DOKEZO Mbeya: Mwanafunzi alazwa baada ya kupata kipigo kutoka kwa Walimu wa Shule ya Sekondari Rohila, inadaiwa alidokoa maandazi manne

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kusema ukweli baadhi ya walimu nchi hii wanaendekeza sana dhiki na kufanya kada ya ualimu iendelee kudharaurika kwa roho zao za kimaskini, maandazi ndo yakumjeruhi mwanafunzi kweli..??! ...
 
Hayo maandazi manne unayaona machache lakini ingekuwa kayaiba uraiani wenda yangesababisha kifo chake.

Na huyo kijana anavyo onekana amesha kuwa sugu huu ujasiri wa kuvunja dirisha ili atoroke ni wa hali ya juu sana.
Hapa ndio huwa tunapishana na nyie
Nchi inaongozwa na sheria sio sheria mkononi

Hata kama ni kibaka kwani hakuna polisi au kumfukuza shule ?

Huko uraiani angeiba wangemuuwa kwa mandazi 4
Sasa ni sifa hizo za kushabikia hayo

Hao waalimu hawana sifa za kuwa waalimu
Mwalimu anafundisha nidhamu kwa watoto pia
Na kuna wazazi pia wa kujulishwa maendeleo ya watoto
Kwanini mshabikie kupigwa kwake?
Imagine kesho yakimuta mwanao kabondwa hivyo utasemaje

Usiseme utafurahia kwa sababu ni uongo
 
Mtoto kuiba chakula si ana njaa jamani
Na hiyo bandeji hospital za serikal [emoji2301]
Waonezi tu hao
Ukute majitu ya hivyo hata wao ni majizi tu tena zaidi
Mbona wanaiba vyakula vya watoto kila kukicha
Tuna watoto na wanatuambia

Haya twende kwenye bandage hiyo itafikiri wanamkomesha

Ngoja nimtafute D. Gwajima kwanza
 
Kusema ukweli baadhi ya walimu nchi hii wanaendekeza sana dhiki na kufanya kada ya ualimu iendelee kudharaurika kwa roho zao za kimaskini, maandazi ndo yakumjeruhi mwanafunzi kweli..??! ...
Shida suo mandazi,hapo ni suala la nidham
 
Ualimu shida Sana 😀lakini huyo mtoto wamuangalie vizuri asome amalize tu atafunzwa na wazaziwake ya nn kujipa presha
 
Muuguzi wa Hospitali aeleza
Mmoja wa wauguzi wa kike ambaye amempokea mgonjwa huyo amesema “Aliletwa hapa akiwa hayupo vizuri kiafya, ana majeraha yanayoonekaa ni ya kupigwa eneo la uso, mguuni na mikononi.

Kuna mmoja wao amewezeshwa

Sijui duka lilikuwa ghorofani!!!
 
Baada ya kupata taarifa kuwa mwanafunzi huyo amelazwa inadaiwa Walimu wakageuza kibao na kudai mwanafunzi ameumia wakati akiruka dirishani baada ya tukio la wizi wa maandazi.
Muuzaji alikuwa wapi?
 
Chanzo kutoka shuleni kinaeleza kuwa licha ya kinachoendelea, shule imegeuza kibao na kumtaka baba wa mwanafunzi huyo alipe gharama za kioo cha dirisha ambacho wanadai mwanafunzi alikivunja wakati akitoroka baada ya kuiba maandazi.
Bora huyo aliiba maandazi, miaka ya nyuma tukiwa shule mwenzetu mmoja alivunja duka la shule akaiba sigara
 
Nilivyomuelewa daktri, kwamba, majeraha ya mwanafunzi yaliongezeka baada ya kuruka kupitia dirisha la vioo. Pata picha dogo anapita kwenye kioo! Mana walimu wamemtaka mzazi wa mwanafunzi alipe kioo.

Kwa hili walimu wanaweza kujivua kwa sababu, ni wajibu wa walimu kumchukulia hatua mwanafunzi mtovu wa nidhamu. Sasa, labda hao walimu walikuwa ndio wanaanza kumuhoji mwanafunzi au walimchapa hata viboko viwili, na yeye akaamua kukimbia kupitia dirisha la kioo, je, makosa ni ya nani?

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…