Mawifi punguzeni gubu

Namkunda OG

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2015
Posts
827
Reaction score
1,048
Habarini wakuu.......
Hawa mawifi wa dada yangu wanaona kama dada yangu anafaidi sana mali za kaka Yao

Nyuma ya pazia dada yangu alichukua mkopo wakakubaliana kama familia wafanye biashara na mme wake

Mungu akasaidia biashara zinaenda vzr wakapata mafanikio yakawaida tu sasa hawa ndugu wa mwanaume wanaona kama dada yangu na sisi ndugu zake tunafaidi sana kila siku wanatusengenya et kaka yao katusaidia maisha

Nyie mawifi kaeni kimya kwasababu hamjui nyuma yapazia kunanini
 
Ungewaambia waolewe na huyo kaka yao kama wanaona huyo dada yako/mdogo wako anafaidi.
 
Asante kwa ushauri nitamwambia shem afanye hvyo
 
Aisee...pia nikiwaangalia Dada zangu nasema mke wangu siku nikioa atapata tabu kidogo hahaaa ingawa wao wote wameolewa lakini wanamind sana vitu visivyowahusu...
Kuna siku walienda kwa mke wa mtoto wa mma madogo...wakamwambia jamaa hapohapo eti huyu mke mkubwa sana...na historia yake huifahamu...
 
Daaaah!hawa Dada zetu tusipo oa wana gubu ukioa gubu wanahamishia kwa wife,job true true
 
Kwakweli mdogo wangu akioa nitakua wifi bora sana.....haya mamtu yanaitwa mawifi ni taabu Jana tu nimetoka kuona wifi wa dada yangu alivyo mpuuzi

Sista kabatiza mwanawe akafanya sherehe ...mapishi yote masufuria zaidi ya matano kapika mwenyewe Sista wifi mtu kakaa kwenye kiti anapiga story anasubiri kiive....kwakweli nimeshangaa sana
 
Alafu wakwanza kupakua huyo wifi cjui wanashida gan
 
Alafu wakwanza kupakua huyo wifi cjui wanashida gan
Wanakera yaani kanitibua eti kisa mke wa mbunge basi weeeeeeeee kama vile ye ndo Janet magufuli ...mawifi jamani ni kerooo
 
Nipe mawasiliano yao ili nioe mmoja wao wanaweza wakapunguza mdomo
 
vipi dada na wewe utakuja kuwa wifi wa mtu? Ila sijui huwa tatizo ni nini hasa huo upande
 
Hii Vita ya mawifi wanaume haituhusu.
Huyo anayesema ananyanyaswa na wifi zake alikoolewa na yeye anawafanyia hivyo wake za kaka zake.
Ni mzunguko zaidi.
 
Yaani nnakuona ulivyo na hasira nao mkuu, sema ukitaka kula bata wapuuze, acha waongeee alaf kimyaaa wanaweza kunywa sumu hakuna jibu hatar kama kukaa kimya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…