#COVID19 Mawaziri waachie Ngazi kutoa Nafasi kwa Mwanzo Mpya

#COVID19 Mawaziri waachie Ngazi kutoa Nafasi kwa Mwanzo Mpya

Uko sahihi mkuu tunahitaji fresh faces kwa kweli, new faces,new vision,harmony

Haisaidii kuwafumbia macho watu hawa. Haisaidii kutokuwataja majina yao. Hawana mishipa ya aibu. Wanatuchukulia poa.

"Sitaona haya kumwonea haya mzembe" -- mwalimu Nyerere (rip).

Unajiuliza hivi Gwajima, Simbachawene, Sirro, Mwigulu na wenzao wanatuona je kweli?

Hatuna sababu ya kuona haya au kuogopa kuwataja kwa majina yao, kuwazodoa kwa unafiki wao, kuwazomea kwa njaa zao, kuwananga kwa ubinafsi wao uliopitiliza, kuwaonyesha kutokutufaa kwao nk.

Hii nchi ni yetu sote. Tunawajibika sote
kuona kuwa inaendeshwa kwa misingi ya haki, usawa na demokrasia kwa mujibu wa katiba. Si kwa utashi wa mtu binafsi.

Hili si shamba binafsi la mtu yeyote!
 
Kwani unataka uteuliwe wewe? Achia mwenye kuwateua anajua cha kufanya

ID yako hii ya msa(h)ada ninaisoma vyema.

IMG_20210726_020708_268.jpg


Hata hivyo nisiache kukupa makavu:

Nchi hii ni yetu sote wala si shamba binafsi la mtu.

"Sitaona haya kumwonea haya mzembe, mwizi, mbinafsi, asiyetufaa, mwongo, na wote namna hiyo" -- mwalimu Nyerere (rip).

IMG_20210707_084839_278.jpg


Hawa hapa hawatufai na sababu zimeorodheshwa. Vipi, eewe ni mmoja wao au japo kuna jamaa yako?

1. Afya:

IMG_20210726_021329_797.jpg


2. Mambo ya ndani:

IMG_20210726_013901_831.jpg


3. Fedha na uchumi:

IMG_20210726_014752_451.jpg


Au nasema uongo ndugu zangu?

Cc: BAK, Mwifwa imhotep
 
ID yako hii ya msa(h)ada ninaisoma vyema.

View attachment 1868344

Hata hivyo nisiache kukupa makavu:

Nchi hii ni yetu sote wala si shamba binafsi la mtu.

"Sitaona haya kumwonea haya mzembe, mwizi, mbinafsi, asiyetufaa, mwongo, na wote namna hiyo" -- mwalimu Nyerere (rip).

View attachment 1868345

Hawa hapa hawatufai na sababu zimeorodheshwa. Vipi, eewe ni mmoja wao au japo kuna jamaa yako?

1. Afya:

View attachment 1868341

2. Mambo ya ndani:

View attachment 1868342

3. Fedha na uchumi:

View attachment 1868343

Au nasema uongo ndugu zangu?

Cc: BAK, Mwifwa imhotep

Braza j una vituko vingi sana...
 
Itakuwa kujidanganya kama taifa kudhani kuwa tuko vizuri.

View attachment 1867150

Matumaini mapya yaliyoibuka baada ya SSH kuchukua nchi yamekwisha baada ya siku 100 ofisini.

Kama taifa tunayumba tokea kwenye corona hadi kwenye mustakabala kama taifa. Taifa limegawanyika hisia kali na munkari juu:

1. Kuhusiana na ugonjwa hatari wa Corona:

(a) Vinara wa misimamo ya awamu ile na Corona, chanjo yakiwamo mahusiano na WHO pia na mataifa mengine wangalipo serikalini.
(b) Kuna tofauti kubwa za kimtazamo kuhusiana na Corona baina ya watu, yakiwa ni madhara ya wazi yatokanayo na misimamo na propaganda za awamu ile.

View attachment 1867159

(c) Athari za ugonjwa zinaendelea kuongezeka na watu wasio na hatia wanaendelea kufa.

View attachment 1867123

(d) Tunapaswa sasa kama taifa kuzikumbatia tahadhari zote zilizokuwa zikibezwa katika awamu ile yakiwamo matumizi chanjo.

View attachment 1867133

Ni wazi kuwa tunahitaji marubani wapya kama kweli tunayo nia ya dhati ya kuyaokoa maisha ya watu.

2. Mustakabala wetu kisiasa kama taifa:

(a) Umoja wetu uliokuwapo katika siku 100 za mwanzo za SSH haupo tena.
(b) Ukiukwaji wa wazi wa sheria na katiba wenye upendeleo, yakiwemo matumizi ya dola dhidi ya makundi mengine umeligawa tena taifa.
(c) Kubambikiziwa kesi kwa Freeman Mbowe kumeongeza mgawanyo chuki zaidi dhidi ya serikali.

View attachment 1867140

Wasaidizi wasioweza kumsaidia rais kutuunganisha kama taifa, hawatufai.

3. Mustakabala wetu kiuchumi:

(a) Mwendelezo wa vigogo kutokulipa kodi, haukubaliki.
(b) Maongezeko ya kodi na tozo mbalimbali ndani ya kipindi cha ongezeko la UVIKO, hayakubaliki.
(c) Utaratibu wa gharama za matibabu ya UVIKO kuwa ni juu ya wahanga wa ugonjwa huu ambao ni janga la dunia, haukubaliki.




Manahodha wasioona umuhimu wa kila mtu kulipa kodi na kuwa ufumbuzi wenye wa haki kwenye majanga, hawatufai.

