John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Mnamo tarehe 03.03.2022 majira ya saa 08:00 asubuhi huko Mtaa wa Igodima, Kata ya Iganzo, Tarafa ya Sisimba, Jijini Mbeya, Kijana aitwaye SHADRACK ZACHARIA [28] Mpiga Picha na Mkazi wa Igodima Jijini Mbeya anayeonekana kwenye “clip” ya video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii akishambuliwa kwa kupigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na viongozi wa Kata ya Iganzo kwa kile kinachoelezwa ni kutoa lugha ya matusi na kuwapiga picha bila idhini yao wakati wakifanya shughuli za maendeleo katika Mtaa wa Igodima.
Chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliotokana na kukataa kutoa eneo kwa ajili ya kupitisha njia ya mtaa.
Awali, mama wa mhanga aitwaye ESTHER ANDREW [58] Mratibu Elimu Kata na Mkazi wa Igodima kabla ya kununua eneo hilo wakazi wa eneo hilo walikuwa wanapita njia lakini baada ya kununua na kujenga nyumba aliziba njia, ndipo wakazi wa mtaa huo walifika ofisi za kata kutoa malalamiko ambayo yaliamuliwa kwenye kikao kuwa kila upande utoe hatua moja ili kupitisha njia ya mtaa.
Hivyo siku hiyo ya tarehe 03.03.2022 asubuhi Diwani wa Kata akiwa ameongozana na Mwenyekiti wa Mtaa na wananchi walifika hadi eneo husika na kuanza kuchonga barabara ndipo ugomvi ulitokea.
Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi mkoani hapa linawashikilia watuhumiwa watatu kwa mahojiano ambao ni:-
1. DANIEL WILLIAM [35] Diwani wa Kata ya Iganzo.
2. ERASTO MWANKENJA [48] Afisa Mtendaji Kata ya Iganzo.
3. HENJE MBOMBO [74] Mkazi wa Iganzo.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linalaani tukio hilo na linatoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake watafute suluhisho la migogoro yao kwa kufuata njia zilizo sahihi ikiwa ni pamoja na kuvihusisha vyombo vya haki likiwemo Jeshi la Polisi kwa hatua zaidi za kisheria ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza kwa kutofuata sheria.
Chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliotokana na kukataa kutoa eneo kwa ajili ya kupitisha njia ya mtaa.
Awali, mama wa mhanga aitwaye ESTHER ANDREW [58] Mratibu Elimu Kata na Mkazi wa Igodima kabla ya kununua eneo hilo wakazi wa eneo hilo walikuwa wanapita njia lakini baada ya kununua na kujenga nyumba aliziba njia, ndipo wakazi wa mtaa huo walifika ofisi za kata kutoa malalamiko ambayo yaliamuliwa kwenye kikao kuwa kila upande utoe hatua moja ili kupitisha njia ya mtaa.
Hivyo siku hiyo ya tarehe 03.03.2022 asubuhi Diwani wa Kata akiwa ameongozana na Mwenyekiti wa Mtaa na wananchi walifika hadi eneo husika na kuanza kuchonga barabara ndipo ugomvi ulitokea.
Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi mkoani hapa linawashikilia watuhumiwa watatu kwa mahojiano ambao ni:-
1. DANIEL WILLIAM [35] Diwani wa Kata ya Iganzo.
2. ERASTO MWANKENJA [48] Afisa Mtendaji Kata ya Iganzo.
3. HENJE MBOMBO [74] Mkazi wa Iganzo.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linalaani tukio hilo na linatoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake watafute suluhisho la migogoro yao kwa kufuata njia zilizo sahihi ikiwa ni pamoja na kuvihusisha vyombo vya haki likiwemo Jeshi la Polisi kwa hatua zaidi za kisheria ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza kwa kutofuata sheria.
Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA