BelindaJacob
Platinum Member
- Nov 24, 2008
- 6,474
- 4,039
Wakuu habari za leo.
Ninaomba ushauri madhubuti kuhusu eneo nililonalo.
Ni heka 20 eneo la Kubaha Misufini. Zaidi ya kupimwa na kusafishwa mara kwa mara hamna kinachoendelea kwenye hilo eneo na sina mpango wa kujenga huko kwa muda huu.
Eneo hilo lina ardhi nzuri pia maji mengi sana. Sasa mimi nipo mbali nalo lakini nilipenda nifikirie kitu na kuweza kuliweka hilo eneo katika hali ya kutumika. Mtu wa kuniangalizia ninaweza kupata ambaye atasimamia shughuli nitakayodhamiria kuiendeleza kutokana na mawazo nitakayopata na kuyashambua.
Natanguliza shukrani kwa mawazo/ushauri wenu.
Hapo kwenye red ndio wapi? Au Kibaha? Kama ndio, vipi umeshawacheki watu wa ardhi ili ujue matumizi yake? Mimi ninalo la heka 25 Visiga. Nilipotaka kulipima, niliambiwa mtu mmoja hawezi kupimiwa eneo kubwa hivyo kwa sasa (labda heka tatu tatu). Kucheki matumizi, nikakuta ni industrial area/residential na wanalichikulia kama ni kibaha mjini.
Baada ya kuona hiyo nikaamua kupanda miembe (ili serikali ikilitaka kwa matumizi yake) nipate kitu cha kuthaminisha (ile inayoota kwa muda mfupi). Hata hivyo kwa sasa nataka nilisurvey na kuligawe viwanja vya makazi. Unaweza ukapitia nyao zangu kama ukiona inafaa
Mkuu ukishagawa kwa ajili ya makazi tuambie na sisi tuambulie kidogo!!
Wakuu habari za leo.
Ninaomba ushauri madhubuti kuhusu eneo nililonalo.
Ni heka 20 eneo la Kibaha Misufini. Zaidi ya kupimwa na kusafishwa mara kwa mara hamna kinachoendelea kwenye hilo eneo na sina mpango wa kujenga huko kwa muda huu.
Eneo hilo lina ardhi nzuri pia maji mengi sana. Sasa mimi nipo mbali nalo lakini nilipenda nifikirie kitu na kuweza kuliweka hilo eneo katika hali ya kutumika. Mtu wa kuniangalizia ninaweza kupata ambaye atasimamia shughuli nitakayodhamiria kuiendeleza kutokana na mawazo nitakayopata na kuyashambua.
Natanguliza shukrani kwa mawazo/ushauri wenu.
Kwa kuwa umesema eneo-------- lina rutuba nzuri--------maji ya kutosha-----na unaweza kumpata kijana wa kuliangalia------- i mean kufyeka nk--------- ushauri wangu--------
wapo wafugaji wengi wa ngombe dsm--- hawa wafugaji wa mjini-----hawana-----majani------
Ligawe hilo eneo katika vipande vya nusu ekari------tafuta aina tofautitofauti ya majani ya ngombe------yaoteshe kwa kila eneo----baada ya muda------utaanza kuvuna-----na kuuza majani-------ukiweza kufanya kwa umakini uatashangaa ------kila kukicha majani yanafuatwa huko huko shambani----
Uwekezaji wa namna hii hautakusumbua saana-----hauhitaji mtaji mkubwa-----na wala hautachukua muda wako kufuatilia
Kila La kheri
PS
Hapo kwenye red ndio wapi? Au Kibaha? Kama ndio, vipi umeshawacheki watu wa ardhi ili ujue matumizi yake? Mimi ninalo la heka 25 Visiga. Nilipotaka kulipima, niliambiwa mtu mmoja hawezi kupimiwa eneo kubwa hivyo kwa sasa (labda heka tatu tatu). Kucheki matumizi, nikakuta ni industrial area/residential na wanalichikulia kama ni kibaha mjini.
Baada ya kuona hiyo nikaamua kupanda miembe (ili serikali ikilitaka kwa matumizi yake) nipate kitu cha kuthaminisha (ile inayoota kwa muda mfupi). Hata hivyo kwa sasa nataka nilisurvey na kuligawe viwanja vya makazi. Unaweza ukapitia nyao zangu kama ukiona inafaa
niuzie hapo heka 10, then utaona nachofanya na wewe utacopy na kupest kutoka kwangu
Kwanza kabisa onana na maofisa ardhi wakupe mipango ya serikali vinginevyo unaweza kupoteza rasilimali uliyo nayo.
Ukiona wanakupa jibu la kutatanisha bora kata vipande vipande na kuza viwanja vya makazi, kisha pesa hiyo tafuta eneo linalofaa kwa kilimo
Hivi hawa serikali wanasurvey viwanja vya watu bila kuwapa info wakazi wa hapo maana yake nini? Belinda nakushauri panda mitiki tu hapo serikali hawatachukua kabisa na hata wakichukua watakupa mpunga mrefu sana hapo!!!!