Pre GE2025 Mbeya: Kikundi cha 'Wanawake shujaa' wilaya ya Rungwe, wamemchangia shilingi milioni moja Rais Samia fomu ya kugombea Urais

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Kikundi cha 'Wanawake shujaa' wilaya ya Rungwe, mkoani Mbeya wamechangia fedha zaidi ya shilingi milioni moja za Kitanzania Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi wa mwaka huu (2025) kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)

Zoezi hilo limeongizwa na Dkt. Yasinta Mafwenga aliyekuwa mgeni rasmi kwenye kongamano la wanawake la kujikwamua kiuchumi ambapo qanawake hao wamesema wamefikia hatua hiyo baada ya kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Your browser is not able to display this video.
 
Rungwe njaa na ukame umeshamiri!
Dkt. Yasinta Mafwenga ,kwanini usiwasaidie hizo fedha walemavu, wajane na yatima,ili waweze kujikomboa???
Nani alikuambia Saa100 anahitaji milioni?
Ukija kujaza fomu kugombea ni wazi utakuwa ulitoa rushwa.
 
Wanawake wa Mbeya , utapenda.
Na ile rekodi yenu ya "Umbili" mko vizuri.
 
Hii fomu kwa bei yake ishakuwa overprice sasa.

Nasikia fisi wanaosumbua simiyu baada ya kuona serikali inawatafuta wameamua nao kumchangia raisi fomu ya uraisi
 
Kujipendekeza tu! Nani kawaambia Maza anakosa hiyo 1 million.
 
wanawake hao ni wazalendo wa kiwango cha juu sana na wanawakilisha mamilioni ya wananchi na waTanzania wote wenye mapenzi ya dhati dhidi ya Dr.Samia Suluhu Hassan na wenye nia ya kumchangia chochote kitu pia 🐒
 
Kikundi cha 'Wanawake shujaa' wilaya ya Rungwe, mkoani Mbeya wamechangia fedha zaidi ya shilingi milioni moja za Kitanzania Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi wa mwaka huu (2025) kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)

Zoezi hilo limeongizwa na Dkt. Yasinta Mafwenga aliyekuwa mgeni rasmi kwenye kongamano la wanawake la kujikwamua kiuchumi ambapo qanawake hao wamesema wamefikia hatua hiyo baada ya kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
Your browser is not able to display this video.
 
Haya maigizo ni kwa faida ya Nani?
 
Hiyo fomu ya nini sasa ilhali hana mtu wa kushindana naye ndani ya chama chao.
 
Yeye ana hela mpaka anagawa kwa timu za mpira, kila goli Mil5.. nyie mnahangaika kuchangishana Mil1...

"Upumbafu ni kipaji kuna watu wanazaliwa nacho:..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…