Maziko ya Abdulwahid Sykes 1968

Maziko ya Abdulwahid Sykes 1968

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MAZIKO YA ABDULWAHID SYKES 1968

Mazishi ya Abdulwahid Sykes yalifanyika siku ya Jumapili tarehe 13 Okrtoba, 1968.
Mazishi yake yalikuwa makubwa yasiyo kifani.

Ukitoa mazishi ya mwaka wa 1950 ya Sheikh Idrissa bin Saad, muasisi na Khalifa wa Tariqa Askariya na mazishi ya Sheikh Kaluta Amri Abeid mwaka 1963, Dar es Salaam ilikuwa haijapata kushuhudia mazishi kama hayo.

Gerezani yote ambako Abdulwahid aliishi katika utoto wake na mahali ambapo alianza harakati zake dhidi ya Waingereza, kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa kama vile imesimama hakuna kinachoendelea ila maziko ya Abdulwahid.

Hii ilikuwa pamoja na sehemu nyingine zilizozunguka Kariakoo kama Misheni Kota na Kisutu.

Gerezani kwa hakika ilikuwa na mwito wa pekee. Ilikuwa ni kutoka Gerezani ndipo walipotoka wanaharakati wa mwanzo waliounda TANU ukimtoa John Rupia.

Siku hiyo Gerezani ilikuwa imekuja kumzika shujaa wao.

Watu walianza kukusanyika nyumbani kwa mama yake, Abdulwahid Bibi Mruguru bint Mussa mapema asubuhi ambako maiti ilipokuwa imepelekwa.

Ilipofika adhuhuri ikawa kama vile Dar es Salaam nzima imekusanywa pale.

Chifu wa Unyanyembe Abdallah Said Fundikira, ambae Abdulwahid alisomanae darasa moja katika shule ya Kitchele mjini Dar es Salam katika miaka ya 1930 na mtu ambae walikwenda wote kuhiji Makka alikuja Dar es Salaam kwa ndege kutokea Nairobi kuja kuhudhuria mazishi.

Wakati ule Chief Fundikira alikuwa Mwenyekiti wa Shirila la Ndege la Afrika ya Mashariki.

Rais Nyerere alikuwa mmoja wa watu waliokwenda kuomboleza kifo cha Abdulwahid.

Watu wa itifaki walimuweka Nyerere jamvi moja na Ahmed Rashad Ali na walikula chakula sinia moja.

Akitembea kwa miguu Nyerere alilifuata jeneza la Abdulahid nyuma kutoka Mtaa wa Lindi, Gerezani hadi Msikiti wa Kitumbini maiti ilipokwenda kuswaliwa swala ya jeneza kama ilivyo ada ya Kiislam.

Pale Kitumbini, Nyerere alisimama nje ya msikiti pamoja na wananchi wengine kungojea maiti ilitolewe nje.

Mfanyabiashara mmoja wa Kiasia kuona Rais amesimama wima, kwa ajili ya heshima alileta kiti na kumuwekea Nyerere akae. Nyerere alikataa kukaa na akawa amesimama pamoja na watu wengine.

Kutoka Kitumbini msafara wa maziko ulielekea makaburi ya Kisutu kwa ajili ya mazishi.

Wakati huu wote wakielekea makaburini, Nyerere alikuwa nyuma ya jeneza kichwa chake amekiinamisha na kila wakati alionekana akifuta macho yake na kitambaa.

Nyerere alikuwa analia.

Ilikuwa mwaka 1952 Abdulwahid alipofahamiana na Nyerere na yeye Abdulwahid akamjulisha kwa watu mashuhuri wa Dar es Salaam - Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Suleiman Takadir, Mwinjuma Mwinyikambi, Mohamed Jumbe Tambaza, Omar Londo, Rajab Diwani, Mshume Kiyate, Bibi Tatu bint Mzee, Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bibi Asha Ngoma, Bibi Titi Mohamed, Bibi Hawa bint Maftah, Bibi Khadija bint Kamba, Said Chamwenyewe na wengi wengine.

Ilikuwa na kutokana na msaada wa Abdulwahid na wazalendo hawa ndiyo uliomuwezesha Nyerere kuwa katika siasa za Dar es Salaam, kuchukua uongozi wa TAA 1953 na mwaka wa 1954 TANU ikaundwa na Nyerere kuchukua uongozi wa nchi miaka tisa baadae.

