Mawaziri Wakuu wote bomu, isipokuwa Kawawa na Sokoine!!

Malecela peke yake ndie aliyekuwa makini

Yap Ive said it sasa wasiopenda kanyweni sumu

Huyo CHIGWIYEMISI aliyewaambia watu watunze pumba halafu zitawafaa wakati wa njaa ndo kabisaaa, ndo maana hata urais wenzio wameona hafai.
 
Huyu Pinda nadhani yeye anafuata upepo tu, kama BIG G anavutika pande zote. Anataka kumridhisha boss wake na WADANGANYIKA vile vile kwa wakati mmoja. Anaonekana ni muoga muoga, dhaifu flani hivi, ingawa EL ni fisadi wa kutupwa lkn jamaa lilikuwa sometimes linakemea kibabe, huyu Pinda dah ni propaganda kwa kwenda mbele. sijui kama tutafika kweli
 
Kawawa naye bomu tu..kawawa si ndo alifilisi mabenki kwa ajili ya miradi ya CCM
 
Nakuunga mkono ni bora ya EL kuliko huyu wa sasa.
 
Hii thread haimek sense if u would ask me. Umahiri wa uwaziri mkuu unaezaje kupimwa objectively?? Je tuna eza u-quantify? System ya utawala inaendana na misifa tunayoimwaga??etc etc

Tuanzie hapo.
 
..makala ya Mihangwa wa raia mwema akiwachambua Mawaziri Wakuu wa Tanzania kuanzia wakati wa Uhuru.
Mkuu, umesikia wapi biography ya mtu aliye hai! Kawawa na Sokoine wanasemwa sasa kwa sababu wameshatangulia na hawaji tena saa hivi. Hata Mtikila akiondoka utaona sifa atakazomwagiwa, achilia mbali Mr zero.
 
Julius Kambarage Nyerere ndiyo alikuwa waziri mkuu bora kuliko wote.....my opinion.
 
C.D. Msuya was among the best PM!!! no longo longo... actions only...
Aa wapi actions zenyewe ni kuelekeza miradi ya maendeleo kwenye jimbo lake hata wakajenga barabara za lami hadi upareni milimani? He was so selfish , what he cared for was the development of his constituency
 
moringe alikuwa bonge la pm yaani alikuwa sirias sana alikuwa mzee wa kaz
sio pinda analialia tu. hiimhhmhi inauma sana hawa maalbino hiiiihmhhhm!
waziri mkuu unalia tena bungeni!
nakumbuka sokoine alianzisha sungu sungu, wachawi na wezi walikiona cha mtema kuni
 

Mkuu, aliyeanzisha sungusungu national ni Augustine Lyatonga Mrema. Sokoine alianzisha Operation Linda Jiji iliyosimamiwa na JKT waakti huo OP Ulinzi. Nilikuwa mmoja wao siku hizo katika ulinzi. Makao makuu ya operation yalikuwa JKT Mgulani na sisi kambi yetu ilikuwa Kunduchi Mtongani pale wanapokaa mapolisi sasa hivi, tuliyabikiri sisi majengo yale. Weacha tu.
 
..hapa chini ni muendelezo wa makala ya Joseph Mihangwa.





 
..kuna masuala ya kihistoria ktk hizi makala na wachangiaji naona kama mnashindwa ku-take note of them.

..kuna suala la Mwalimu Nyerere kujiuzulu uwaziri mkuu. wakati miaka yote tunaambiwa alifanya hivyo ili kwenda kuimarisha chama, mwandishi anadai Mwalimu alijiuzulu baada ya kushindwa mjadala mkali uliohusu sera ya Africanization.
 
Mi Sokoine peke yake ndio namfagilia.Pinda kidogo,Lowasa hata kidogo sipo kwenye boti yake kabisa,hao wengine siwafahamu vizuri.
 
