Pre GE2025 Mbeya: Wanawake wamchangia Rais pesa ya fomu ya ugombea

Pre GE2025 Mbeya: Wanawake wamchangia Rais pesa ya fomu ya ugombea

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

the guardian 17

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
395
Reaction score
570
Kikundi cha Wanawake SHUJAA Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya wamchangia Fedha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zaidi ya Milioni Moja kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea Urais, ikiwa ni kumuunga mkono katika jitihada zake za uongozi.

Zoezi hilo limeongozwa na Dkt. Yasinta Mafwenga ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye kongamano la wanawake la kujikwamua kiuchumi.

Wanawake hao wamesema wamefikia hatua baada ya kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais Dkt. Samia, ambapo katika Wilaya ya Rungwe, huduma za afya na maji zimeimarishwa kwa kiwango kikubwa.

Baadhi ya vituo vya afya vilivyojengwa katika Wilaya ya Rungwe ni pamoja na Kituo cha Afya Ikuti, Masukulu, Isongole na Mpuguso.
 
Kwani zile zilizochangwa na walimu wakuu wa kule Bukoba hazikutosha au ndio kujipendekezalism kunaendelea. Lkn maandiko yanajidhirisha hapa kwamba mwenye kidogo atapokonywa hata hicho kidogo alichonacho, na mwenye nacho ataongezewa juu ya kile alicho nacho. Goli tu la mama ni milioni tano, hilo ni goli tu. Nyie mnajipendekeza kwa milioni moja kama sio kujichoresha. Mtahangaika sana. Tunajua mwisho wa vioja hivi humalizika baada ya baraza jipya la Mawaziri kutangazwa lkn kwa kipindi hiki ni vioja juu ya vioja.
 
Back
Top Bottom