Mazoea ya Serikali Kudhulumu Wadai Yarithiwa na TFF

Mazoea ya Serikali Kudhulumu Wadai Yarithiwa na TFF

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,455
Reaction score
73,145
Kumbe ni kweli mazoea hujenga tabia. Serikali yetu imeonyesha mazoea mabaya ya kutopenda kulipa madeni yake hadi ishtakiwe na kupambana mahakamani kisha linakuwa jambo LA kujisifia hadi bungeni kuwa tuko makini.
Tumeona hayo kesi ya deni LA mzungu hadi ndege kukamatwa, kule Canada nako, madeni ya makandarasi na watumishi wa umma ambayo hayajalipwa na ni vigumu kulipwa mwaka huu wa fedha kwa kisingizio cha uchaguzi.
Sasa na TFF nayo kumbe pamoja na kumfukuza kazi kocha Amunike bado hata hela zake hajalipwa na katushitaki FIFA. Hii ni aibu jamani.
Hivi mahela yote yale tunajifanya kugawa kwa wachezaji, tunagharamia kamati FEKI ya hamasa mamilioni kwenda mpaka Misri bila sababu ya msingi lakini kumlipa kocha haki yake mpaka TUSHTAKIWE FIFA?
Kweli mazoea hujenga tabia, serikali ni aibu kuwa na sifa ya udhulumati
Screenshot_20190912-093432.jpeg
 
Tatizo la wabongo ni ile roho ya korosho ambayo wengi tumeirithi tokea utotoni kwa sababu tu ya maisha magumu tuliyopitia. Haiwezekani umuajiri mtu wewe mwenyewe, halafu kwenye malipo unamsumbua na kuleta uswahili. Dawa ya deni ni kulipa tu.
 
Back
Top Bottom