Maxence Melo: JamiiForums imefanikiwa kujenga Fikra Mbadala kwa watanzania wengi

Chief Kabikula, sidhani kama tatizo ni kufutwa kwa nyuzi. Ninaweza kujenga hoja kwamba wale waliokuwa wakitoa nyunzi zenye mashiko wali-withdraw!

Sijasikiliza mahojiano hayo ya Bw Melo, lakini hata bila kusikiliza huyu ndugu ni mmojawapo ya mashujaa wa zama hizi! Hongera sana Bw Melo.

Kwa mfano, JF ndio jukwaa pekee au mojawapo ya majukwaa machache yaliyoendelea kutoa nafasi kwa wadau kuelezea fikira zao kwa kiasi fulani cha uhuru wakati wa enzi za "New Stone Age" (enzi za Shujaa wa Afrika).

Lakini hata kabla ya zama za "New Stone Age", wadau wengi waliokuwa wakibandika mada fikirishi au kuchangia mada fikirishi walikuwa wameishaanza kukaa pembeni na kubakia ku-peruzi tu. Mtakumbuka hata baadhi ya vigogo walijiunga kwa utambulisho wao halisi (mfano Mama Prof Tibaijuka, Mwigulu Mchemba, nk). Sababu kubwa iliyochangia wadau wenye fikira pevu kukaa pembeni na kuwa wasomaji tu, ni baada ya Lumumba kufungulia jeshi ya Lumumba Buku 7 Club! Hawa walivamia jukwaa kweli kweli kiasi cha kugeuza JF-Siasa kuwa jukwaa la matusi na utoto.

Kuna watu hata kama wanatumia IDs fake lakini conscience zao zinawazuia kuwa sehemu ya mijadala ya kitoto! Kwa maneno mengine ile hadhi ya JF kwa kiasi fulani ilishushwa na mkakati wa watawala kwa kufungulia jeshi lao kugeuza mijadala fikirishi kuwa mipasho ya uswahilini.

Kimkakati, watawala walifanikiwa sana.
 
Hongera umepigana mpaka kimeeleweka.
Keep it up comrade
 
Tumefanikiwa ku share experience on how ate Tunda ki masihara
 
Hongera sana Melo! Swali langu ni je, siku Melo hayupo,JamiiForums itaendelea kusimama?

Kwa maneno mengine,Melo umeandaa au unaandaa mbadala wako?

Nasema hivi kwasababu, ili legacy yako ya kuanzisha JamiiForums idumu, itakuwa ni pale tu ambapo JamiiForums itaendelea kuwepo na kusimama imara uwepo au usiwepo.
 
Aki
Akikujibu nitag
 
Miaka 10 ya mafanikio hongera sana Jf... labda kuna kitu gani kipya sasa tutarajie huko mbele..maono mapya..Pia swali kwa Jf je imefanikiwa kufikisha ujumbe kwa vijana mashuleni na vyuoni ili nao wawe wabunifu kama jamii forum?au huu ugunduzi wa max unaonekana kwa vijana nao wakaweza kufanya kitu sio lazima kifanane na jf hata kwenye fani zingine pia na hii yote ni katika kulikomboa taifa letu litoke kwenye umaskini huu hasa vijijini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…