Mazingira ya Mashine za maji ya kunywa ya bure kwa Wananchi Dar es Salaam haziko salama, Wizara ya Afya fatilieni kinachoendelea

Mazingira ya Mashine za maji ya kunywa ya bure kwa Wananchi Dar es Salaam haziko salama, Wizara ya Afya fatilieni kinachoendelea

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
photo_2024-07-09_09-31-02 (4).jpg
Katika pitapita zangu kwenye maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, zaidi ya miezi mitano kuna jambo nimekuwa nikilichunguza ikiwa ni baada ya kukumbana nalo kwa mara kwa mara kwenye nyakati na maeneo tofauti.

Ukipita baadhi ya maeneo yaliyopo pembezoni mwa barabara kwenye Jiji la Dar es Salaam kuna vituo maalumu ambavyo jamii au Mtu anaweza kupita na kupata huduma ya maji ya kunywa bure bila gharama yoyote.

Nimeuliza baadhi ya watu nimeambiwa mashine zilizo nyingi zimefungwa na wadau kwa kujitolea, mfano eneo la Ofisi za Zimamoto karibia na mataa ya Fire, Kariakoo Bigbon, Kinondoni Biafra, Kawe-Malingo eneo la Msikiti.
photo_2024-07-09_09-31-03 (2).jpg

photo_2024-07-09_09-31-03.jpg
Huduma hizo zimekuwa na msaada kwa Wananchi hususani kwa watembea kwa miguu hasa wenye kipato duni, mfano baadhi ya waokota taka za plastiki, machinga watembeza bidhaa ikiwemo ukwaju, nguo na viatu, Watoto wa shule za Serikali hasa shule za msingi, watu wenye ulemavu ambao upendelea kukaa maeneo ya kando na barabara pamoja na wengine.

Hata hivyo licha ya tija hizo lakini watumiaji katika maeneo mengi ambayo nimefanikiwa kufika na kufuatilia wapo katika hatari zaidi ya kupata magonjwa ya kuambukiza pamoja na magonjwa ya mlipuko, na uenda wengine wameshakumbana nayo kwa kujua chanzo au kutokujua.

Ni katika hali ya kuuzunisha maeneo mengi ambapo kuna huduma hizo, unakuta vikombe vinavyotumika ni vitatu au viwili tokea asubuhi mpaka jioni bila kuoshwa, yaani Mtu anafika eneo husika yalipo mabomba yanayotoa maji anachukua kikombe ambacho hakijasafishwa vizuri palepale anakunywa maji na kuondoka.
photo_2024-07-09_09-31-02 (2).jpg
Akija mwingine na mwingine anafanya hivyo hivyo (katika baadhi ya maeneo, mfano Kinondoni Biafra, kikombe kimoja kwa siku kinaweza kutumiwa na Watu 50 hadi 70 bila kusafishwa).

Pia katika mazingira hayo unakuta Mtu anafika eneo hilo, mfano wanaookota taka za plastiki anashika kikombe na kunywa maji bila kunawa mikono, vilevile wakija na wengine na chombo kilekile nao wanaitumia kwa mtindo huohuo.

Kuna maeneo mengine vyombo hizo zimefungiwa na kamba kabisa, ikiwa ni kuhofiwa kuibiwa, kutokana na hali hiyo nimeshuhudia mara kwa mara Mtu anaishika ‘glasi’ ikiwa kwenye kamba anakunywa maji na kuondoka, bila kuoshwa wala kusafishwa vizuri na mwingine akija anatembea kwenye mtindo huohuo.

Uenda waliojitolea au kuratibu huduma hizo walikuwa na dhamira njema, lakini kwa mtindo huo, afya za Wananchi wengi zipo hatarini ikiwemo Watoto, Wanafunzi ambao wemekuwa wakifika maeneo hayo na kupata huduma.

Wito wangu katika hilo, ni vyema mamlaka kushirikiana na wadau kuja na ubunifu wa kuboresha utoaji wa huduma za aina hiyo ili kuwezesha jamii kujikinga na magonjwa ya kuambukiza pamoja na magonjwa ya milipuko.

Licha hilo ni muhimu mamlaka husika hasa Wizara ya Afya kuchukua hatua za haraka ikiwemo kukagua maeneo hayo, sambamba na kusitisha vituo hivyo kuendelea kutoa huduma kwa sasa mpaka vitakapoboreshwa, maana inavyoonekana athari zake uenda zikawa kubwa zaidi ya faida inayoweza kuwa ipatikana kwa sasa.
 