Hakuna aliyeweza kukisia ni mawazo gani yalikuwa yanapita katika fikra za Nyerere.

Lakini ni wazi kuwa alikuwa akimfikiria Abdulwahid na jinsi pamoja walivyoweza kuanzisha harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Ilikuwa miaka15 iliyopita katika Ukumbi wa Arnatouglo, si mbali na pale alipokuwa, Nyerere aligombea urais wa TAA dhidi ya Abdulwahid.

Wote wawili wakiwa vijana wadogo.

Abdulwahid akiwa na umri wa miaka 30 na Nyerere akiwa na miaka 32.

 
Habari Mzee, unaweza kutupatia history kidogo ya Bibi Hadija Kamba? Mana nimeona mtaa wake ilala Bungoni pale.
 
Habari Mzee, unaweza kutupatia history kidogo ya Bibi Hadija Kamba? Mana nimeona mtaa wake ilala Bungoni pale.
1621851945526.png

Bi. Khadija bint Kamba

1621854158348.png


Kajembejr,
TANU ilifungua Idara yake ya Ujasusi kujikinga na maadui.
Bi. Khadija alikuwa mmoja wa hao.

TAAZIA: BI. KHADIJA BINT KAMBA (1922-2016) MWANAMAMA MPIGANIA UHURU - MAKALA HISANI YA SAIGON GROUP​

Mohamed Said Historia, Siasa na Maendeleo Tanzania December 01, 2016 0
Bi. Khadija Bint Kamba

Mtaa wa Bi. Khadija Bint Kamba, Ilala

Anaitwa Hadija Bint Kamba, Bint mrefu mweusi mwenye umbo lililosadifu Unyamwezi, asili yake ni Tabora ndipo alipotokea baba yake na Kigoma ndipo wazazi wa mama yake walipotokea.

Ni kama ilivyo kwa familia ya Sykes, Bint Kamba alitoka katika familia mashuhuri jijini Dar es Salaam katika miaka ya 1950s.

Aliingia katika harakati za ukombozi akiwa bint mdogo mwenye malengo tofauti kabisa na ya kipekee sana.

Pamoja na kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ukoloni tena akiuza roho kwani alikuwa ni bint pekee wa Kiafrika aliyeweza kujichanganya na Wazungu, hivyo aliweza kupata siri nyingi za wakoloni na kuwasaidia wapigania uhuru wasikamatwe na wakati mwingine wasidhurike.

Alifanya kazi hii kwa siri kubwa sana, kiasi kwamba hakuwa akijulikana sana kwa watu hasa wanaharakati. Alikuwa mtu mwenye uwezo wa kipekee wa kutunza siri.

Mwaka 1955 akiwa na Bibi Titi na Hawa Bint Maftah walishirikiana kuunda Baraza la Wanawake Tanganyika ikiwa ni kikundi ndani ya TANU kilichokuwa kikitoa ushawishi kwa akina mama kuiunga mkono TANU.

Mwaka 1961 wakati wa uhuru, Bint Kamba alikuwa ni mmoja wa timu iliyoundwa kubuni Nembo ya Taifa (maarufu kama nembo ya Ikulu ama nembo ya Adam na Hawa ambayo mpaka sasa imeendelea kuwa alama kuu ya taifa (baadhi ya waandishi wanamtaja kuwa yule mwanamke anayeonekana kwenye nembo hiyo ndiye Bint Kamba.

Novemba 2 ya Mwaka 1962 Mwalimu Nyerere alipotangaza kuunda Umoja wa Wanawake wa Tanganyika (UWT) Bint Kamba alikuwa ndio mpanga mikakati na mfumo wa uongozi wa UWT.

Pamoja na kushiriki katika mapambano ya kudai uhuru akiwa msiri mkubwa wa Mwalimu Nyerere, Bint Kamba hakuwahi kushika nafasi yeyote ya kisiasa kwa kugombea ama kuteuliwa.

Baada tu ya nchi kupata uhuru Bint Kamba alieleza kuwa lengo lake limetimia na kwamba haitaji cheo chochote.

Mwaka 1985 katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Mwalimu Nyerere akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) pamoja na Baraza la Wazee wa Dar es salaam juu ya kung'atuka alimtaja mtu mmoja ambaye ni wa kipekee aliyeyashangaza maisha yake ya uongozi.

