Mawaziri Wakuu wote bomu, isipokuwa Kawawa na Sokoine!!

JokaKuu

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2006
Posts
34,188
Reaction score
62,952
..makala ya Mihangwa wa raia mwema akiwachambua Mawaziri Wakuu wa Tanzania kuanzia wakati wa Uhuru.

 
C.D. Msuya was among the best PM!!! no longo longo... actions only...
 
Ah wapi msuya alijenga kwao upareni akapeleka umeme, barabara mpaka milimani, mbona hakujenga barabara ya dodoma-tabora-singida-kigoma, ile ya tunduma-sumbawanga mbona hakujenga? huyu si yule aliyesema kila mtu abebe msalaba wake mwenyewe. dah mimi kwangu ni sokoine tu ndiye mwanaume hakukumbuka barabara ya arusha-monduli bali alijenga barabara ya makambako-songea na mengine lukuki aliyoyafanya
 
Kila mtu hodari sana wa kulaumu wenzake, ingekuwa nyinyi mungefanya vibaya zaidi ya hao.

MKUKI KWA NGURUWE LAKINI KWA BINAADAMU NI MCHUNGU!
 
hapa kuna ukweli hakuna aliye na unafuu wote wamekaa kifisadi tu
 

Chimunguru,

..mradi wa Songea--Makambako ulifadhiliwa na ODA. kuna mahali inasomeka kwamba mradi huo ulikuwa kati 1976--1984, sehemu nyingine inasomeka ulitekelezwa kati ya 1980--1985.

..kwa msingi huo, inawezekana mradi huo ulihusisha mawaziri wakuu watatu au hata wanne yaani Kawawa,Sokoine,Msuya,na Salim Ahmed Salim.

..kwenye nchi yenye umasikini kama Tanzania, ukianza kuchunguza na kuhoji kila mradi wa maendeleo nchi hii, basi utaishia kulaumu kila kiongozi kwa upendeleo au kuonea eneo fulani. kwa mfano ikiwa ni kweli mradi wa makambako--songea ulianza 1976, je ni halali kumtupia lawama Rashidi Kawawa ambaye anatokea Songea kwa upendeleo?
 
Nionavyo mimi kila moja ana udhaifu wake na mafanikio katika utendaji (kumbuka binadamu si malaika) lakini kipimo sahihi ni mwenye mafanikio mazuri kiutendaji usio wa kibaguzi kuliko mwingine. Kwa maoni yangu Sokoine ni wa kwanza na Kawawa anafuata kwa awamu zilizopendwa, Pinda anaonyesha dalili njema kwa awamu tuliyonayo kibindoni lakini bado yu kwenye mizani. Mawaziri wakuu waliobakia walipiga chenga sana, walitoa pasi mbovu na kubutua mpira nje badala ya kufunga magoli kuwezesha timu ishinde. Wengine walicheza rafu mbaya ambayo iliwapa kadi nyekundu kama Lowasa anavyo sugua benchi la kudumu.Mwisho nafikiri hata hawa makocha wanaoteua hawa wachezaji uwezo wao ni wakutilia mashaka.
 
kula tano..PInda sio mtu katudanganya na mali zake.
 
Malecela peke yake ndie aliyekuwa makini

Yap Ive said it sasa wasiopenda kanyweni sumu
 
Sumaye ndo alikuwa makini kupita wote. Hama hutaki nicheki kwenye PM
 
Msuya alikuwa safi lakina mbovu kuliko wote na anayefaa kunyongwa ni masai!
 
Msuya mjinga kweli.. Yani alienda kujenga na kuendeleza kule kwao kulivyo pakavu. Sehemu haina ata uchumi wakueleweka zaidi ya vumbi alafu akaforce development projects zifanyike hazijawasaidia wapare wenzake wala nini. Kule pako kama Helmand Province..lol
 
Kwangu mimi Sokoine was the really man. We lost him we lost the opportunity of using our heads to be creative.Waliomfuatia Sokoine wakaanza kujisifu mpaka hata kuruhusu uuzaji wa mitumba.Yaiyofuatia ndio hayo...hatuna hata kiwanda kimoja kinachozaisha kitu cha kueleweka mpaka tuwaite wawekezaji.
 
pm wa sasa ni mtu wa kauli mbiu tu kama bosi wake hapo juu, kila kukicha ni kubuni kauli mbiu tu! mara maisha bora sijui nini nini, mara kilimo sijui nini nini...! too much of slogans!
 
mnaweza vipi kumpima Waziri Mkuu ambaye siyo executive; haundi serikali na hawezi kumwajibisha waziri mwingine yeyote aliye chini yake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…