Katika pitapita zangu kwenye maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, zaidi ya miezi mitano kuna jambo nimekuwa nikilichunguza ikiwa ni baada ya kukumbana nalo kwa mara kwa mara kwenye nyakati na maeneo tofauti.

Ukipita baadhi ya maeneo yaliyopo pembezoni mwa barabara kwenye Jiji la Dar es Salaam kuna vituo maalumu ambavyo jamii au Mtu anaweza kupita na kupata huduma ya maji ya kunywa bure bila gharama yoyote.

Nimeuliza baadhi ya watu nimeambiwa mashine zilizo nyingi zimefungwa na wadau kwa kujitolea, mfano eneo la Ofisi za Zimamoto karibia na mataa ya Fire, Kariakoo Bigbon, Kinondoni Biafra, Kawe-Malingo eneo la Msikiti.
Huduma hizo zimekuwa na msaada kwa Wananchi hususani kwa watembea kwa miguu hasa wenye kipato duni, mfano baadhi ya waokota taka za plastiki, machinga watembeza bidhaa ikiwemo ukwaju, nguo na viatu, Watoto wa shule za Serikali hasa shule za msingi, watu wenye ulemavu ambao upendelea kukaa maeneo ya kando na barabara pamoja na wengine.

Hata hivyo licha ya tija hizo lakini watumiaji katika maeneo mengi ambayo nimefanikiwa kufika na kufuatilia wapo katika hatari zaidi ya kupata magonjwa ya kuambukiza pamoja na magonjwa ya mlipuko, na uenda wengine wameshakumbana nayo kwa kujua chanzo au kutokujua.

Ni katika hali ya kuuzunisha maeneo mengi ambapo kuna huduma hizo, unakuta vikombe vinavyotumika ni vitatu au viwili tokea asubuhi mpaka jioni bila kuoshwa, yaani Mtu anafika eneo husika yalipo mabomba yanayotoa maji anachukua kikombe ambacho hakijasafishwa vizuri palepale anakunywa maji na kuondoka.
Akija mwingine na mwingine anafanya hivyo hivyo (katika baadhi ya maeneo, mfano Kinondoni Biafra, kikombe kimoja kwa siku kinaweza kutumiwa na Watu 50 hadi 70 bila kusafishwa).

Pia katika mazingira hayo unakuta Mtu anafika eneo hilo, mfano wanaookota taka za plastiki anashika kikombe na kunywa maji bila kunawa mikono, vilevile wakija na wengine na chombo kilekile nao wanaitumia kwa mtindo huohuo.

Kuna maeneo mengine vyombo hizo zimefungiwa na kamba kabisa, ikiwa ni kuhofiwa kuibiwa, kutokana na hali hiyo nimeshuhudia mara kwa mara Mtu anaishika ‘glasi’ ikiwa kwenye kamba anakunywa maji na kuondoka, bila kuoshwa wala kusafishwa vizuri na mwingine akija anatembea kwenye mtindo huohuo.

Uenda waliojitolea au kuratibu huduma hizo walikuwa na dhamira njema, lakini kwa mtindo huo, afya za Wananchi wengi zipo hatarini ikiwemo Watoto, Wanafunzi ambao wemekuwa wakifika maeneo hayo na kupata huduma.

Wito wangu katika hilo, ni vyema mamlaka kushirikiana na wadau kuja na ubunifu wa kuboresha utoaji wa huduma za aina hiyo ili kuwezesha jamii kujikinga na magonjwa ya kuambukiza pamoja na magonjwa ya milipuko.

Licha hilo ni muhimu mamlaka husika hasa Wizara ya Afya kuchukua hatua za haraka ikiwemo kukagua maeneo hayo, sambamba na kusitisha vituo hivyo kuendelea kutoa huduma kwa sasa mpaka vitakapoboreshwa, maana inavyoonekana athari zake uenda zikawa kubwa zaidi ya faida inayoweza kuwa ipatikana kwa sasa.
Mwenzako amejitolea mashine na maji.
Wewe punguza maneno weka vikombe Disposable tatizo liishe acha kulalamika.
 