Chimunguru said:
Ah wapi msuya alijenga kwao upareni akapeleka umeme, barabara mpaka milimani, mbona hakujenga barabara ya dodoma-tabora-singida-kigoma, ile ya tunduma-sumbawanga mbona hakujenga?

Chimunguru,

..kumbe Cleopa Msuya alishayatolea majibu haya madai yako kwamba alihujumu maendeleo ya maeneo mengine ya Tanzania na kupeleka jimboni kwake Mwanga.

..soma kipande cha mahojiano yake na Absalom Kibanda.


MWANANCHI JUMAPILI: Kumekuwa na madai kwamba ukiwa kiongozi, uliamua kutumia ramani ya Mpango wa Maendeleo wa Makao Makuu Dodoma (CDA) kwa ajili ya maendeleo ya Wilaya ya Mwanga. Madai haya yana ukweli wowote?

MSUYA: Huo ni uongo kabisa kabisa, Huwezi kuchukua mpango wa Dodoma ambao maumbile yake ni tofauti nikaupeleka Mwanga ambako ni tofauti. Kuna watu walikuwa wanaeneza hayo mambo lakini ni uongo. Kitu ambacho nakiri kimefanyika ni kwamba, Wilaya ya Mwanga ilianzishwa na Serikali Julai 1979 kwa hiyo wizara ya Ardhi ya Mipango Miji iliombwa iende Mwanga kutengeza plan (mpango), wakaja wakatoa mapendekezo ya jinsi ya kuanza, mapendekezo yale yalikuwa mafinyu sana, tukashauri kwamba viongozi wa Wilaya ya Mwanga na viongozi wa Wizara ya Ardhi na Mipango Miji waende CDA kuona kwamba kweli itafaa na walipofika watalaam kule wakaona kuna marekebisho mengi ya kuyafanya na wakayafanya. Kwa hiyo kutumia utaalam na ushauri wao ndiyo, lakini, kusema tulichukua mipango miji ya Dodoma kupeleka Mwanga ni uongo.

MWANANCHI JUMAPILI: Kuna madai mengine kwamba ukiwa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais ulitumia muda wako mwingi kuangalia maendeleo ya jimbo lako la uchaguzi na wilaya yako ya Mwanga zaidi kuliko hata ilivyokuwa kwa maeneo mengine ya nchi, jambo ambalo baadhi ya watu wanaliona kuwa ni matumizi mabaya ya madaraka

MSUYA: Hilo nalo pia napenda niseme ni uongo. Yamezushwa mambo mengi, unajua kwenye hizi nafasi za uongozi kila mtu anaona ni jalala lake la anatupa uchafu. Nakumbuka kuna watu walikwenda wakaeleza kwamba, huyu mzee pamoja na mambo yote, ametia barabara zote za lami katika Wilaya ya Mwanga sasa safari moja niko nyumbani kule kwenye hizi sherehe za mbio za Mwenge, hawa vijana wa Mwenge wakashangaa mabarabara yetu mabovu kule milimani, wakauliza yale mabarabara ambayo tunaambiwa Msuya kajenga yako wapi, wakaambiwa hayo ni maneno tu yanazongumzwa huko Dar es Salaam.

Kitu ambacho nakubali nimefanya, na si aibu nashauri hata wenzangu wabunge. Nilikuwa mbunge wa kuchaguliwa pale tangu mwaka 1980 mpaka 2000 nilipostaafu. Katika mwanzo wake, miaka ya 1980 kama mnavyofahamu hali ya uchumi ilikuwa mbaya sana, kwa hiyo kama mbunge kazi yangu ya kwanza ilikuwa ni kwenda kueleza wananchi kwamba wasije wakatazamia kwa sababu wamenichagua mimi kama mbunge wasifikiri kwamba watapata vinono kutoka serikalini, kwa sababu hamna lakini kama wakitaka maendeleo ni lazima tuungane nao watu wajikusanye nguvu, wachange, na wanaoweza kufanya kazi kwa mikono wafanye.

