Mbeya kumekucha, nategemea makubwa kutoka kwa Rais Samia

Mbeya kumekucha, nategemea makubwa kutoka kwa Rais Samia

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Wadau niko mbeya kwa ajili ya maonesho ya nane nane, nimeona mwitikio ni mkubwa sana ,unaweza kupotea ulikotokea ,hii imenipa picha kwamba watanzania wana kiu ya kusikia kero za kilimo zinatatuliwa.

Nchi yetu kwa sasa haina chakula kabisa. Hata hawa NMC hawana akiba tena. Tutasingizia mvua ilikuwa haitoshi lakini hapana mimi nachojua wakulima walishindwa kumudu bei ya pembejeo. Kama yale maeneo yanayozalisha chakula tungeyapa kipaumbele mahindi yangekuwa mengi sana

Serikali angalieni maeneo kama Rukwa, Mbeya, Ruvuma na Katavi ikiwezekana wakopesheni hawa wakulima pembejeo kama mbolea na mbegu mtakuja kunishukuru.

Benki ya kilimo mikopo yake ni migumu kwa wakulima wa vijijini kuipata na masharti yake ni magumu , pelekeni mbolea Rukwa na maeneo mengine ya kimkakati. Wakopesheni mbolea mkifanya hivyo hata vijana wanaokaa vijiweni watalima
 
Wadau niko mbeya kwa ajili ya maonesho ya nane nane, nimeona mwitikio ni mkubwa sana ,unaweza kupotea ulikotokea ,hii imenipa picha kwamba watanzania wana kiu ya kusikia kero za kilimo zinatatuliwa.
alima
Tupia picha ya hayo maonyesho,umeongea vizuri sana.
 
Wadau niko mbeya kwa ajili ya maonesho ya nane nane, nimeona mwitikio ni mkubwa sana ,unaweza kupotea ulikotokea ,hii imenipa picha kwamba watanzania wana kiu ya kusikia kero za kilimo zinatatuliwa...
Neno lako zuri, ila hebu tusiaidie pia kutafiti aspects zingine. Bado kuna kazi kubwa sana katika Kilimo kwenye mambo mengi huko Mbeya na kwingineko.

Mfano bei za mazao ya biashara kama chai, parachichi nk. Shida si pembejeo peke yake watu hawakipendi kilimo kwa sababu ya kukosekana kwa uwiano wa mitaji vis a vis faida!
 
Mbeya hiyo hali ni ya Kawaida miaka yote iko hivyo.
 
Back
Top Bottom