Weka disaposable..sio kila mtu ana pesa ya maji ya 500
 
Katika pitapita zangu kwenye maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, zaidi ya miezi mitano kuna jambo nimekuwa nikilichunguza ikiwa ni baada ya kukumbana nalo kwa mara kwa mara kwenye nyakati na maeneo tofauti.

Ukipita baadhi ya maeneo yaliyopo pembezoni mwa barabara kwenye Jiji la Dar es Salaam kuna vituo maalumu ambavyo jamii au Mtu anaweza kupita na kupata huduma ya maji ya kunywa bure bila gharama yoyote.

Nimeuliza baadhi ya watu nimeambiwa mashine zilizo nyingi zimefungwa na wadau kwa kujitolea, mfano eneo la Ofisi za Zimamoto karibia na mataa ya Fire, Kariakoo Bigbon, Kinondoni Biafra, Kawe-Malingo eneo la Msikiti.
Huduma hizo zimekuwa na msaada kwa Wananchi hususani kwa watembea kwa miguu hasa wenye kipato duni, mfano baadhi ya waokota taka za plastiki, machinga watembeza bidhaa ikiwemo ukwaju, nguo na viatu, Watoto wa shule za Serikali hasa shule za msingi, watu wenye ulemavu ambao upendelea kukaa maeneo ya kando na barabara pamoja na wengine.

Hata hivyo licha ya tija hizo lakini watumiaji katika maeneo mengi ambayo nimefanikiwa kufika na kufuatilia wapo katika hatari zaidi ya kupata magonjwa ya kuambukiza pamoja na magonjwa ya mlipuko, na uenda wengine wameshakumbana nayo kwa kujua chanzo au kutokujua.

Ni katika hali ya kuuzunisha maeneo mengi ambapo kuna huduma hizo, unakuta vikombe vinavyotumika ni vitatu au viwili tokea asubuhi mpaka jioni bila kuoshwa, yaani Mtu anafika eneo husika yalipo mabomba yanayotoa maji anachukua kikombe ambacho hakijasafishwa vizuri palepale anakunywa maji na kuondoka.
Akija mwingine na mwingine anafanya hivyo hivyo (katika baadhi ya maeneo, mfano Kinondoni Biafra, kikombe kimoja kwa siku kinaweza kutumiwa na Watu 50 hadi 70 bila kusafishwa).

Pia katika mazingira hayo unakuta Mtu anafika eneo hilo, mfano wanaookota taka za plastiki anashika kikombe na kunywa maji bila kunawa mikono, vilevile wakija na wengine na chombo kilekile nao wanaitumia kwa mtindo huohuo.

Kuna maeneo mengine vyombo hizo zimefungiwa na kamba kabisa, ikiwa ni kuhofiwa kuibiwa, kutokana na hali hiyo nimeshuhudia mara kwa mara Mtu anaishika ‘glasi’ ikiwa kwenye kamba anakunywa maji na kuondoka, bila kuoshwa wala kusafishwa vizuri na mwingine akija anatembea kwenye mtindo huohuo.

Uenda waliojitolea au kuratibu huduma hizo walikuwa na dhamira njema, lakini kwa mtindo huo, afya za Wananchi wengi zipo hatarini ikiwemo Watoto, Wanafunzi ambao wemekuwa wakifika maeneo hayo na kupata huduma.

Wito wangu katika hilo, ni vyema mamlaka kushirikiana na wadau kuja na ubunifu wa kuboresha utoaji wa huduma za aina hiyo ili kuwezesha jamii kujikinga na magonjwa ya kuambukiza pamoja na magonjwa ya milipuko.

Licha hilo ni muhimu mamlaka husika hasa Wizara ya Afya kuchukua hatua za haraka ikiwemo kukagua maeneo hayo, sambamba na kusitisha vituo hivyo kuendelea kutoa huduma kwa sasa mpaka vitakapoboreshwa, maana inavyoonekana athari zake uenda zikawa kubwa zaidi ya faida inayoweza kuwa ipatikana kwa sasa.

Maji yameshawekwa, chombo cha kunywea ni suala la mteja mwenyewe kujiongeza
Lakini pia; ni bora kunywa maji hayo kuliko kunywa kwenye mfereji... au yale yanayofungwa kwa nailoni hata hujui yametoka wapi
Ulimwengu wa tatu maisha ni magumu sana.......
 
