Mawifi inakuwaje? Kunakuwa na kutokuelewana na mke wa kaka yao

Mawifi inakuwaje? Kunakuwa na kutokuelewana na mke wa kaka yao

Simtegemei chochote kila mtu na maisha yake. Changamoto ninayo pata ni mawifi dada wa mume wangu..hawa viumbe ni shida
🤣 tatizo ni wanawake, nikimaanisha na wewe kama una kaka na ameowa utaingia katika kundi au inakuwaje,nashindwa kuelewa nipo nipo tu
🙅‍♀️
 
Umeandika kwa kuegemea upande mmoja. Umesahau kuna waolewaji huwa wakorofi pia
Hapaaanah, Ni mtu na mkewe sasa madada inawahusu nini,mimi na mke wangu wao inakuwaje wanaleta ujumbe na wajumbe kutuhabarisha kama haitoshi wanamfuata mke wangu, ..toka kakuoa hata simu hapigi nyumbani .. halafu maneno yao yanaweza kumzalisha mwenye mimba.
 
Mama Mkwe na Mawifi wanaweza kuwa watu wazuri lakini mke wa Kaka akawa mbaya hivyo inategemea.
Inawezekana unapoint,Mke wa kaka anakuwa mbaya kivipi ? Hio kauli ndio inakuwa umeanza kulipuka unamjaza ubaya mke wa kaka ako.
 
Ukioa mwenye haiba na uwezo tofauti na dada zako, jipange tu kuweka mipaka, kuback up.
Mimi sina ugomvi najitahidi kumezea na wifi wangu waungwana na maneno yanaishia kwa kaka yao.
 
Ndo nasubiri show...na hivi hamna referee Ma mkwe kashafariki manake ndio alikuwa mtetezi wangu, huwezi kunisema vibaya akuelewe...Mwenzenu nilikuwa najua kujipendekeza Kwa ma mkwe...Yani hazipiti siku Tatu nimempigia, mara nimtumie vocha, mara posho ya mazingira magumu, mara fao la kunizalia mume...nikamtekaaaaa, mawifi wakakituliza...
Sasa game linaenda kuanza 1-1🤣🤣🤣 halafu mawifi wazaramo.
Hongera ulikua na mtetezi, kuna familia unakuta mama moto, mawifi moto hadi unajihisi ndio ushafika ahera sasa😂😂😂 kumbe bado upo duniani
 
Ndugu yangu tu mwenyewe atakunyoosha. Hujui tumeishi vipi toka awali. Magumu mangapi tumebebana leo hii eti hutaki ukaribu na ndugu wa mume. Umeolewa ama umeoa?

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
Waeleze wanadhani kutubwba kitandani ndio inatosha kufanya tuwasahau dada zetu...mbususu zipo nyingi tuu na ukikubali kuolewa kaa ukijua kua huo ni muunganiko wa familia mbili sio watu wawili
 
Dada wa wanaume wanasahau kuwa mwanaume akishaoa wao si kipaumbele tena, kipaumbele na jukumu lake ni kuhusu mkewe.

Wao inabaki kuwa msaada na msaada si lazima.

Nanyie huwa mnakuja kuhakikisha Mume na ndugu zake wanakaa mbali na ikiwezekana wasiwe karibu kama zamani!
 
Wanawake huwa tuna shida sana.... ukiachana na uanamke mawifi pia sisi ni shida nyingine....ukute sasa na mawifi hawana wanaume wa kuwakeep busy macho pua na masikio kwa kaka basi mnakua kama wake wenza.

hivo hivo tu tutafika, tukishindwa kufika tunakula kona.

Hahaha ni kweli wengine wakiingia nyumba fulani basi kama ndugu walikuwa na mawasiliano mazuri basi lazima waanze kugombana na wengine kuto kuongea kabisa!

Ngwajima alisema toka Doroth aolewe kwao basi ndugu yao(kaka) amegombana na kila mtu kwao na kufikia kugombana na hata baba yake mzazi na hawasemeshani na baba kufikia hatua ya kusema hamtambui mwanae..kisa na chanzo ni Doroth!
 
Back
Top Bottom