KWELI Maziwa ya Mama Hayaharibiki wala Kuchacha yakiwa Kifuani

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Mwanamke asipo mnyonyesha mtoto kwa zaidi ya siku moja maziwa yake huchacha na kuharibika.

Wanawake hushauriwa kumwachisha mtoto ziwa ili asidhurike kwa sababu maziwa hayo hukosa tena sifa ya kutumiwa na mtoto.

Ukweli upoje?
 
Tunachokijua
Maziwa ya matiti ya binadamu ni maziwa yanayotolewa na mama ili kumnyonyesha mwanawe. Maziwa hayo hutoa chanzo msingi cha lishe kwa watoto kabla ya wao kupata uwezo wa kula vyakula vingine, yaani watoto wachanga hadi umri kadiri wanavyoweza kuendelea kunyonyeshwa.

Maziwa ya mama huchacha?
Suala la Maziwa ya Mama kuchacha au kuharibika yakiwa Kifuani ni Imani potofu ndani ya Jamii, ni jambo ambalo halina ukweli kwasababu Maziwa hayachachi yakiwa ndani ya Mwili hata asiponyonyesha.

Endapo Mama ameajiriwa anashauriwa kufanya maandalizi mapema ya kukamua Maziwa na kuyagandisha kwenye Jokofu/Friji ili aweze kuyatumia kumlisha Mtoto pale likizo ya Uzazi inapomaliza.

Maziwa ya mama yaliyokamuliwa huweza kukaa na kuwa salama kwa lishe ya mtoto ndani ya miezi 6 kama yamegadishwa na siku 4 kama yamehifadhiwa kwenye jokofu bila kuganda, pia hukaa masaa 8 bila kuwekwa kwenye jokofu.
Hivyo, kwa sababu yoyote ile, mtoto hapaswi kuachishwa maziwa haya kwa kuwa hubeba virutubisho muhimu vinavyofaa kwa ukuaji bora wa afya ya mwili na akili.
Jamiiforums tunahitaji kufanya utafiti zaidi juu ya hili swala.

Kwa utafiti niliofanya katika tovuti za masuala ya afya , myoclonic na llli.org nimebaini kuwa kuwa na mazoea ya kumchelewesha mtoto kunyonya hupelekea mastitis, ugonjwa ambao huathiri mirija ya maziwa.

Huu ugonjwa hupelekea maziwa kuharibika aka kuchacha. Kwa hio wazee wetu wako sahihi. Ila suala la kukamua maziwa na kuyahifadhi vizuri ni jambo linalokubalika kisayansi.
 
Wakuu, hapa namnukuu mama anayenyonyesha ambapo amesema kuwa aliambiwa kama hajanyonyesha mtoto kwa muda mrefu basi hatakiwi kumnyonyesha mtoto kabla ya kukamua na kumwaga yale maziwa ya mwanzo kwasababu si mazuri kwa afya mtoto kutokana na kuwa yanakaa muda mrefu kwenye matiti.

Msaada kwa hili JamiiCheck ili wamama wanaokwenda kazini wenye watoto wasiwe na shaka.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…