Sol de Mayo
JF-Expert Member
- Sep 10, 2016
- 6,515
- 6,230
KWai haki yake,ila akuna ajuaye mwisho wake
Mtu anajiuwa akijua eti anaepoenda anaenda kurest hahhhaaaa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
KWai haki yake,ila akuna ajuaye mwisho wake
Safi. Nikajua umejiunga nao 😅😅Mkuu mimi siwezi chezea timu ya wazinzi na wapiga punyeto.
Hapa ndoa ndio mpango mzima.
🤣🤣🤣
Leo zamu yetu...Hivi nyie wanaume ni mmekuja kuishiwa akili au shida ni gani?
Watu wana stress sana aisee daah...Hivi nyie wanaume ni mmekuja kuishiwa akili au shida ni gani?
BROWN suger watu WA mbeya mnakwama wapi?Hapa kataa ndoa ni halali Yao kujichukulia points ....daaa
Kupenda gani huko? Huo ni ujinga!Duuh!
Wivu uliopitiliza huo.
Kuna watu wanapenda vibaya mno.
CHANZO kwanini haisemwi ni KUKOSEKANA UAMINIFU KTK NDOA/ USALITI KWA WANANDOA!!!na iwekwe wazi WITO: wanandoa waache UZINZI na uasherati na UKAHABA/PROSTITUTION kupunguza haya mauaji yanayotakana na USALITI.View attachment 2549166
Mtoto wa marehemu akiwa Hospitalini akiendelea na matibabu
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na operesheni, misako na doria katika maeneo mbalimbali ya Mkoa ili kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao. Aidha tumeendelea kupata mafanikio kwa kukamata watuhumiwa wa makosa mbalimbali na kuwafikisha mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Benjamin E. Kuzaga amesema Mnamo tarehe 08.03.2023 majira ya saa 04:00 usiku huko maeneo ya Nyigamba, Mtaa wa Itezi, Jijini Mbeya, mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la HAMIS PIUS [41] Dereva, Mkazi wa Nyigamba alifariki dunia kwa kuungua moto baada ya kujifungia ndani ya chumba anacholala na mke wake aitwaye REBELIA MAKOSO [38] Mkazi wa Nyigamba kisha kumwaga mafuta ya Petroli na kuwasha moto.
Wakati wa tukio hilo, mke wa marehemu alipiga kelele kuomba msaada kwa mtoto wake aitwaye MKESHILISI HAMIS [21] ambaye alikuwa chumba kingine ambaye alikwenda kutoa msaada kwa kupiga teke mlango wa chumba na kisha kumuokoa mama yake lakini baba yake alikataa kutoka ndani na kupelekea kuungua hadi kupoteza maisha.
Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi. Majeruhi ambao ni mke na mtoto wa marehemu wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali Teule ya Ifisi iliyopo Mji Mdogo wa Mbalizi kutokana na majeraha ya moto waliyoyapata mwilini.
View attachment 2549167
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Benjamin E. Kuzaga
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa jamii kuachana na vitendo vya kujichukulia sheria mkononi. Aidha tunatoa wito kwa jamii kutatua migogoro yao ya kifamilia na ndoa kwa kukaa meza moja ya usuluhishi badala ya kuchukua maamuzi magumu kama hayo.
Kati ya alichokifanya na kumfukuza yapi ni maamuzi ya kiume?asa huyo mwanaume na yeye jamani alikosa kabisa maamuzi ya kiume kweli, ai angemfukuza tu huyo mke wake