Alimtaja Hadija Bint Kamba kuwa ni mwanamama na mpambanaji wa kipekee aliyeshiriki mapambano ya uhuru bila tamaa ya cheo.

Mwalimu Nyerere alisema kuwa amekaa Ikulu kwa miaka 25 na kila alipotaka kumteua, Hadija Bint Kamba aliendelea kubaki na msimamo wake kuwa hakupigania cheo bali alipigania haki na usawa...alitaka kuona Mwafrika anathaminiwa katika nchi yake na kwamba ametimiza lengo hilo.

Tangu Mwaka huo wa 1985, Mwalimu alimtangaza Bint Kamba kuwa ni, ''Shujaa Asiyevaa Nishani,'' na tangu wakati huo alishirikia vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na Mikutano Mikuu yote akiwa ni mwalikwa mpaka pale umri ulipokuwa mkubwa na kumfanya ashindwe kuhudhuria vikao na mikutano hiyo.

BI. Hadija Bint Kamba amefariki jana tarehe 30 Novemba, 2016 akiwa ni miongoni wa waasisi waliobahatika kuishi kwa muda mrefu katika nchi huru ya Tanzania.

Bint Kamba amezikwa mchana wa leo tarehe 1 Desemba 2016 katika makaburi ya Kisutu yaliyopo jijini Dar es Salaam.

Anakufa bila cheo lakini anazikwa kwa heshima ya kiongozi wa kitaifa, kwa msafara wa magari ya askari na viongozi wa CCM na Serikali kutoka mtaani kwake mtaa wenye jina lake Bint Kamba Street Ilala Bungoni mpaka Kisutu.

Maraisi wastaafu, Katibu Mkuu wa CCM, Naibu Katibu Mkuu na viongozi wengine wa CCM wakiongoza jeneza lenye mwili wake.

Anakufa bila utajiri lakini anazikwa kwa hadhi ya bilionea.
HIVI NDIVYO ULIVYO MWISHO WA WATU WEMA...!!!
***
Mara tu nilipopata taarifa ya msiba huu katika Saigon Group niliandika maneno haya yafuatayo:

''Bi. Khadija Kamba katika sifa yake kubwa katika TANU ni yeye kukubali kutoka TANU kwenda Congress kama "mole," yaani mpelelezi.

Hii ilimjengea uadui mkubwa na wenzake...bahati mbaya sana hizi ni katika historia zinazowatisha baadhi ya viongozi kwa hiyo historia ya mama yetu huyu haifahamiki vizuri wala haijaandikwa. Allah ampe kauli thabit.''
***

Nimepokea vilevile maneno kutoka kwa baadhi ya watu kuhusu msiba huu wa Bi. Khadija Bint Kamba:

''Uncle unatisha.
Muandike Binti Kamba.

Nadhani moja ya picha yake nzuri ni ile ya Ikulu na Nyerere wakati akiaga.
CCM ilimjengea upya nyumba yake Bungoni. Namkumbuka huyu bibi akiishi Aggrey.

Na wakati Kasanga Tumbo alipounda chama cha upinzani yeye na Issa Mtambo wakatangdaza kujiunga.
Wakati huo Mtambo akiishi mtaa wa Pemba kwa mkwewe Bi Mwajuma Mlenda, ndugu yake Bi Hawa Maftaha.

Mtambo alikaa kibarazani na kuichana kadi ya TANU.
Ilikuwa, ''shock,'' kwa wengi.

Kisha rafiki yake Roland Mwanjisi akaenda kumsihi, lakini wapi, akashikilia.
Kumbe yote yale yalikuwa machezo!

Inatisha!!!''
***

''Bi khadija Bint Kamba alizaliwa 1922 Tabora.

Mama yake ni Muhombo.
Kwao ni Ng'ambo Mbirani.

Baba yake ni Mzaramo wa Bagamoyo.
Allah hakumjalia watoto.

Lakini alikuwa ni mlezi mkubwa wa watoto wote wa nduguze.
Ukihitaji historia yake nitafute.

Mie ni Dada yangu upande wa umama.

