#COVID19 Mawaziri waachie Ngazi kutoa Nafasi kwa Mwanzo Mpya

#COVID19 Mawaziri waachie Ngazi kutoa Nafasi kwa Mwanzo Mpya

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Itakuwa kujidanganya kama taifa kudhani kuwa tuko vizuri.

IMG_20210218_174254_207.jpg


Matumaini mapya yaliyoibuka baada ya SSH kuchukua nchi yamekwisha baada ya siku 100 ofisini.

Kama taifa tunayumba tokea kwenye corona hadi kwenye mustakabala kama taifa. Taifa limegawanyika hisia kali na munkari juu:

1. Kuhusiana na ugonjwa hatari wa Corona:

(a) Vinara wa misimamo ya awamu ile na Corona, chanjo yakiwamo mahusiano na WHO pia na mataifa mengine wangalipo serikalini.
(b) Kuna tofauti kubwa za kimtazamo kuhusiana na Corona baina ya watu, yakiwa ni madhara ya wazi yatokanayo na misimamo na propaganda za awamu ile.

IMG_20210725_012351_122.jpg


(c) Athari za ugonjwa zinaendelea kuongezeka na watu wasio na hatia wanaendelea kufa.



(d) Tunapaswa sasa kama taifa kuzikumbatia tahadhari zote zilizokuwa zikibezwa katika awamu ile yakiwamo matumizi chanjo.

IMG_20210725_072229_590.jpg


Ni wazi kuwa tunahitaji marubani wapya kama kweli tunayo nia ya dhati ya kuyaokoa maisha ya watu.

2. Mustakabala wetu kisiasa kama taifa:

(a) Umoja wetu uliokuwapo katika siku 100 za mwanzo za SSH haupo tena.
(b) Ukiukwaji wa wazi wa sheria na katiba wenye upendeleo, yakiwemo matumizi ya dola dhidi ya makundi mengine umeligawa tena taifa.
(c) Kubambikiziwa kesi kwa Freeman Mbowe kumeongeza mgawanyo chuki zaidi dhidi ya serikali.

IMG_20210723_052829_482.jpg


Wasaidizi wasioweza kumsaidia rais kutuunganisha kama taifa, hawatufai.

3. Mustakabala wetu kiuchumi:

(a) Mwendelezo wa vigogo kutokulipa kodi, haukubaliki.
(b) Maongezeko ya kodi na tozo mbalimbali ndani ya kipindi cha ongezeko la UVIKO, hayakubaliki.
(c) Utaratibu wa gharama za matibabu ya UVIKO kuwa ni juu ya wahanga wa ugonjwa huu ambao ni janga la dunia, haukubaliki.




Manahodha wasioona umuhimu wa kila mtu kulipa kodi na kuwa ufumbuzi wenye wa haki kwenye majanga, hawatufai.

Mawaziri waliopo hawawezi kukwepa lawama kwa kushindwa kumsaidia rais kutuunganisha.

Kama wao hawauoni umuhimu wa kuachia ngazi ili kumpa Mama SSH nafasi ya mwanzo mpya wa kuisafisha hali hii, na wafurushwe tu kwa maslahi ya taifa.

Ninawasilisha.
 
Tumsaidie Mama Samia kuisafisha nchi.


Hata kwa kupiga kelele tu.
 
Tumsaidie Mama Samia kuisafisha nchi.


Hata kwa kupiga kelele tu.

Cc: BAK Erythrocyte Salary Slip Jumbe Brown
Salaam mkuu Brazaj !!!

Mh.SSH ameapa kuilinda KATIBA....najua huridhishwi na kukamatwa kwa mh.Mbowe)

Mh.Rais SSH ana ile mikono yake yenye nguvu mno kikatiba "presidential decree"...hii imemilikishwa kwake na WATANZANIA katika kuyalinda maslahi yao kiafya ,kiuchumi na kijamii.....

Ukimuangalia vyema mh.Rais wetu unamaizi ile KIU YAKE KALI NA UCHUNGU WA KUTUBADILISHIA MENGI "yanayotuzonga"....

Ninatumai tukimpa muda atatupeleka mbele sana....

