Mbegu zipi za mahindi za DK zinafanya vizuri?

Mbegu zipi za mahindi za DK zinafanya vizuri?

Sijajua unapenda nijazie wapi lakini ngoja niboreshe andiko langu lote kwa ujumla kuhsu kilimo cha Mahindi.

1.Kitu muhimu kabla ya kulima shamba hakikisha umelilisha chakula cha kutosha. Chakula cha shamba( udongo) ni samadi.Samadi huwaamsha "soil microbes" ambao wanaumuhimu mkubwa katika kuandaa na kutengeneza virutubisho vya udongo.Mbolea za viwandani hutumika km "supplement" tu na si za kuzitegemea 100%. Afya ya udongo haiboreki kwa kuweka mbolea za viwandani. Ni vema kwanza tukalijua hilo.

2. Kwa kawaida gari (tipa) lenye ujazo wa 4.5m3 linaweza kubeba trip 4 kwa eka moja na ikatosha. Uzuri wa samadi ya ngo'mbe inadumu kwenye udongo kwa mda mrefu. Kazi ya kumwaga samadi shambani ifanywe miezi ya kiangazi Mfano miezi ya August,September October hadi mwanzoni mwa Novemba. Kisha uisambaze kabla ya mvua kunyesha.

3.Ukisha rutubisha shamba hapo ndo unaweza kuzitafuta hizo gunia 40. Sifa ingine ya samadi ni kutunza unyevu hasa miaka hii yenye tatizo la upungufu wa mvua.

4. Km utatumia vibarua wakati wa upandaji basi hakikisha umewasimamia vzri ili wachimbe mistari, mashimo na kupanda mbegu kwa usahihi.

5. Nafasi za upandaji wa mahindi inategemea na aina ya mbegu na ubora wa shamba. Km mbegu yako ni fupi unaweza kutumia "Spacing" ya kubananisha lakini hapo hapo ukiangalia ubora wa shamba. Km shamba ni dhaifu(halina rutuba ya kutosha) si vema kubananisha mimea itagombania chakula na kuwa dhaifa.
Hivyo Spacing zipo za aina nyingi. Utachagua mojawapo kutegemea na hizo factors juu nilizozieleza.
20cmx75
25cmx75
30cmx75-(Very common used).
60cmx75(two seeds per hole)
N.k


5.Palizi ya kwanza ifanyike wiki 2 hadi 3 toka mahindi kuoto kutegemea na kasi ya uotaji wa magugu. Hatua ya palizi ni muhimu sana kwani ukichelewa yataweza kuathiri ukuaji wa mahindi na vivyo hivyo kuathiri mavuno.

Nb: Mahindi ni mimea ambayo iko "sensitive" sana na magugu. Ukiyapalilia baada ya muda mfupi huanza kubadilika na kuwa mazuri na ukiyaacha kwenye msitu wa majani baada ya siku chache utakuta yameathirika. Hivyo ni vema shamba la mahindi liwe safi muda wote.
Kwa utaalam wako je kuna uwezekano wa kufanya maximization of output kwa zao kama maharage?
 
Kwa utaalam wako je kuna uwezekano wa kufanya maximization of output kwa zao kama maharage?
Maximization inawezekana kwenye kila zao. Mojawapo ya maximization techniques ni pamoja na kuzingatia nafasi za upandaji ili kuwa na mimea mingi shambani. Shida kubwa kwa wakulima wetu ni kupanda ovyo ovyo. Unakuta mtu anasema amelima eka 5 ila ukihesabu jumla ya mimea iliyo shambani ni sawa na eka moja.

Pili,panda mbegu bora. Huwezi ku maximize production km utalima mbegu zisizo bora.

Tatu,panda kwa wakati.

Nne palilia kwa wakati.

Nb. Mbolea za viwandani si lazima sana kwenye maharage, kwani maharage yana uwezo kufix Atmospheric Nitrogen into organic nitrogen. Kwa kifupi sana.
 
