Maxence Melo: Kukosa sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi ni hatari kwa usalama wa nchi

Maxence Melo: Kukosa sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi ni hatari kwa usalama wa nchi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Forums amesema ukusanyaji holela na kuzagaa kwa taarifa binafsi za watu mitaani ikiwemo makaratasi yanayotumika kama vifungashio vya chakula au madawa ni madhara ya kutokuwa na sheria inayolinda taarifa binafsi za watu jambo ambalo linaiweka pia nchi kwenye hali isiyo salama.

Amesema kuwa Jamii Forums ikishirikiana na wadau wengine imeandaa muswada wa mfano ambao imeupeleka serikalini ili kutoa mapendekezo yatakayosaidia kutungwa kwa sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi za wananchi.

Pamoja na mambo mengine, muswada huo unatoa muongozo wa taarifa gani zikusanywe, zitatumikaje, zikusanywe kwa kiasi gani, mwisho wa matumizi ya taarifa hizo ni upi na lini pamoja na uwepo wa chombo huru kitakacho simamia zoezi hilo.

Aidha ametolea mfano jumbe za "tuma kwa namba hii" na "waganga wa kienyeji" kuwa ni uthibitisho kuwa mifumo ya ulinzi wa taarifa za faragha za wananchi na watumiaji wa mitandao haiko salama.

"Katiba ya nchi ibara ya 16 inataka taarifa zako binafsi zilindwe katika hali yoyote, kwa mfano mnaenda mitaani mnaona mandazi yanafungwa kwenye makaratasi mbalimbali kama mitihani, na magazeti, taarifa zetu zinapatikana kirahisi sana."

"Tunaitaka mamlaka ya nchi kuzingatia takwa la kisheria la katiba ibara ya 16 na ibara ya 18 inayotaka mawasiliano ya mtu yasiingiliwe na mtu yoyote, na kwangu huo ndio uzalendo wa kweli."

"Katiba ya nchi inalinda taarifa za mtu, ingawa katiba yenyewe imeelekeza mamlaka husika kuweka utaratibu wa kisheria, lakini kuwa na sheria rasmi ya ulinzi wa taarifa binafsi hatuna na majirani zetu wote wanayo."

"Umoja wa Afrika ulielekeza nchi wanachama kwamba, lazima mataifa yetu yatengeneze chombo huru kwa ajili ya uchakataji wa taarifa binafsi za watu wake, na ukiangalia Kenya wana chombo kama hicho ambacho kinawasaidia." - Maxence Melo, Mkurugenzi Mtendaji, Jamii Forums.
 
Mkuu akumbuke hi ni nchi masikini bado watu wana pambana kupata milo mitatu kwa siku, leteni miswada inao leta unafuu wamaisha kwa watu, hiyo ya kutunza makaratasi itakuja badaye tukiingia middle class income.
Umeongea vyema.
Usiri wa taarifa za mtu ni muhimu, ila kwa sasa unafuu wa maisha kwa watanzania wa kada ya chini(ambao ndio wengi) ni muhimu zaidi.

Hoja ya kupambana na utitiri wa tozo ulioibuka katika kipindi hiki ambacho uchumi wa dunia umeyumba ni muhimu mno.

Wakati nchi nyingine zinajitahidi kuwanasua wananchi wake kwenye hii hali, serikali yetu inatuchezea mchezo wa karata tatu.

Inaweka ruzuku kwenye mafuta kisha inazitoa pamoja na faida kupitia mlango wa tozo.
 
Umeongea vyema.
Usiri wa taarifa za mtu ni muhimu, ila kwa sasa unafuu wa maisha kwa watanzania wa kada ya chini(ambao ndio wengi) ni muhimu zaidi...
Tatizo la elites class wetu, ni waoga sana na awajiamini kazi yao ni ku jipendekeza na kuahakikisha hawa kosoe serikali na viongozi wake.

Sasa hivi hali ya maisha ni ngumu kupita maelezo ila nani kutetea watu hao (wage earners)
 
Mkuu akumbuke hi ni nchi masikini bado watu wana pambana kupata milo mitatu kwa siku, leteni miswada inao leta unafuu wamaisha kwa watu, hiyo ya kutunza makaratasi itakuja badaye tukiingia middle class income.........
Ungekuwa umeitafakari mada ukaielewa vizuri hunge comment hivi.
 