********************

Hapa sitaki kukukumbushia kuwa yule Prof.Cheeseman aliyehojiwa na CNN na kuuponda sana utawala wa awamu ya 6 kumbe "ALIOKOTEZA HABARI" kutoka kwa NON-AUTHORITATIVE SOURCE 🤣🤣

#KaziInaendelea
#NchiKwanza
#UtulivuNaAmaniKwanza
#TanzaniaIsASovereignState
 
Itakuwa kujidanganya kama taifa kudhani kuwa tuko vizuri.

View attachment 1867150

Matumaini mapya yaliyoibuka baada ya SSH kuchukua nchi yamekwisha baada ya siku 100 ofisini.

Kama taifa tunayumba tokea kwenye corona hadi kwenye mustakabala kama taifa. Taifa limegawanyika hisia kali na munkari juu:

1. Kuhusiana na ugonjwa hatari wa Corona:

(a) Vinara wa misimamo ya awamu ile na Corona, chanjo yakiwamo mahusiano na WHO pia na mataifa mengine wangalipo serikalini.
(b) Kuna tofauti kubwa za kimtazamo kuhusiana na Corona baina ya watu, yakiwa ni madhara ya wazi yatokanayo na misimamo na propaganda za awamu ile.

View attachment 1867159

(c) Athari za ugonjwa zinaendelea kuongezeka na watu wasio na hatia wanaendelea kufa.

View attachment 1867123

(d) Tunapaswa sasa kama taifa kuzikumbatia tahadhari zote zilizokuwa zikibezwa katika awamu ile yakiwamo matumizi chanjo.

View attachment 1867133

Ni wazi kuwa tunahitaji marubani wapya kama kweli tunayo nia ya dhati ya kuyaokoa maisha ya watu.

2. Mustakabala wetu kisiasa kama taifa:

(a) Umoja wetu uliokuwapo katika siku 100 za mwanzo za SSH haupo tena.
(b) Ukiukwaji wa wazi wa sheria na katiba wenye upendeleo, yakiwemo matumizi ya dola dhidi ya makundi mengine umeligawa tena taifa.
(c) Kubambikiziwa kesi kwa Freeman Mbowe kumeongeza mgawanyo chuki zaidi dhidi ya serikali.

View attachment 1867140

Wasaidizi wasioweza kumsaidia rais kutuunganisha kama taifa, hawatufai.

3. Mustakabala wetu kiuchumi:

(a) Mwendelezo wa vigogo kutokulipa kodi, haukubaliki.
(b) Maongezeko ya kodi na tozo mbalimbali ndani ya kipindi cha ongezeko la UVIKO, hayakubaliki.
(c) Utaratibu wa gharama za matibabu ya UVIKO kuwa ni juu ya wahanga wa ugonjwa huu ambao ni janga la dunia, haukubaliki.




Manahodha wasioona umuhimu wa kila mtu kulipa kodi na kuwa ufumbuzi wenye wa haki kwenye majanga, hawatufai.

Mawaziri waliopo hawawezi kukwepa lawama kwa kushindwa kumsaidia rais kutuunganisha.

Kama wao hawauoni umuhimu wa kuachia ngazi ili kumpa Mama SSH nafasi ya mwanzo mpya wa kuisafisha hali hii, na wafurushwe tu kwa maslahi ya taifa.

Ninawasilisha.

Tatizo hujui serikali inavyoongozwa. Mawaziri ni was Audi was Rais na kamwe siyo decision makers!

usimdharau Samia kwa vile ni mwanamke ana maamuzi yake ambayo ndiyo yanayotekelezwa. Ni kosa kulaumu mshauri baadala ya mtoa maamuzi ambaye ni Rais.
 
Salaam mkuu Brazaj !!!

Mh.SSH ameapa kuilinda KATIBA....najua huridhishwi na kukamatwa kwa mh.Mbowe)

Mh.Rais SSH ana ile mikono yake yenye nguvu mno kikatiba "presidential decree"...hii imemilikishwa kwake na WATANZANIA katika kuyalinda maslahi yao kiafya ,kiuchumi na kijamii.....

Ukimuangalia vyema mh.Rais wetu unamaizi ile KIU YAKE KALI NA UCHUNGU WA KUTUBADILISHIA MENGI "yanayotuzonga"....