Maximization inawezekana kwenye kila zao. Mojawapo ya maximization techniques ni pamoja na kuzingatia nafasi za upandaji ili kuwa na mimea mingi shambani. Shida kubwa kwa wakulima wetu ni kupanda ovyo ovyo. Unakuta mtu anasema amelima eka 5 ila ukihesabu jumla ya mimea iliyo shambani ni sawa na eka moja.

Pili,panda mbegu bora. Huwezi ku maximize production km utalima mbegu zisizo bora.

Tatu,panda kwa wakati.

Nne palilia kwa wakati.

Nb. Mbolea za viwandani si lazima sana kwenye maharage, kwani maharage yana uwezo kufix Atmospheric Nitrogen into organic nitrogen. Kwa kifupi sana.
hapo kuna kitu nimejifunza
 
Gunia 40, inawezekana lakin sio kitu rahisi. Walioitengeneza hyo mbegu management walizofanya most of the time haziko sawa na ambazo wakulima wetu wanafanya. Hizo 40bags tunasema 'under favourable conditions' and while other factors remain constant.
 
Gunia 40, inawezekana lakin sio kitu rahisi. Walioitengeneza hyo mbegu management walizofanya most of the time haziko sawa na ambazo wakulima wetu wanafanya. Hizo 40bags tunasema 'under favourable conditions' and while other factors remain constant.
Umesema mwenyewe si kitu rahisi lakini inawezekana. Hata Yesu alisema kwenda mbinguni si kitu rahisi rahisi lakini kwa mwenye bidii inawezekana. Mambo mazuri yote ndivyo yalivyo unahitaji bidii na juhudi ili kuyafikia.
 
Somo zuri sana ukizingatia pia tayari mvua zimeanza kunyesha. Vipi na aina hizi za mbegu "AMINIKA " ubora wake ikoje kwa wenye uzoefu nazo.
 
Sijajua unapenda nijazie wapi lakini ngoja niboreshe andiko langu lote kwa ujumla kuhsu kilimo cha Mahindi.

1.Kitu muhimu kabla ya kulima shamba hakikisha umelilisha chakula cha kutosha. Chakula cha shamba( udongo) ni samadi.Samadi huwaamsha "soil microbes" ambao wanaumuhimu mkubwa katika kuandaa na kutengeneza virutubisho vya udongo.Mbolea za viwandani hutumika km "supplement" tu na si za kuzitegemea 100%. Afya ya udongo haiboreki kwa kuweka mbolea za viwandani. Ni vema kwanza tukalijua hilo.

2. Kwa kawaida gari (tipa) lenye ujazo wa 4.5m3 linaweza kubeba trip 4 kwa eka moja na ikatosha. Uzuri wa samadi ya ngo'mbe inadumu kwenye udongo kwa mda mrefu. Kazi ya kumwaga samadi shambani ifanywe miezi ya kiangazi Mfano miezi ya August,September October hadi mwanzoni mwa Novemba. Kisha uisambaze kabla ya mvua kunyesha.

3. Ukisharutubisha shamba hapo ndo unaweza kuzitafuta hizo gunia 40. Sifa ingine ya samadi ni kutunza unyevu hasa miaka hii yenye tatizo la upungufu wa mvua.

4. Km utatumia vibarua wakati wa upandaji basi hakikisha umewasimamia vzri ili wachimbe mistari, mashimo na kupanda mbegu kwa usahihi.

