Mbatia: Ndugai alipaswa kupeleka barua ya kujiuzulu bungeni na siyo kwa Katibu wa bunge, Nakata rufaa!

Sasa Betina na PhD ya Sheria. Anajisikiaje akiona yanayoendelea, wakati alikimbilia fasta kujipendrkeza ashike nafasi ya bosi wake!
 
Baada ya JYN kuandika barua batili kujiuzulu uspika, kwanza nilimuombea JYN msamaha
Kisha kuna kitu nilipendekeza kwenye uzi huu
Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge? nilipendekeza
Habari njema kwa watu wote, pendekezo No. 3 na No. 4 Katika bandiko hili, limetekelezwa kwa asilimia 100% kama lililopendekezwa.
Hivyo sasa ule ubatilifu katika barua ya kujiuzulu kwa JYN umeondolewa kama nilivyo shauri, kwa kuwasilishwa barua mpya halali, ambayo ni backdated.
Hivyo ile taarifa ya JYN kwa waandishi wa habari, kuwa ameandika barua kwa Katibu Mkuu CCM, sasa imebatilishwa na imefutwa kwenye website ya Bunge, barua rasmi ni kwa Katibu wa Bunge, na CCM kupewa nakala.
Hongera sana Bunge letu tukufu kuubatilisha ubatili huu. Sasa kwenye hili la Spika umebaki ubatili mmoja wa Naibu Spika, Dr. Tulia Akson kujiuzulu u Naibu Spika, kabla ya kugombea Uspika.
P
 
Atajiuzulu siku ya kupiga kura.
 
Mbatia anazeeka vibaya
Anahangaika bure tu, hawezi kushinda.
Mahakama ya Rufaa hawasikilizi shauri jipya.
Hilo lake ni jipya.

Shauri la msingi. Barua imepelekwa kwa Katibu wa CCM badala ya Bungeni.

Rufaa. Barua imepelekwa kwa Katibu wa Bunge na sio Bungeni.

Jamani sio bangi hizi?
 
Mbatia Wakati wa Mwendazake aliahidiwa majimbo 20 Bungeni, hivyo akaweka mortgage nyumba yake ili apate Mkopo wa benki kwa ajili ya kampeni.

Mwendazake hakumuachia Jimbo hata moja, kwa hiyo hana ruzuku, hana chanzo cha fedha na hana haiba ya siasa zinazoendana na Rais SSH. Benki wanataka marejesho, Mbatia hana hela, atapata wapi?

Kwa hiyo ameamua kuwa msumbufu fulani ili watu wa system wamuone ni mwiba na ikibidi watafute namna ya kumalizana naye.

Mark hii post, Mbatia atasumbua sana kwa sababu ya nyumba yake ya Mbezi Beach iliyo mbioni kupigwa mnada
 
The so called Separation of Power wala haipo japa Afrika...Ndugai Mwenyewe ni mtu wa hovyo sana wala Mbatia huna haja kuhangaikia mtu wa namna ile wa nini?
 
Mbatia sasa anakuwa mpuuzi, Katibu wa bunge ndio bunge, au anadhani Spika angeenda awasomee wabunge?
 
Wamemlazimisha Ndugai kuandika barua nyingine za kuhalalisha kujiuzulu na kum-out smart Mbatia,tusishangae.
 
Anatakiwa kujiuzulu kabla hajaomba uspika.
p
Huyo Mwalimu wako na PhD yake ya Sheria, anatuonyesha alivyo mweupe!
Halafu kafundisha Sheria! Anashindwaje kuchambua kipengele muhimu kama hicho!

Anafanya haramu iwe halali, halafu umemtengenezea andiko la TUTUGEMEE AJE KUWA SPIKA BORA😅😅

Ule wembamba ni ishara tu ya tamaa alizonazo ROHONI mwake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…