mbongo_halisi
JF-Expert Member
- Apr 16, 2010
- 7,074
- 5,486
Kwa zitto kabwe kwa kweli ana uthubutu wa kipekee sana, yaani kwa kile alichokifanya mpaka sasa ni ushujaa wa hali ya juu kabisa nadhani wewe mwenyewe utakubaliana na mimi hakuna Mtu mwingine mwenye uwezo wa kuitisha press conference na kuongea vitu vya kuimiza serikali hii ya awamu ya tano.
Hivyo Zitto kamaliza kuplay part yake kilichopaswa kufuatia sasa baada ya sisi kujiridhisha kwamba kile alichokisema kina ukweli basi ilibidi tuandamane mpaka kwenye ofisi za wizara ya fedha kisha tumalizie na ikulu hili watupe majibu hizo hela zimeenda wapi.
Ingekuwa ndio china mpaka sasa hivi raisi angekuwa uhamishoni sema basi tu watanzania aliyeturoga alikuwa ni nguru wa dunia kiuchawi
Ubaya wa Zitto ni kwamba hajitambui bado, wenzake wanampotosha tu. Umesikia hotuba ya rais leo na uthibitisho wa CAG pamoja na katibu mkuu? Zitto atulizane tu kwa sasa, anapenda sana kupotosha watu kwa kuamini kuwa habari za uwongo anazopewa ni za kweli, matokeo yake ndiyo haya....haibu.