Mawaziri waliopo hawawezi kukwepa lawama kwa kushindwa kumsaidia rais kutuunganisha.

Kama wao hawauoni umuhimu wa kuachia ngazi ili kumpa Mama SSH nafasi ya mwanzo mpya wa kuisafisha hali hii, na wafurushwe tu kwa maslahi ya taifa.

Ninawasilisha.

Huku uko unazama huku tuko vizuri tutembee vifua mbere
 
Alikuwa na nafasi ya kufanya hivyo, akaichezea. Sasa hawa jamaa wanamwadhibu. Na wameshaongeza mizizi yao kwenye system. Kwa sasa kuwatoa ni vigumu mno.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app

Beberu anasema "it's never too late." Waswahili nao hakubakia nyuma, "wajinga ndiyo waliwao." Kigugumizi cha nini?


Kimya chake kinafanya watu kuhitimisha kuwa labda yeye ndiye mwenye makando kanda zaidi. Anapoteza uungwaji mkono.

Siamimi kuwa kipo asichokijua. Itakuwa ni kutojitendea haki yeye mwenyewe.

Cc: Mshana Jr
 

Mkuu kwenye bandiko lako namba moja sioni waziri yoyote wa kuachia ngazi, ifahamike hapa kwetu uwaziri ni njia kuupata utajiri. Mfano Jenister Mhagama anaachia vipi uwaziri hata kama hana tija, yeye anapigania kipapai tu aendelee kukaa kwenye ulaji.

Mwigulu ndio huyo kumuelekeza mama wa kambo kibla, saa hii anatengeneza sinema za kuusaka urais akijifanya ana suluhu ya matatizo ya watanzania. Nakumbuka Magufuli alimfukuza uwaziri kwa kumtuhumu anafanya kampeni za kujijenga kisiasa kuusaka urais. Alichokifanya Mwigulu ni kwenda kuloga akarudishwa tena kwenye uwaziri. Sasa hivi wameshamshikia mama wa kambo chini, wanafanya watakavyo. Mama ameambiwa atulie pesa ikusanywe kwenye tozo, na Mwigulu ameanza matumizi kwa kuzunguka huko na huko kuendelea na kampeni zake za Urais.
 
Mkuu kwenye bandiko lako namba moja sioni waziri yoyote wa kuachia ngazi, ifahamike hapa kwetu uwaziri ni njia kuupata utajiri. Mfano Jenister Mhagama anaachia vipi uwaziri hata kama hana tija, yeye anapigania kipapai tu aendelee kukaa kwenye ulaji.

Mwigulu ndio huyo kumuelekeza mama wa kambo kibla, saa hii anatengeneza sinema za kuusaka urais akijifanya ana suluhu ya matatizo ya watanzania. Nakumbuka Magufuli alimfukuza uwaziri kwa kumtuhumu anafanya kampeni za kujijenga kisiasa kuusaka urais. Alichokifanya Mwigulu ni kwenda kuloga akarudishwa tena kwenye uwaziri. Sasa hivi wameshamshikia mama wa kambo chini, wanafanya watakavyo. Mama ameambiwa atulie pesa ikusanywe kwenye tozo, na Mwigulu ameanza matumizi kwa kuzunguka huko na huko kuendelea na kampeni zake za Urais.

Mkuu ninakubaliana na yote uliyoyaandika. Ila sina hakika kwa sehemu ya mwisho kwenye mada kama uliiona:


IMG_20210726_035304_433.jpg


Suala la wao kutoka si kwa hiari yao peke yao. Bali hata kutoka kwa kufurushwa kama ikibidi, nayo ni sehemu ya mchezo vile vile.

Tunao wajibu uliotukuka wa kumsaidia SSH kuwaondosha watendaji kama hao. Yeye akiwa au hata asipokuwa sehemu ya uozo huo.


Nchi si kama shamba la mtu binafsi. Nchi huendeshwa kwa mujibu wa katiba. Isitoshe kuna yaliyo mikononi mwetu kama wananchi:

IMG_20210707_084839_278.jpg


Au nasema uongo ndugu yangu bwana Jumbe Brown?
 
Salaam mkuu Brazaj !!!

Mh.SSH ameapa kuilinda KATIBA....najua huridhishwi na kukamatwa kwa mh.Mbowe)

Mh.Rais SSH ana ile mikono yake yenye nguvu mno kikatiba "presidential decree"...hii imemilikishwa kwake na WATANZANIA katika kuyalinda maslahi yao kiafya ,kiuchumi na kijamii.....

Ukimuangalia vyema mh.Rais wetu unamaizi ile KIU YAKE KALI NA UCHUNGU WA KUTUBADILISHIA MENGI "yanayotuzonga"....

Ninatumai tukimpa muda atatupeleka mbele sana....

********************

Hapa sitaki kukukumbushia kuwa yule Prof.Cheeseman aliyehojiwa na CNN na kuuponda sana utawala wa awamu ya 6 kumbe "ALIOKOTEZA HABARI" kutoka kwa NON-AUTHORITATIVE SOURCE 🤣🤣

#KaziInaendelea
#NchiKwanza
#UtulivuNaAmaniKwanza
#TanzaniaIsASovereignState
Kwa huyu mama tayari kafail hana cha kubadili
 
Kwa huyu mama tayari kafail hana cha kubadili
Ila waswahili wanasema kawia ufike. It is never too late.

Mtu mzima akisema "samahani." Humaanisha fresh start. Hakuna cha kuongeza wala kupungua.
 
Tumsaidie Mama Samia kuisafisha nchi.


Hata kwa kupiga kelele tu.
Kuna watu hawataki hilo

wao wanataka maandamano na drama tu
 
Back
Top Bottom