Ninatumai tukimpa muda atatupeleka mbele sana....

********************

Hapa sitaki kukukumbushia kuwa yule Prof.Cheeseman aliyehojiwa na CNN na kuuponda sana utawala wa awamu ya 6 kumbe "ALIOKOTEZA HABARI" kutoka kwa NON-AUTHORITATIVE SOURCE 🤣🤣

#KaziInaendelea
#NchiKwanza
#UtulivuNaAmaniKwanza
#TanzaniaIsASovereignState

Niko imara mheshimiwa Jumbe Brown busy kidogo kazini leo. Naamini uko vyema pia.

Nitakurejea kwa kina. Nchi ni yetu sote.

Ila tumsaidie Mama kuinyoosha nchi. Tunapopenda kumwuunga mkono naye atunyooshee mkono - "kitambaa cheupe" -- king Kiki.

Au nasema uongo ndugu yangu?
 
Niko imara mheshimiwa Jumbe Brown busy kidogo kazini leo. Naamini uko vyema pia.

Nitakurejea kwa kina. Nchi ni yetu sote.

Ila tumsaidie Mama kuinyoosha nchi. Tunapopenda kumwuunga mkono naye atunyooshee mkono - "kitambaa cheupe" -- king Kiki.

Au nasema uongo ndugu yangu?
🤣🤣
 
Itakuwa kujidanganya kama taifa kudhani kuwa tuko vizuri.

View attachment 1867150

Matumaini mapya yaliyoibuka baada ya SSH kuchukua nchi yamekwisha baada ya siku 100 ofisini.

Kama taifa tunayumba tokea kwenye corona hadi kwenye mustakabala kama taifa. Taifa limegawanyika hisia kali na munkari juu:

1. Kuhusiana na ugonjwa hatari wa Corona:

(a) Vinara wa misimamo ya awamu ile na Corona, chanjo yakiwamo mahusiano na WHO pia na mataifa mengine wangalipo serikalini.
(b) Kuna tofauti kubwa za kimtazamo kuhusiana na Corona baina ya watu, yakiwa ni madhara ya wazi yatokanayo na misimamo na propaganda za awamu ile.

View attachment 1867159

(c) Athari za ugonjwa zinaendelea kuongezeka na watu wasio na hatia wanaendelea kufa.

View attachment 1867123

(d) Tunapaswa sasa kama taifa kuzikumbatia tahadhari zote zilizokuwa zikibezwa katika awamu ile yakiwamo matumizi chanjo.

View attachment 1867133

Ni wazi kuwa tunahitaji marubani wapya kama kweli tunayo nia ya dhati ya kuyaokoa maisha ya watu.

2. Mustakabala wetu kisiasa kama taifa:

(a) Umoja wetu uliokuwapo katika siku 100 za mwanzo za SSH haupo tena.
(b) Ukiukwaji wa wazi wa sheria na katiba wenye upendeleo, yakiwemo matumizi ya dola dhidi ya makundi mengine umeligawa tena taifa.
(c) Kubambikiziwa kesi kwa Freeman Mbowe kumeongeza mgawanyo chuki zaidi dhidi ya serikali.

View attachment 1867140

Wasaidizi wasioweza kumsaidia rais kutuunganisha kama taifa, hawatufai.

3. Mustakabala wetu kiuchumi:

(a) Mwendelezo wa vigogo kutokulipa kodi, haukubaliki.
(b) Maongezeko ya kodi na tozo mbalimbali ndani ya kipindi cha ongezeko la UVIKO, hayakubaliki.
(c) Utaratibu wa gharama za matibabu ya UVIKO kuwa ni juu ya wahanga wa ugonjwa huu ambao ni janga la dunia, haukubaliki.




Manahodha wasioona umuhimu wa kila mtu kulipa kodi na kuwa ufumbuzi wenye wa haki kwenye majanga, hawatufai.

Mawaziri waliopo hawawezi kukwepa lawama kwa kushindwa kumsaidia rais kutuunganisha.

Kama wao hawauoni umuhimu wa kuachia ngazi ili kumpa Mama SSH nafasi ya mwanzo mpya wa kuisafisha hali hii, na wafurushwe tu kwa maslahi ya taifa.

