uwezekano wa faida unapokuwa finyu watu wanaamua kufanya other staff
 
Timu yoyote Ulaya? Acha masihara wewe, amakuwa nani Gaucho?

sio gaucho ila kwa uwezo wake timu nyingi ulaya anaweza kucheza na nimesikia kuna timu ya slovenia ina mtaka mm naimani huyu anafuzu
 
Back
Top Bottom