Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Akizindua wiki ya nenda kwa usalama barabarani kimkoa, Kamanda Kuzaga amewataka madereva wa Pikipiki, Bajaji, Magari madogo na magari ya abiria kuhakikisha vyombo vyao vya moto zinakaguliwa na wakaguzi wa magari wa Jeshi la Polisi waliopo katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya ili kuangalia ubora wake na kama vina sifa ya kutembea barabarani.
Naye, Mwenyekiti wa Usalama barabarani Mkoa wa Mbeya Eng. Rajab Ghulika amewataka madereva kujitokeza kuhudhuria mafunzo ya udereva ili kuwajengea uwezo na umahiri wa matumizi ya vyombo vya moto ikiwa ni pamoja na kujikumbusha alama na michoro mbalimbali ya usalama barabarani.
Wiki ya nenda kwa usalama barabarani imeambatana na ukaguzi wa vyombo vya moto, ubandikaji stika za nenda kwa usalama, utoaji wa elimu ya usalama barabarani kwa madereva na watumiaji wengine wa barabara Pamoja na utoaji wa mafunzo maalum ya udereva kwa madereva na utoaji vyeti vya udereva kwa wahitimu. Kilele cha maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani kitafanyika Aprili 20, 2023 katika uwanja wa Ruanda Nzovwe Jijini Mbeya.