Ninawasilisha.

Obvious ipo haja ya kufanya review ya baraza la mawaziri ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya Uchumi wa Dunia sambamba na kukabiliana na sakata la Uviko -19,ingawa isiwe kwa shinikizo bali itakavyoonekana inafaa.
 

Nakushukuru kwa kunielewa. Kimsingi sifurahishwi na kamata kamata yoyote kinyume cha sheria na hata kubambikiziana kesi.

Kwanini kudhulumu haki ya mtu?

Tofautisha presidential decree, katiba na matamko ya rais. Usichanganye mambo hapo. Rejea, ni presidential decree ipi ambayo labda wewe unayo kwenye mawazo inayokufanya kuweka angalizo lako?

It's so unfortunate kwamba Mbowe na wote waliokamatwa Mwanza walikamatwa kinyume cha sheria na kuishia kubambikiziwa kesi. Inasikitisha zaidi kuwa aliyefanya hivyo ni dola mwenye dhamana ya kutulinda.




Dalili za mvua ni mawingu. Siyo siri SSH siku 100 za mwanzo alikuwa kaenda vizuri hadi lilipokuja suala la katiba mpya.
Akaenda kulikoroga zaidi kwa dola iliyoyafanya Mwanza na yatokanayo yote kutokea hapo:


Wanaoona katiba mpya ni kipaumbele siyo magaidi.

Jumbe Brown nchi haipelekwi mbele na mtu mmoja.

Wewe unadhani:

1. Ni sawa kwa vinara wa kulikoroga la Corona awamu ya 5 kuendelea kuwa bado ni vinara wa kupambana na Corona leo?
2. Ni sawa shughuli za ndani za Chadema kuzimwa kwa nguvu za dola wakati za CCM, au mikusanyiko mingine yote katika mazingira yale yale ikiendelea?
3. Ni sawa kwa wahanga wa Corona kujigharimia wenyewe matibabu achilia mbali kuongezewa kodi na tozo mbalimbali ambazo vigogo hawa haziwahusu?

Unawaonaje manahodha wa majahazi hawa waliotakiwa kumsaidia SSH kutuvusha? Wewe huoni kuwaitisha kuachia ngazi ni katika kumpa nafasi SSH kama kadhamiria kutuvusha, atuvushe bila ya vikwazo vyao?
 
Obvious ipo haja ya kufanya review ya baraza la mawaziri ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya Uchumi wa Dunia sambamba na kukabiliana na sakata la Uviko -19,ingawa isiwe kwa shinikizo bali itakavyoonekana inafaa.

Halipo shinikizo lolote wala popote ila kilichopo ni uhalisia wa wazi tu:

1. Hivi kinara wa nyungu, michai chai, mikaratusi nk; porojoza za kuwa Corona ni vita vya kiuchumi, chanjo ni upigaji wa mabeberu, nk hatauficha uso wake kwenye kutuhamasisha leo kuchukua tahadhari ikiwamo hata kuvaa barakoa na hata kupata chanjo?!

IMG_20210614_192655_399.jpg


2. Vipi aliyevuruga kongamano la Chadema kinyume cha katiba akiiaacha mikutano ya wazi ya CCM, mikusanyiko ya watu kwenye mipira, matamasha nk, kuendelea bila vikwazo, ana weledi upi uliobakia kiasi cha kufumbia macho na kuendelea kujipa matumaini ya kuwa na kesho bora zaidi?!

3. Vipi anayetuongezea kodi na tozo katikati ya janga la Corona linalo tusuka suka vilivyo? Vipi huyu anayeendeleza vigogo kutohusika na kodi na tozo hizi? Vipi mwenye kututaka kujigharimia wenyewe kwa matibabu kwenye janga hili?

Unadhani kuwataka watu hawa kutupisha ni kuwashinikiza?

Tunapoogopa kutokea hadharani kuandamana, tushindwe hata kupaza sauti kwa hawa jamaa kuachia ngazi na huku tukitumia fake IDs?