Mkuu akumbuke hi ni nchi masikini bado watu wana pambana kupata milo mitatu kwa siku, leteni miswada inao leta unafuu wamaisha kwa watu, hiyo ya kutunza makaratasi itakuja badaye tukiingia middle class income.........
Kwani kuna shida gani the two going in parallel? If doing one thing at a time is your policy, then we will reach the middle class you are focusing a million yrs to come!
 
Kwani kuna shida gani the two going in parallel? If doing one thing at a time is your policy, then we will reach the middle class you are focusing a million yrs to come!
Priority au kipaumbele ni muhimu katika planning in development strategy plans, sioni kama kuna ubaya wowote tungeweka efforts zetu zote kwenye vitu basics, ili tupata quality nguvu kazi, itakao weza kutafakari na kujua umuhimu wa documetation nzur,ili tuingie middle class na jamii isio kua na njaa ya basics za kuishi
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Forums amesema Ukusanyaji Holela na kuzagaa kwa taarifa binafsi za watu mitaani ikiwemo Makaratasi yanayotumika kama vifungashio vya chakula au madawa ni madhara ya kutokuwa na Sheria inayolinda taarifa binafsi za watu jambo ambalo linaiweka pia nchi kwenye hali isiyo salama.
Bahati mbaya sana wasio na uwezo wa kuelewa umuhimu huo wametamalaki nchini na lazima tu watabeza kama si kupinga kabisa...masikini Tanzania😕
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Forums amesema Ukusanyaji Holela na kuzagaa kwa taarifa binafsi za watu mitaani ikiwemo Makaratasi yanayotumika kama vifungashio vya chakula au madawa ni madhara ya kutokuwa na Sheria inayolinda taarifa binafsi za watu jambo ambalo linaiweka pia nchi kwenye hali isiyo salama.

Amesema kuwa Jamii Forums ikishirikiana na Wadau wengine imeandaa Muswada wa mfano ambao imeupeleka Serikalini ili kutoa mapendekezo yatakayosaidia kutungwa kwa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi za wananchi.

Pamoja na mambo mengine, Muswada huo unatoa muongozo wa taarifa gani Zikusanywe, Zitatumikaje, Zikusanywe Kwa Kiasi Gani, Mwisho wa Matumizi ya Taarifa hizo ni upi na lini pamoja na uwepo wa Chombo Huru kitakacho simamia zoezi hilo.

Aidha ametolea mfano jumbe za "Tuma Kwa Namba Hii", au "Waganga wa Kienyeji" kuwa ni uthibitisho kuwa mifumo ya ulinzi wa taarifa za faragha za wananchi na watumiaji wa mitandao haiko salama.

"Katiba ya nchi ibara ya 16 inataka taarifa zako binafsi zilindwe katika hali yoyote, kwa mfano mnaenda mitaani mnaona mandazi yanafungwa kwenye makaratasi mbalimbali kama mitihani, na magazeti, taarifa zetu zinapatikana kirahisi sana"

"Tunaitaka mamlaka ya nchi kuzingatia takwa la kisheria la katiba ibara ya 16 na ibara ya 18 inayotaka mawasiliano ya mtu yasiingiliwe na mtu yoyote, na kwangu huo ndio uzalendo wa kweli"

"Katiba ya nchi inalinda taarifa za mtu, ingawa katiba yenyewe imeelekeza mamlaka husika kuweka utaratibu wa kisheria, lakini kuwa na sheria rasmi ya ulinzi wa taarifa binafsi hatuna na majirani zetu wote wanayo"

"Umoja wa Afrika ulielekeza nchi wanachama kwamba lazima mataifa yetu yatengeneze chombo huru kwa ajili ya uchakataji wa taarifa binafsi za watu wake, na ukiangalia Kenya wana chombo kama hicho ambacho kinawasaidia" - Maxence Melo, Mkurugenzi Mtendaji, Jamii Forums
Huyo Mello aache kuhangaika na kutapatapa App yenyewe imemshinda imekuwa ya kidwanzi itakuwa hayo mambo makubwa?.
 
Kulindwa ni muhimu sana, ila haki iende na wajibu, kuna wengi hawajui wajibu wao ila ni hodari kudai haki
 
Huyu apelekwe gereza zuri Ili apambane na Hali yake
 
Back
Top Bottom