Mazishi ya Kanumba, kamati yapiga hela ndefu

Mbali na misiba hata kwenye harusi muhimu waweka hazina wawe ndugu aliyependekezwa na wanandugu. Nakumbuka yaliyonitokea kwenye kamati ya harusi ya kaka baada ya kubaki salio la 1000000/= mwenyekiti na katibu wakataka 400000 nikawamgomea then baada ya harusi wakataka kutumia hizo hela kuvunja kamati nikagoma. Baada ya fungate nikamkabidhi kaka akazitumia kununulia mabati na kumalizia nyumba yake ijapokuwa walinichukia lkn baadae walieleweshwa
 

ulichosema ni kweli kabisa
 
Waliokula hela za msiba watapata matatizo makubwa sana,mi yangu macho mi kinachonishangaza walishatangaza kuwa mtu asiye mwanachama wao hawataenda ilikuaje tena kuwa mpaka kwn kamati? wewe JB na wenzako mmeshalaanika mtabakia kununua vigari vitagongwa mtabaki km mlivyo. maneno ya watu ni mabaya sn nyie hata kwa siri rudisheni,hata haya hamna looooh! usuper star wa njaa tu nyie ndio mngeongoza kwa kutoa michango mikubwa kinyume chake nyie ndio mnaiba mtapukutika km ***** mi nipo hapa!
 
mkuu inawezekana ni matumizi mabaya ya hela,pia msimba mkubwa kama ule nadhani pia matumizi yatakuwa mengi...ila kama kweli kuna hujuma imefanyika basi ubinadam kazi

Mi nadhani kila kitu kilikuwa documented... Hasa mapato.. Kwenye matumizi hapo inategemea...

Lakini gharama za ujenzi wa majukwaa,kampuni ya mazishi,na vingine vina documents.. Sijui vyakula..
 
Duh mweka hazina alikua CLOUD mtoto wa ilala..
 
naskia milion 30 zilitumika kununulia suti nyeusi za tukio..

Kha! ivi ilikuwa lazima kuvaa suti nyeusi kama huna. Kwanini iwe gharama ya wafiwa? Kwani si wangevaa nguo zao nyeusi tu kama mtu hana suti. Hii kwakweli kwa mtizamo wangu ni mis-use of funds. Sidhani kama familia ya Kanumba ingekubaliana na hili.
 
 
Shitaki peke yako.Hatuna haja kuangalia ya KImagharibi.Hatujaja kuishi kutegemea mali za marehemu.Usilete uchonganishi.Usiwachonganishe waliofanikisha zoezi na kuwakashifu.Au ulitaka uteuliwe wewe!
 
Ulichoongea ni kweli kabisa. By the way, hivi walipata wapi ruhusa ya ku'spend hizo so called "70 million"? Its like karibia hela yote iliokusanywa wamesema imeenda kwenye gharama za mazishi wakati familia iliokua inamtegemea marehemu imeachwa with peanuts! Kwanza, its obvious msiba hauku cost all that money, and familia ilitakiwa kua na maamuzi ni jinsi gani msiba uwe na hata gharama zake. Alafu they should provide mchanganuo wa jinsi walivotumia hizo hela supported by receipts! Sio tu kudanganya watu. Yaani watu wengi wanalalamika sana, kamati imetia aibu!




 
Hilo nalo neno!

Mbona hawakurusha moja kwa moja msiba wa mzee kipara.....clouds wezi sana....wanafata kwenye maslahi tu..!!! Kwanza matangazo ya tv live hawawezi.....ili boa kishenzy siku ile...!!!
 
Binafsi naona tatizo ni kuwa na mtu mmoja tu "nguzo" katika familia au pengine hata katika ukoo mzima,anapoondoka sasa matokeo yake ndo yanakuwa kama hayo,msiba ulikuwa ni wa Kanumba iweje kamati isimhusishe hata ndugu mmoja wa Kanumba,eti alikuwepo akaondolewa kwa sababu kamati ilitaka ifanye mambo kwa uhuru zaidi,ni uhuru gani waliokuwa wanautaka zaidi ya ule wa kuiba,mimi nafikiri Familia yenyewe ndo inapaswa kujilaumu kwa kutengeneza mwanya huo.
 
Ni kawaida ya watu waOVU kupenda kuvaa mamiwani makubwa myeusi kuficha Sura zao huku dhamira zikiwasuta. Walikuwa wapigaji hawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…