Mayele anatafuta mboga, viongozi Yanga jitahidini kutafuta mchele

NITAKUKAMATA TU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2021
Posts
347
Reaction score
432
Baada ya hapo jana mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga kutoka DRC, Fiston Kalala Mayele kuzawadiwa ng'ombe mwingine na mashabiki huko Mwanza, ni wazi sasa viongozi waanze kutafuta mchele, kwani Mayele anaendelea kutafuta mboga hili siku ya mwananchi day mashabiki wakale uwanjani, mpaka ligi kuisha ng'ombe watakuwa wametosha.
 
unawaza misosi ya kwenye matamasha. Watafutie wanao misosi ya nyumbani
 
Wasiwasi wangu ni jamaa kuwepo jangwani msimu ujao kama janja janja ya mikataba itaendelea kuwepo. Makolo sio watu wazuri.
 
Matusi ya nini tena sheikh, mpira burudani!
Burudani zenyewe ndio hizo ,unavutiwa na mayele unampa ng'ombe,mashabiki simba amjakatazwa kuwapa kina sakho ata ngamia kama mnaweza
 
Boko nae afunge tumpe mnyama kiboko
 
Burudani zenyewe ndio hizo ,unavutiwa na mayele unampa ng'ombe,mashabiki simba amjakatazwa kuwapa kina sakho ata ngamia kama mnaweza
Fedha taslimu ndio kila kitu, na zinapatikana CAF CL & CC. Sasa unampa Mayele ng'ombe halafu amsafirishe yeye mwenyewe, chenji atakayobaki nayo ni shilingi ngapi? πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 

Fedha taslimu ndio kila kitu, na zinapatikana CAF CL & CC. Sasa unampa Mayele ng'ombe halafu amsafirishe yeye mwenyewe, chenji atakayobaki nayo ni shilingi ngapi? πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Hapa ndio imeongea kiuanamichezo sio kuanza kuleta maswala yasiioeleweka
 
Bocco mpira umemshinda aje achunge hizo ng'ombe za Mayele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…