SI KWELI Maziwa fresh ni tiba sahihi ya tatizo la vidonda vya tumbo

SI KWELI Maziwa fresh ni tiba sahihi ya tatizo la vidonda vya tumbo

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Vidonda vya tumbo ni tatizo linalosumbua watu wengi. Husababisha maumivu makali sana, kiasi cha kufanya liwe tatizo lisilovumilika kirahisi.

Katika kutafuta tiba, baadhi ya watu hutumia dawa za hospitalini, huku baadhi wakitumia dawa za asili.

E2CE031C-C502-49A1-9F8D-3059C9B9FB0E.jpeg

Pia, maziwa ni miongoni mwa dawa zinazo zungumzwa sana. Ni kweli kuwa maziwa hutibu tatizo la vidonda vya tumbo?
 
Tunachokijua
Vidonda vya tumbo ni michubuko inayotokea kwenye kuta za mfumo wa chakula, hasa kwenye sehemu ya tumbo au pia sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo.

Ukubwa wa vidonda hivi hutofautiana, kuanzia millimita chache hadi sentimita kadhaa.

Dalili za ugonjwa huu mara nyingi hutegemea umri pamoja na eneo husika vilipo vidonda hivi. Miongoni mwake ni -
  1. Maumivu makali ya kuvuta kwa misuli, au kuwaka moto kwa misuli ya tumbo
  2. Tumbo kujaa gesi mara kwa mara
  3. Kiungulia
  4. Kichefuchefu
  5. Kujisaidia choo chenye damu, au choo cheusi
  6. Kutapika uchafu wenye damu, au wenye rangi ya weusi
  7. Kupata maumivu kifuani, kama moto unaochoma
Sababu kubwa ya kutokea kwa tatizo la vidonda vya tumbo ni uwepo wa maambukizi ya bakteria jamii ya H. pylori pamoja na matumizi mabaya ya dawa za kupunguza maumivu zinazopatikana kwenye kundi la NSAIDs mfano aspirin, ibuprofen, mefenamic acid na diclofenac

Matibabu
Matumizi ya dawa za antibayotiki hufaa wakati huu, pia dawa za kudhibiti uzalishwaji wa asidi nyingi hupaswa kumezwa.

Ikiwa changamoto hii itaendelea kujirudia, pia ikiwa changamoto zinazosababishwa na ugonjwa huu kama vile kuziba kwa utumbo au kuvuja kwa damu tumboni zitatokea, upasuaji huwa ni chaguo sahihi.

Matumizi ya Maziwa kama tiba
Baadhi ya watu hudhani kuwa maziwa fresh husaidia kutibu tatizo hili. Madai haya hayana ukweli.

Maziwa huleta ahueni ya muda mfupi kwa kutengeneza utando juu ya kuta za vidonda. Aidha, aina hii ya maziwa huongeza uzalishwaji wa asidi tumboni pamoja na vimeng’enya vingine ambavyo baada ya kuisha kwa utando wa maziwa husababisha maumivu makali zaidi pamoja na kuongeza ukubwa wa tatizo.

Uthibitisho mwingine unatolewa pia na tovuti maarufu ya Afya, WebMD inayotoa maelezo kuwa maziwa yanaweza kuongeza ukubwa wa tatizo kwa kuzalisha asidi nyingi zaidi.

Hivyo, JamiiForums imebaini kuwa Mtu mwenye vidonda vya tumbo hashauriwi kutumia maziwa fresh kwa kuwa hayana uwezo wa kutibu na kufuta uwepo wa tatizo hili.
Fulu mikanganyiko. Ngoja waje wengine waseme tangawizi na pilipili ndio tiba sahihi
Nchi ya wajuaji wengi hii
 
Vidonda vya tumbo ni tatizo linalosumbua watu wengi. Husababisha maumivu makali sana, kiasi cha kufanya liwe tatizo lisilovumilika kirahisi.

Katika kutafuta tiba, baadhi ya watu hutumia dawa za hospitalini, huku baadhi wakitumia dawa za asili.

View attachment 2517925

Pia, maziwa ni miongoni mwa dawa zinazo zungumzwa sana. Ni kweli kuwa maziwa hutibu tatizo la vidonda vya tumbo?
Maziwa sio tiba zaidi yanaongeza vidonda vya tumbo kutokana na kusababishwa na release ya enzyme yenye acid kwa ajiri ya mmeng'enyo wake
 
Utafiti wa hivi karibuni unasema matumizi ya maziwa yanaweza kusababisha shida ya vidonda kuongezeka zaidi
20230215_130344.jpg
 
Hili linafahamika ni vile watanzania si wafuatiliaji na wadadisi. Maziwa hayasaidii kutibu wala kupoza vidonda vya tumbo. Huwa nashangaa wanaoshauri watu kutumia maziwa. Maziwa yanachubua ile coat ya kwenye kuta za tumbo.
 