Kudai haki kuna gharama. Nothing comes for free:


Ajabu ni kuwa tunataka mabadiliko tunaogopa kuandamana na hata kusema pia? Tunataka nani aseme? Ila matunda tunataka na ubingwa wa kukosoa yule kakosea hapa na yule kakosea kule tunao? Kwani mchango wetu sisi ni nini hasa? Au kusubiria teuzi kama kina Mashinji na kina Mdee na kina Pascal Mayalla 😂😂😂?!

Hiiiiii bagosha!
 
Halipo shinikizo lolote wala popote ila kilichopo ni uhalisia wa wazi tu:

1. Hivi kinara wa nyungu, michai chai, mikaratusi nk; porojoza za kuwa Corona ni vita vya kiuchumi, chanjo ni upigaji wa mabeberu, nk hatauficha uso wake kwenye kutuhamasisha leo kuchukua tahadhari ikiwamo hata kuvaa barakoa na hata kupata chanjo?!

View attachment 1867810

2. Vipi aliyevuruga kongamano la Chadema kinyume cha katiba akiiaacha mikutano ya wazi ya CCM, mikusanyiko ya watu kwenye mipira, matamasha nk, kuendelea bila vikwazo, ana weledi upi uliobakia kiasi cha kufumbia macho na kuendelea kujipa matumaini ya kuwa na kesho bora zaidi?!

3. Vipi anayetuongezea kodi na tozo katikati ya janga la Corona linalo tusuka suka vilivyo? Vipi huyu anayeendeleza vigogo kutohusika na kodi na tozo hizi? Vipi mwenye kututaka kujigharimia wenyewe kwa matibabu kwenye janga hili?

Unadhani kuwataka watu hawa kutupisha ni kuwashinikiza?

Tunapoogopa kutokea hadharani kuandamana, tushindwe hata kupaza sauti kwa hawa jamaa kuachia ngazi na huku tukitumia fake IDs?

Kudai haki kuna gharama. Nothing comes for free:


Ajabu ni kuwa tunataka mabadiliko tunaogopa kuandamana na hata kusema pia. Tunataka nani aseme? Ila matunda tunataka na ubingwa wa kukosoa yule kakosea hapa na yule kakosea kule tunao? Kwani mchango wetu sisi ni nini hasa? Au kusubiria teuzi kama kina Mashinji na kina Mdee na kina Pascal Mayalla 😂😂😂?!

Hiiiiii bagosha!
Hoja zako zisiwe kuzijibu kwa kuwa ziko nje ya swali la mleta Mada kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa.
Vyote ulivyouliza viko katika siasa.
 
...for a regime change through endless demonstrations eeee?!!!!🤣🤣

#KaziIendelee

Issue siyo regime change bali kuondoka viongozi mizigo wakiwamo mawaziri where applicable.

Au wewe wawaonaje waheshimiwa hawa afya, mambo ya ndani na fedha?

Mh. Kangi Lugora mwenyewe akiita mtu kuliwa kichwa hadi alipoliwa yeye.

Hiiiiii bagosha!

IMG_20210704_051559_619.jpg
 
Hoja zako zisiwe kuzijibu kwa kuwa ziko nje ya swali la mleta Mada kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa.
Vyote ulivyouliza viko katika siasa.

Umeandika kiyahudi?

Rejea kupasoma kujiridhisha kama unasomeka 😂😂😂!

Au ulikuwa waandika kwa uzi au mada tofauti na hii ya waheshimiwa mizigo mheshimiwa waziri mzigo 😂😂😂?
 
Uko sahihi mkuu tunahitaji fresh faces kwa kweli, new faces,new vision,harmony
 
Aanze na Siro na Mwigulu hao ndio wanaomvua nguo hadharani

Ninaunga mkono hoja.

Kama Mwigulu na Siro hawahusiki kwenye kadhia hizi (mada inavyojieleza). Wawili hawa wajiengue wenyewe. Vinginevyo hawa ni watendaji mizigo kwenye maeneo yao na ndiyo maana wanatuletea:

Miendelezo hii fyongo isiyokubalika:

1. Siro na Simbachawene:

IMG_20210726_013901_831.jpg


2. Mwigulu:

IMG_20210726_014752_451.jpg
 
Back
Top Bottom