Kwa kweli nilifanya kazi ya ku-mobilise opinion na wananchi kujishughulisha na kazi ndogondogo za maendeleo za kujenga zahanati, shule maji, barabara na kitu kimoja ambacho nilijivunia na nikashawishi wakakubali si sehemu moja katika kila pembe ya Wilaya tuwe tunashawishi chini ya kamati zao wawe na kitu cha kufanya na kazi za mbunge unakuwa unapita na unaona wanavyofanya na wakiwa wana matatizo unawasaidia, ukipata msaada unawapelekea, hivyo ndivyo tulivyofanya. Kwa uzoefu wenu kama vyombo vya habari ukichunguza wabunge waliopo pale bungeni wale wabunge ambao wako karibu sana na wapigakura wao na wanajishughulisha na hizi kazi ambazo wananchi wanafanya kuna vuguvugu la maendeleo. Ukikuta wale wabunge ambao wanakwenda siku moja, wakishachaguliwa hawarudi tena wanakaa mjini huku na kuuliza serikali itafanya nini hapa, utaona hakuna kitu kinachofanyika.

Mimi niliungana na wale wenzangu ambao walikuwa wanamotisha wilaya zao, wako wengi utaona kama kule wilaya ya Njombe, Mufindi, Lushoto mahali kama Ruvuma sehemu kama Songea, mobilization imekuwa ni kubwa sana na watu wamefanya mambo mengi, mobilisation kama ya kilimo na kadhalika.

Wale ambao wanajua historia, zamani Ruvuma haikuwa kitu lakini katika mobilisation ile Gama na nani wamemobilise watu sasa iko katika Big Four, wanazalisha mahindi, wanazalisha tumbaku, watu wamejenga nyumba nzuri. Kwa hiyo mobilisation inafanya kazi, wenzetu wa Rukwa wanafanya hivyo hivyo. Kwa hiyo hicho ndicho nilichofanya, kwa hiyo hii shutuma inayokuja kuwa ooho ametumia nguvu zake..., mimi tena kila wakati nilikuwa nikiomba hao wenye shutuma hizo waende wakakague ni vitu gani hivyo?
 
''Mwaka 1977 Kawawa aliondolewa uwaziri mkuu; tukio ambalo wengi waliliona kama matokeo ya ‘laana' kwake kutokana na jinsi alivyoendesha kwa matumizi ya nguvu, zoezi la kuhamisha watu kujiunga na Vijiji vya Ujamaa, na lile la "Operesheni Maduka", kwa kufunga maduka ya watu binafsi ili kutoa nafasi kwa maduka ya ushirika. Matukio hayo mawili yalimpunguzia kwa kiwango kikubwa sifa na umaarufu kwa wananchi wengi.
Kwa kushtushwa na kasi ya Kawawa ya "Operesheni Maduka", Nyerere alilaani akisema: "Kiongozi yeyote anayefunga maduka ya watu binafsi kwa nguvu na kusababisha usumbufu kwa watu wasipate mahitaji; ni adui wa Ujamaa. Maduka binafsi yatakufa kifo cha kawadia vitakapotokea vyama vya ushirika makini na vyenye nguvu, vitakavyosimamiwa vizuri".


Hebu nisaidieni bandugu, mbona hapo naona JKN alikosea? kwa nini wasingemalizana na mheshimiwa ofisini mpaka aseme hayo maneno kwa wananchi?
 
Waberoya,
JKN ilibidi aseme hayo hadharani kwa sababu he was politically responsible. hasira za wananchi zingeelekezwa kwake badala ya Kawawa.
 
Waberoya,
JKN ilibidi aseme hayo hadharani kwa sababu he was politically responsible. hasira za wananchi zingeelekezwa kwake badala ya Kawawa.

So kawawa alifanya bila consent ya mwalimu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…