Maxio Maximo asema Mwakalebela ndio anafaa kwa urais wa TFF

AUGUSTINO CHIWINGA

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2017
Posts
220
Reaction score
689
Aliyekua kocha mkuu wa Taifa Stars mbarazili Maxio Maximo amesema kwamba Frederick Mwakalebela ndio mgombea pekee anayefaa kuchaguliwa kuongoza TFF.

Maximo amesema kwamba MWAKALEBELA alifanya kazi kama Katibu mkuu enzi za Rais Leodgar Chilla Tenga na kila mtu aliona jinsi soka la Tanzania lilivyopiga hatua kipindi kile.

Maximo akaongeza kwamba Mwakalebela atatumia mbinu na mikakati ileile aliyoitumia wakati wa Tenga ili kuendeleza mpira wa miguu Tanzania.

Akamaliza kusema Mwakalebela ni mtu anayeamini katika soka la Vijana, soka la wanawake na uadilifu katika utawala.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wapiga kura wataona maoni yake na wao wana wagombea wao tusubiri

Sent from Ili iweje
 
Mkuu source ya habari yako please if u don't mind.
 
Maximo anajua Mwakalebela akipita atapata shavu la kuinoa stars kwa hiyo apo anatengeneza ugali wake japo tukimpima Mwakalebela kwa historia yake ya nyuma anamzidi Ally Mayai kwa CVs
 
Mkuu ni mada ya ngapi kwa leo tu umeanzisha kumpigia debe huyo kada wako?
 
Maximo anajua Mwakalebela akipita atapata shavu la kuinoa stars kwa hiyo apo anatengeneza ugali wake japo tukimpima Mwakalebela kwa historia yake ya nyuma anamzidi Ally Mayai kwa CVs
Kuna ubaya gani akirudi?
 
Mkuu Maximo ni vema ukatuambia na kiasi ulicholipwa kumpigia kampeni mtoa rushwa Mwakalebela ( ikumbukwe kwamba aliwahi kuondolewa kugombea ubunge ccm kwa sababu ya rushwa , akishirikiana na mkewe .
 
maelezo yako yanaonyesha upo ant-maximo
 
Ameshamwahidi nafasi ya ukocha Taifa Stars
 
Tatizo la mpira wetu...ni siasa...viongozi wengi.wanakua wanasiasa...sasa ni wakati wa wanamichezo kushika hatamu...ally mayai...namfahamu ni mwadilifu na ni mchapakazi...anamapenz na yanga africa...lakn..kwenye ukweli atasimamia namwamini....anaweza kutuvusha.....tumpe ajaribu maana ndio damu changa pale...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…