5. Nafasi za upandaji wa mahindi inategemea na aina ya mbegu na ubora wa shamba. Km mbegu yako ni fupi unaweza kutumia "Spacing" ya kubananisha lakini hapo hapo ukiangalia ubora wa shamba. Km shamba ni dhaifu(halina rutuba ya kutosha) si vema kubananisha mimea itagombania chakula na kuwa dhaifa.
Hivyo Spacing zipo za aina nyingi. Utachagua mojawapo kutegemea na hizo factors juu nilizozieleza.
20cmx75
25cmx75
30cmx75-(Very common used).
60cmx75(two seeds per hole)
N.k

5. Palizi ya kwanza ifanyike wiki 2 hadi 3 toka mahindi kuoto kutegemea na kasi ya uotaji wa magugu. Hatua ya palizi ni muhimu sana kwani ukichelewa yataweza kuathiri ukuaji wa mahindi na vivyo hivyo kuathiri mavuno.

Nb: Mahindi ni mimea ambayo iko "sensitive" sana na magugu. Ukiyapalilia baada ya muda mfupi huanza kubadilika na kuwa mazuri na ukiyaacha kwenye msitu wa majani baada ya siku chache utakuta yameathirika. Hivyo ni vema shamba la mahindi liwe safi muda wote.
Vipi kwenye parizi naweza tumia dawa za kuua magugu??
 
Za kawaida tu hazina maajabu kivilee!
Chief vipi kuhusu na hizi mbegu SEED CO, ziko vizuri.!? Mfano nimeona hii TUMBILI SC 419 inatoa Hadi gunia 40 - 48 per Eka.. Na ni kwa muda mfupi sana Siku 75 - 90 unavuna..

Mawazo Yako yatanisaidia sana Chief..
 
Huyu hajawahi kulima mm nalima na kujaribu kufuata taratibu zote lakini hakuna kitu Kama hicho
 
Shida yenu mnalima km babu zenu walivyolima ndio maana kila kitu hamuamini. We mtu unapanda ovyo ovyo, hauzingatii idadi ya mimea kwa ekari, shamba kubwaa mimea michache, hufanyi palizi kwa wakati, mbolea unaweka mara moja, toka babu hadi mjukuu shamba halijawahi rutubishwa kwa mbolea za asili kwanini usivune gunia 8 kwa ekari?

Hizo gunia 40-44 unazipata km shamba litakua na rutuba ya kutosha, na upande kwa "proper spacing"itakayokupa mimea 20,000 hadi 22,000. Mfano kwa spacing ya 25cmx75cm plant population per acre 4000m2÷0.1875m2/plants=21,000plants.

Hii ndo idadi ya mimea inayopaswa kuota na kuzaa kwenye eneo la ekari moja.

Sasa shida wengi mnawaachia vibarua kuchimba mistari na kupanda mbegu. Matokeo yake wanachimba mistari na mashimo kwa umbali ili wamalize kazi haraka. Hapo ukihesabu mimea kwenye ekari unakuta kuna mimea elfu 15 au chini ya hapo. Ndio maana mkiona hizi takwimu hamuamini. Ukiwa serious haya mambo yanawezekana.
Mkuu, tusaidie na ishu ya mbolea.
Ni mbolea zipi zinatumika kukuzia mahindi na zipi ni nzuri kwa ajiri ya kuzalishia mahindi.???
 
Je kwa ukanda wa Geita nataka kulima mahindi February hii ili nivume mwezi WA Tano,je mbegu ipi nitumie inatokomaa haraka nanitapata mavumo mengi
 
DK777 -Hukomaa kwa siku 130-150, hukupa magunia 40-44 km shamba ni zuri na utazingatia kanuni bora za kilimo.
-Uzuri wa hii mbegu hata km shamba halina rutuba ya kutosha bado hujitahidi kuzaa tofauti na mbegu zingine.

DK9089 Hukomaa kwa siku 110-120,hukupa magunia 40-44.

Tatizo la DK 9089 mimea yake inaathiriwa sana na ugonjwa wa kuoza shoots au mimea "ku- misbehave".
kumisbehave km vp? mm nimepanda dk9089 na kuna kam tatzo imechanua (mbelewele) lakn mahnd meng hayana watoto na yana siku 63?watalaam wa dk mje hapa
 
Back
Top Bottom