Vidonda vya tumbo ni tatizo linalosumbua watu wengi. Husababisha maumivu makali sana, kiasi cha kufanya liwe tatizo lisilovumilika kirahisi.

Katika kutafuta tiba, baadhi ya watu hutumia dawa za hospitalini, huku baadhi wakitumia dawa za asili.


Pia, maziwa ni miongoni mwa dawa zinazo zungumzwa sana. Ni kweli kuwa maziwa hutibu tatizo la vidonda vya tumbo?
Nina jamaa wachache waliofanikiwa kupitia maziwa fresh pamoja na mchanganyiko wa dawa asilia itoanayo na "cannabis" na kufanikiwa kupona kabisa maziwa ya mbuzi,Kwa sasa wanakunywa,wanakula pilpili,maharage na hata juice ya malimao.
 
Sasa inakuwaje watu wanatumia na inaonekana kuwasaidia? Sayansi ni pana chief ujue, inapanuka na inapanuliwa kila kukicha.

Mfanye utafiti wa kuyapima na kuyasoma maziwa na msaada wake katika vidonda vya tumbo.

Isije kuwa asidi labda sio kisababishi cha tatizo. Maana ni kila mwanadamu anayo asidi nyingi tu tumboni na ni kali 'kweri kweri'

Kama serikali ingewekeza kwenye tafiti kuona labda ile effect ya kuupumzisha mwili inayotokana na maziwa ndiyo inayosaidia madonda ya tumbo kupona.
Kupumzisha mwili namaanisha rest. Kama tu ambavyo katoto kakinyonya maziwa kanalala, na mtu mzima akioiga glasi ya maziwa jioni anapata usingizi mnono -Fact

Inahitajika akili kuanza kuyaona matatizo kwa namna mpya ili tuyatatue.

Swali; Kama asidi ndio sababu, kwa nini dawa za kuituliza hazijawahi kufanikiwa kutibu.

Nadharia yangu ni; vidonda vitapona pale mtu atakapomaster kupumzika. Na vyote vinavyomsaidia mtu kupumzika basi vitasaidia kupona madonda hayo. Maziwa yakiwamo.
Vidonda vya tumbo ni tatizo linalosumbua watu wengi. Husababisha maumivu makali sana, kiasi cha kufanya liwe tatizo lisilovumilika kirahisi.

Katika kutafuta tiba, baadhi ya watu hutumia dawa za hospitalini, huku baadhi wakitumia dawa za asili.


Pia, maziwa ni miongoni mwa dawa zinazo zungumzwa sana. Ni kweli kuwa maziwa hutibu tatizo la vidonda vya tumbo?
 
Kwa Wahanga Wenzangu Wanaosumbuliwa

Mimi Huwa Nikitumia Tangawizi Huwa Vinapoa Kidogo ! Pia Nlishauriwa Kula Matunda Kama Parachichi, Tikiti ...Mboga za Majani,Mlenda, Bamia,Nyanya Chungu,

Pia Hautakiwi Kula Chakula Kingi Kwa Mara Moja
Unashauriwa Kula Kidogo Kidogo Kusaidia Mmeng’enyo Mzuri wa Chakula!
Kula Kidogo Kidogo Ila Mara kwa Mara!

Wali sio Mzurii unashauriwa Kula Ugali Dona sio Sembe!

Maji Mengiii Sanaa! Kiukweli Tangu Nianze Kufwata Utaratibu Huu! Namshukuru Mungu Naendelea Vzur Sanaa [emoji1317][emoji1317]
 
Vidonda vya tumbo ni tatizo linalosumbua watu wengi. Husababisha maumivu makali sana, kiasi cha kufanya liwe tatizo lisilovumilika kirahisi.

Katika kutafuta tiba, baadhi ya watu hutumia dawa za hospitalini, huku baadhi wakitumia dawa za asili.


Pia, maziwa ni miongoni mwa dawa zinazo zungumzwa sana. Ni kweli kuwa maziwa hutibu tatizo la vidonda vya tumbo?
ii ni kwel 100%
 
Back
Top Bottom