Mbatia: Ndugai alipaswa kupeleka barua ya kujiuzulu bungeni na siyo kwa Katibu wa bunge, Nakata rufaa!

Mbatia: Ndugai alipaswa kupeleka barua ya kujiuzulu bungeni na siyo kwa Katibu wa bunge, Nakata rufaa!

Sasa Betina na PhD ya Sheria. Anajisikiaje akiona yanayoendelea, wakati alikimbilia fasta kujipendrkeza ashike nafasi ya bosi wake!
 
James Mbatia amesema kufuatian hukumu ya leo juu ya kujiuzulu Spika Ndugai kinyume cha mutaratinu anaishukuru mahakama kwa maamuzi yake ya kumuonyesha barua ya Ndugai kwenda kwa Katibu wa bunge.

Mbatia amesema hukumu hiyo mimefungua mlango wa yeye kukata rufaa kwani katiba inasema barua itawasilishwa bungeni na siyo kwa Katibu wa bunge.

PIA SOMA: News Alert: - Mahakama Kuu yatupilia mbali kesi ya kupinga Ndugai kujiuzulu Uspika. Yasema hakuna ukiukwaji wa Katiba uliofanywa (28/01/2022)

Source: ITV habari

View attachment 2098850
Ni vigumu kuamini kuwa Mheshimiwa Ndugai hajui utaratibu wa kikatiba wa kujiuzulu nafasi ya uspika. Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri wa muungano wa Tanzania spika au naibu spika anaweza kujiuzulu nafasi yake kwa kuandika barua kwa BUNGE na kuisaini. Spika atahesabika kuwa amejiuzulu baada ya barua yake kupokelewa na Bunge.

Afisa wa bunge anayeshughulika na mambo ya utawala ni Katibu wa bunge. Lakini Ndugai ameandika barua ya kujiuzulu kwa Katibu wa CCM, mtu ambaye katiba haijamtaja katika mchakato wa spika kujiuzulu.

Kwa mantiki hiyo, kikatiba Ndugai bado hajajiuzulu, maana hajaandika barua ya kujiuzulu kwa mamlaka inayohusika!! Je hii imetokea kwa makusudi au kwa bahati mbaya? Sidhani kama angeamua kuchukua uamuzi mkubwa kiasi hicho bila ya kujiridhisha matakwa ya kikatiba kuhusu hatua hiyo au bila ya ushauri wa kisheria.

Ninaamini Ndugai amefanya hivyo kwa makusudì, huku akijua kuwa maadui zake amewapa mwanasesere badala ya mtoto!! Watakapogundua kuwa wamepewa mwanasesere atakuwa amejipanga kwa mapambano sawasawa!!

Kinachonishangaza zaidi ni katibu wa CCM kukubali kupokea barua hiyo ambayo kikatiba haikupaswa kuelekezwa kwake!! Nilidhani asingekubali kuipokea bali angemwelekeza mahali pa kuipeleka!!
Baada ya JYN kuandika barua batili kujiuzulu uspika, kwanza nilimuombea JYN msamaha
Kisha kuna kitu nilipendekeza kwenye uzi huu
Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge? nilipendekeza
3. Japo Spika Mhe. JYN tayari ameisha jiuzulu uspika, kujiuzulu huko, japo ni kujiuzulu batilifu, lakini kujiuzulu ni kujiuzulu na Spika amejiuzulu, lakini kwa kuheshimu katiba, lazima ubatili katika barua hizo uondolewe kwa kuandikwa barua rasmi kwa mujibu wa katiba.
4. Bunge lipokee kimya kimya barua mpya ya kujiuzulu kwa Spika iliyoandikwa kwa mujibu wa katiba, kisha Bunge ndio litoe copy kwa CCM.
Hitimisho.
Namalizia kwa lile swali la msingi la uzi huu
Je wajua, haramu Isipoharimishwa Inageuka halali?, na batili Isipobatilishwa inageuka halali!. Je, Tanzania, tuhalalishe ubatili huu wa kujiuzulu kinyume cha katiba kwa mkuu wa mhimili wetu wa Bunge? Kama katiba imeelekeza jinsi ya kufanyika kwa jambo fulani, kuna sababu gani ya msingi ya kutofuata katiba na badala yake tukumbatie ubatili?

Jumatatu Njema.
Pascal
Habari njema kwa watu wote, pendekezo No. 3 na No. 4 Katika bandiko hili, limetekelezwa kwa asilimia 100% kama lililopendekezwa.
Hivyo sasa ule ubatilifu katika barua ya kujiuzulu kwa JYN umeondolewa kama nilivyo shauri, kwa kuwasilishwa barua mpya halali, ambayo ni backdated.
Hivyo ile taarifa ya JYN kwa waandishi wa habari, kuwa ameandika barua kwa Katibu Mkuu CCM, sasa imebatilishwa na imefutwa kwenye website ya Bunge, barua rasmi ni kwa Katibu wa Bunge, na CCM kupewa nakala.
Hongera sana Bunge letu tukufu kuubatilisha ubatili huu. Sasa kwenye hili la Spika umebaki ubatili mmoja wa Naibu Spika, Dr. Tulia Akson kujiuzulu u Naibu Spika, kabla ya kugombea Uspika.
P
 