Na malezi yake yote yalikuwa kwa mjomba wetu marehemu Khamis Mnubi pale Chemchem Mtaa wa Caravan siku hizi unaitwa Mtaa wa Uhuru.''
***
''Ni mama yangu bint Kamba hawa ndio kina mama wa mwanzo kabisa kujiunga na TANU akiwemo Bi. Baita wa Dodoma BI. Mtumwa wa Tabora, Bint Mrisho wa Tabora pia ni mama wa mwanzo katika TANU kwa ngoma yao ya Lelemama.''
***
[01/12, 10:57 p.m.] ‪+255 717 423 353: Tumekuelewa Shekh Said

[01/12, 11:00 p.m.] ‪+255 717 423 353: Shekh Said huyu Bi Hadija hukumuandika hata ww katika nakala zako sheikh ndio maana naona hata Tanzia kwa hisani ya Saigon.
***
[01/12, 11:41 p.m.] mohamedsaidsalum: Kuna tatizo sana kumtafiti "mole," yaani mpelelezi.

Bi. Khadija baada ya 1958 hakuwa mwana TANU ila ni ''kibaraka msaliti.''
Uongozi wa juu kabisa ndiyo wakijua kuwa alikuwa katika kazi maalum.

Sasa huyu anahitaji utafiti makhususi na CCM inawajibika kuweka wazi hili jalada la mama yetu huyu tujue yote aliyofanya.

Yuko, ''mole,'' mwingine iko siku nitamtaja huyu aliangamiza umma na mwenyewe alikereka sana mtu akimuuliza mchango wake katika historia ya Tanzania.
 
Asante kwa historia nzuri.
Swali langu lipo nje ya topic yako, ukipenda utalijibu. Nini chimbulo au chanzo cha jina Gerezani? Palikua na gereza mahali pale? Kama lilikuwepo ni sehemu gani hasa ya Dar es Salaam ya leo.
 
Asante kwa historia nzuri.
Swali langu lipo nje ya topic yako, ukipenda utalijibu. Nini chimbulo au chanzo cha jina Gerezani? Palikua na gereza mahali pale? Kama lilikuwepo ni sehemu gani hasa ya Dar es Salaam ya leo.
Kibu...
Sijui asili yake.
 
Alafu makonda alisema atatufukuza kwenye mkoa wake
 
Nina picha ya soko la Kariakoo ya 1950s na nyingine ya mtaani.

Naingia Maktaba.
Mzee Mohamed watu wanakupuuza sana sababu ya masuala yako ya udini. Yaani kwa kuwa TANU ilitokana na African Association ambayo chimbuko lake ni akina Sykes ambao ni waislamu basi unataka kuaminisha umma kuwa waislamu wao pekee ndio walikuwa chachu ya kupigania uhuru. That is a big mistake.
 
Mzee Mohamed watu wanakupuuza sana sababu ya masuala yako ya udini. Yaani kwa kuwa TANU ilitokana na African Association ambayo chimbuko lake ni akina Sykes ambao ni waislamu basi unataka kuaminisha umma kuwa waislamu wao pekee ndio walikuwa chachu ya kupigania uhuru. That is a big mistake.
Idugunde,
Namshukuru Allah kwa kuniweka mbali na upuuzi hivyo kukosa kupuuzwa.

Wachapa vitabu, magazeti, radio na TV stesheni wanakuja hadi nyumbani kwangu kunihoji wewe unasema napuuzwa tena sana.

Hili juma la tatu niko Clouds Plus na Masudi Kipanya ananihoji kuhusu Abdul Sykes DSTv Channel 294.

1621959167651.png
 
Idugunde,
Namshukuru Allah kwa kuniweka mbali na upuuzi hivyo kukosa kupuuzwa.

Wachapa vitabu, magazeti, radio na TV stesheni wanakuja hadi nyumbani kwangu kunihoji wewe unasema napuuzwa tena sana.

Hili juma la tatu niko Clouds Plus na Masudi Kipanya ananihoji kuhusu Abdul Sykes DSTv Channel 294.
Ok fine mzee Mohamed utahojiwa na Clouds Tv na Abdul Sykes ni mmoja wa waasisi wa African Association alikuwa muislamu. Je hii ni justification kuwa waislamu pekee ndio walipigania uhuru wa Tanzania?

Utumwe mwandishi makini hapa Tanzania utamtaja Massoud Kipanya?
 
Back
Top Bottom