Unajuwa Kuna watu wao ni kutowa makosa kufanya hawajuwi ndio Bongo akili nyingi
 
Osha kikombe kabla ya kunywa maji hapo.
Tatizo waswahili mnapenda kufanyiwa kila kitu.
Acheni UPUMBAVU
 
Katika pitapita zangu kwenye maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, zaidi ya miezi mitano kuna jambo nimekuwa nikilichunguza ikiwa ni baada ya kukumbana nalo kwa mara kwa mara kwenye nyakati na maeneo tofauti.

Ukipita baadhi ya maeneo yaliyopo pembezoni mwa barabara kwenye Jiji la Dar es Salaam kuna vituo maalumu ambavyo jamii au Mtu anaweza kupita na kupata huduma ya maji ya kunywa bure bila gharama yoyote.

Nimeuliza baadhi ya watu nimeambiwa mashine zilizo nyingi zimefungwa na wadau kwa kujitolea, mfano eneo la Ofisi za Zimamoto karibia na mataa ya Fire, Kariakoo Bigbon, Kinondoni Biafra, Kawe-Malingo eneo la Msikiti.
Huduma hizo zimekuwa na msaada kwa Wananchi hususani kwa watembea kwa miguu hasa wenye kipato duni, mfano baadhi ya waokota taka za plastiki, machinga watembeza bidhaa ikiwemo ukwaju, nguo na viatu, Watoto wa shule za Serikali hasa shule za msingi, watu wenye ulemavu ambao upendelea kukaa maeneo ya kando na barabara pamoja na wengine.

Hata hivyo licha ya tija hizo lakini watumiaji katika maeneo mengi ambayo nimefanikiwa kufika na kufuatilia wapo katika hatari zaidi ya kupata magonjwa ya kuambukiza pamoja na magonjwa ya mlipuko, na uenda wengine wameshakumbana nayo kwa kujua chanzo au kutokujua.

Ni katika hali ya kuuzunisha maeneo mengi ambapo kuna huduma hizo, unakuta vikombe vinavyotumika ni vitatu au viwili tokea asubuhi mpaka jioni bila kuoshwa, yaani Mtu anafika eneo husika yalipo mabomba yanayotoa maji anachukua kikombe ambacho hakijasafishwa vizuri palepale anakunywa maji na kuondoka.
Akija mwingine na mwingine anafanya hivyo hivyo (katika baadhi ya maeneo, mfano Kinondoni Biafra, kikombe kimoja kwa siku kinaweza kutumiwa na Watu 50 hadi 70 bila kusafishwa).

Pia katika mazingira hayo unakuta Mtu anafika eneo hilo, mfano wanaookota taka za plastiki anashika kikombe na kunywa maji bila kunawa mikono, vilevile wakija na wengine na chombo kilekile nao wanaitumia kwa mtindo huohuo.

Kuna maeneo mengine vyombo hizo zimefungiwa na kamba kabisa, ikiwa ni kuhofiwa kuibiwa, kutokana na hali hiyo nimeshuhudia mara kwa mara Mtu anaishika ‘glasi’ ikiwa kwenye kamba anakunywa maji na kuondoka, bila kuoshwa wala kusafishwa vizuri na mwingine akija anatembea kwenye mtindo huohuo.

Uenda waliojitolea au kuratibu huduma hizo walikuwa na dhamira njema, lakini kwa mtindo huo, afya za Wananchi wengi zipo hatarini ikiwemo Watoto, Wanafunzi ambao wemekuwa wakifika maeneo hayo na kupata huduma.

Wito wangu katika hilo, ni vyema mamlaka kushirikiana na wadau kuja na ubunifu wa kuboresha utoaji wa huduma za aina hiyo ili kuwezesha jamii kujikinga na magonjwa ya kuambukiza pamoja na magonjwa ya milipuko.

Licha hilo ni muhimu mamlaka husika hasa Wizara ya Afya kuchukua hatua za haraka ikiwemo kukagua maeneo hayo, sambamba na kusitisha vituo hivyo kuendelea kutoa huduma kwa sasa mpaka vitakapoboreshwa, maana inavyoonekana athari zake uenda zikawa kubwa zaidi ya faida inayoweza kuwa ipatikana kwa sasa.
Maji upewe bure na kikombe uoshewe?? Ewe pimbi umasikini sio sifa!!!
Cc : Mahondaw ephen_ FaizaFoxy
 
Back
Top Bottom