Baada ya JYN kuandika barua batili kujiuzulu uspika, kwanza nilimuombea JYN msamaha
Kisha kuna kitu nilipendekeza kwenye uzi huu
Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge? nilipendekeza

Habari njema kwa watu wote, pendekezo No. 3 na No. 4 Katika bandiko hili, limetekelezwa kwa asilimia 100% kama lililopendekezwa.
Hivyo sasa ule ubatilifu katika barua ya kujiuzulu kwa JYN umeondolewa kama nilivyo shauri, kwa kuwasilishwa barua mpya halali, ambayo ni backdated.

Hivyo ile taarifa ya JYN kwa waandishi wa habari, kuwa ameandika barua kwa Katibu Mkuu CCM, sasa imebatilishwa na imefutwa kwenye website ya Bunge, barua rasmi ni kwa Katibu wa Bunge, na CCM kupewa nakala.
Hongera sana Bunge letu tukufu kuubatilisha ubatili huu. Sasa kwenye hili la Spika umebaki ubatili mmoja wa Naibu Spika, Dr. Tulia Akson kujiuzulu u Naibu Spika, kabla ya kugombea Uspika.
P
Atajiuzulu siku ya kupiga kura.
 
Mbatia anazeeka vibaya
Anahangaika bure tu, hawezi kushinda.
Mahakama ya Rufaa hawasikilizi shauri jipya.
Hilo lake ni jipya.

Shauri la msingi. Barua imepelekwa kwa Katibu wa CCM badala ya Bungeni.

Rufaa. Barua imepelekwa kwa Katibu wa Bunge na sio Bungeni.

Jamani sio bangi hizi?
 
James Mbatia amesema kufuatian hukumu ya leo juu ya kujiuzulu Spika Ndugai kinyume cha mutaratinu anaishukuru mahakama kwa maamuzi yake ya kumuonyesha barua ya Ndugai kwenda kwa Katibu wa bunge.

Mbatia amesema hukumu hiyo mimefungua mlango wa yeye kukata rufaa kwani katiba inasema barua itawasilishwa bungeni na siyo kwa Katibu wa bunge.

PIA SOMA: News Alert: - Mahakama Kuu yatupilia mbali kesi ya kupinga Ndugai kujiuzulu Uspika. Yasema hakuna ukiukwaji wa Katiba uliofanywa (28/01/2022)

Source: ITV habari

View attachment 2098850
Mbatia Wakati wa Mwendazake aliahidiwa majimbo 20 Bungeni, hivyo akaweka mortgage nyumba yake ili apate Mkopo wa benki kwa ajili ya kampeni.

Mwendazake hakumuachia Jimbo hata moja, kwa hiyo hana ruzuku, hana chanzo cha fedha na hana haiba ya siasa zinazoendana na Rais SSH. Benki wanataka marejesho, Mbatia hana hela, atapata wapi?

Kwa hiyo ameamua kuwa msumbufu fulani ili watu wa system wamuone ni mwiba na ikibidi watafute namna ya kumalizana naye.

Mark hii post, Mbatia atasumbua sana kwa sababu ya nyumba yake ya Mbezi Beach iliyo mbioni kupigwa mnada
 
The so called Separation of Power wala haipo japa Afrika...Ndugai Mwenyewe ni mtu wa hovyo sana wala Mbatia huna haja kuhangaikia mtu wa namna ile wa nini?
 
Mbatia sasa anakuwa mpuuzi, Katibu wa bunge ndio bunge, au anadhani Spika angeenda awasomee wabunge?
 
Mbatia siyo mjinga anaelewa anachofanya. Hayo maswali ya kejeli tunayomtupia,yule amewahi kuwa mbunge anaelewa kanuni na taratibu zote. Sote tuliambiwa Ndugai amewasilisha barua ya kujiuzuru kwa Katibu mkuu wa ccm, na nakala amepewa katibu wa bunge. Leo serikali imetoa barua ya kwenda kwa Katibu wa bunge na kwenda kwa Katibu mkuu wa ccm, tofauti na ilivyokuwa awali, ni wazi wameona Mbatia ana hoja.
Wamemlazimisha Ndugai kuandika barua nyingine za kuhalalisha kujiuzulu na kum-out smart Mbatia,tusishangae.
 
Anatakiwa kujiuzulu kabla hajaomba uspika.
p
Huyo Mwalimu wako na PhD yake ya Sheria, anatuonyesha alivyo mweupe!
Halafu kafundisha Sheria! Anashindwaje kuchambua kipengele muhimu kama hicho!

Anafanya haramu iwe halali, halafu umemtengenezea andiko la TUTUGEMEE AJE KUWA SPIKA BORA😅😅

Ule wembamba ni ishara tu ya tamaa alizonazo ROHONI mwake!
 
Back
Top Bottom